Kurutu wa Mungu
JF-Expert Member
- Oct 23, 2017
- 366
- 571
Wana JF, miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa kwa wazazi hususani wanaokaa mijini kuwapeleka wahitimu wa darasa la saba kusoma masomo ya sekondari kama maandalizi maarufu kama Pre form one.
Kwa upande wangu naona kama nikuwapotezea mda vijana, maana wakishafungua shule kuanza kidato cha kwanza walimu huwa wanaanzia kufundisha utangulizi (introduction) kwa kila somo nakujikuta wakirudia kile kile walichojifunza huko mitaani, huku tatizo kubwa kwao likiwa ni kuandika, kusoma na kuongea lugha ya Kiingereza.
Ni bora wangekuwa wanatumia vizuri muda wanaokaa nyumbani kujifunza Kiingereza, juzi nimekutana na vijana wanne wanatoka huko wanakosoma Pre form one, nimesikitika ata kujitambulisha kwa Kiingereza hawajui, nikawauliza maswali madogo juu ya kile walichosoma ata kutamka hayo maneno yaliwashinda, nikaona kuna umuhimu wazazi na wadau wanaowafundisha hawa vijana kuanza kujikita kuwasadia katika lugha ya kiingereza ili kuwapa mwanga pindi watakapoanza masomo ya sekondari wasiwe wagumu na wazito katika kuelewa na inaweza kuwa chachu kwao kuanza kupenda kufanya mazoezi ya kuongea Kiingereza wawapo mashuleni.
Kwa upande wangu naona kama nikuwapotezea mda vijana, maana wakishafungua shule kuanza kidato cha kwanza walimu huwa wanaanzia kufundisha utangulizi (introduction) kwa kila somo nakujikuta wakirudia kile kile walichojifunza huko mitaani, huku tatizo kubwa kwao likiwa ni kuandika, kusoma na kuongea lugha ya Kiingereza.
Ni bora wangekuwa wanatumia vizuri muda wanaokaa nyumbani kujifunza Kiingereza, juzi nimekutana na vijana wanne wanatoka huko wanakosoma Pre form one, nimesikitika ata kujitambulisha kwa Kiingereza hawajui, nikawauliza maswali madogo juu ya kile walichosoma ata kutamka hayo maneno yaliwashinda, nikaona kuna umuhimu wazazi na wadau wanaowafundisha hawa vijana kuanza kujikita kuwasadia katika lugha ya kiingereza ili kuwapa mwanga pindi watakapoanza masomo ya sekondari wasiwe wagumu na wazito katika kuelewa na inaweza kuwa chachu kwao kuanza kupenda kufanya mazoezi ya kuongea Kiingereza wawapo mashuleni.