Ngurumo acha kumchafua JK baada ya kukunyima nafasi Ikulu

na wewe prove kama hawana ugomvi binafsi

Majibu yako haya hapa chini. Hii ni makala moja mnayoilalamikia, na mdau kaamua kuprove ukweli wa hoja za Ngurumo.

Hebu tuangalia mambo mengi aliyosema Ngurumo kama yana uongo, tutajua:

"Chuki ya wazi dhidi ya CCM inasababishwa na maisha magumu waliyonayo wananchi. Udhaifu wa serikali ndio umekiua CCM, maana kimegeuka chama cha viongozi waongo, wasioaminika." TRUE KABISA!


"Ile jeuri ya wanachama na mashabiki wa CCM kutembea kifua mbele wakiwa wamevaa mashati na fulana na kijani na njano mitaani, imenyauka." TRUE KABISA, mfano ni baba yangu mzazi, japo ccm siku hizi hata Tshirt ya kijani ukimnunulia havai!

"Hii ndiyo sababu inayowafanya CCM kuandaa mikutano ya hadhara kwa gharama kubwa mno, ikuhusisha kubeba wananchi kwenye malori na mabasi kutoka sehemu za mbali na kuwaleta mahali pa mkutano, tena baada ya kuwaahidi au kuwagawia pesa au fadhila nyinginezo." TRUE KABISA! imekuwa jadi! hadi kuhudhuria kwenye mikutano ya shina, tawi au kata wanadai posho!

"Sasa hivi hata watoto wadogo wanasalimiana kwa kunyosha vidole viwili, ishara ya ushindi inayotumiwa CHADEMA" hili halina ubishi, nenda hata mtaania ukutane na uangalie watoto wanaocheza uangalia wangapi utasikia wakisema kidumu, ila utasikia salam ya peoplez!

"Sasa hivi hata watoto wadogo wanasalimiana kwa kunyosha vidole viwili, ishara ya ushindi inayotumiwa CHADEMA" hili halina ubishi, nenda mtaani maeneo wanakocheza watoto uone kama utasikia hata mmoja wao akitamka kidumu chama … na uangalie kama utasikia salaam au alama ya peoplez!



"Shule za sekondari na vyuo vya elimu ya kati na ya juu vimejaa wanafunzi wasiokipenda CCM. Katika mazingira haya, CCM kinazidi kukosa mvuto, na wanachama wa CCM wanazidi kupungua." Hili hata kwenye report yao ya kujivua gamba, waliweka kama kiashiria cha kushuka hadhi mbele ya umma!



"Ni miaka sita ya shida na umaskini unaosababisha chuki ya wananchi dhidi ya Rais Kikwete. Hatujasahau kwamba mwaka 2005 Kikwete aliomba kura akiahidi maisha bora kwa kila Mtanzania. Yako wapi? " TRUE KABISA maana hata ile kauli mbiu yao ya ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya bila fikra mpya na dira mpya, nayo imekufa kibudu kama ahadi ya maisha bora yenyewe! sasa kwa hili Ngurumo karudia tu mambo ambayo yako wazi, hata anaetumia masaburi kufikiri, na mtumwa wa kuchumia tumbo atayaona!

Ukweli uliowazi ni kuwa ccm imekuwa a disappointment! Imewalet watz down siku ilipoamua kuwatelekeza wakulima na wafanya kazi na kukumbatia matajiri! Hata mwalimu alisema siku ikiacha misingi ya kuanzishwa kwake, basi itakufa! Ndio maana wao wenyewe wanakiri hadhi ya ccm imeporomoka na wakaja na usanii wa kujivua gamba, ambalo sasa limegoma!

Sasa na wewe prove kwamba wana ugomvi binafsi.
 
Mkuu tusaidie kujibu/pangua hoja za Ngurumo ili tuone kwamba anachoandika ni chuki binafsi baada ya kukosa kazi Ikulu.
hakuna hata mmoja aliyej
ibu hoja makini za ngurumo zaidi ya wivu wa baadhi ya waandishi..jamaa anakubalika sana
 
sikutegemea kwamba mtu kama Ansbert Ngurumo angaweza kuandika habari za kumchafua Rais Kikwete na kubeza yote yaliyofanywa na serikali ya chama cha mapinduzi

tutakumbuka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, Ngurumo ni mmoja kati ya watu waliotegemea kupata nafasi ikulu kama shukrani toka kwa Jk na chama cha mapinduzi amekuwa akilalamika kwa muda mrefu baada ya kukosa nafasi hiyo na akasema wazi kupitia mtandao huu wa JF kwamba mtu pekee anayeweza kumshambulia ni Rais Kikwete.
hiyi yule daktari wako wa milembe bado yupo? kama yupo nakushauri kamuone haraka iwezekanavyo au tafuta vile vidonge alivyokuwa amekuandikia . fuata ushauri wangu vinginevyo tutakukuta umebeba suruali kichwani
 
Ngurumo Ansebert,kwa wasio jua unachokiandika mara kadhaa,wape nafasi watukane kwa kadri wajuavyo,na kwa taarifa hawa ni wale ambao wanashiriki kwa kiasi kikubwa kunyonya,kui-fisadi nchi,na wanakula kwa kujikomba kwa magamba.hayo ni maneno ya kutaka kumsafisha JK.kwa taarifa yenu fanyeni ibada zote lakini bila dhamira ya kweli ya kuanchana na ufisadi,siasa za majungu na makundi za sisiemu na uongo uliovuka mipaka wa kuongopea taifa hili maisha bora kwa kila mtanzania,hamwezi kumsafisha kwa kupinga hoja humu jukwaani,maovu ni mengi sana hata ninyi mnayajua,hakuna jambo la kujivunia ambalo ccm imelifanya na hata chini ya mwenyekiti Kikwete tena mpasuko na kuwindana kwa wazi ndani ya CCM kumejitokeza,sasa anaepinga ni kutaka kutuonyesha jinsi gani alivyo na matatizo ya kifra na anahitaiji msaada ama tiba.
Hakuna cha kubisha juu ya uozo wa CCM ya Kikwete unaoonekana katika kila sehemu ya kazi na hakuna anaechukua hatua wala watu hawaogopi kufanya ubadhilifu wa mali ya umma,maana hakuna cha kuwafanya wala hakuna wa kuwakemea nadni ya mfumo wa serikali inayoongozwa na CCM.
Mnaobisha wote rejeeni barua ya mwenyekiti wa CCM mkoani Mara mzee Joseph Butiku,alisema wazi na alitoboa kila kitu lakini hakuna kilichotekelezwa na mwisho wa siku mkaanza kumchukia eti anawasaidia wapinzani.
Ngurumo hongera sana kwa kazi nzuri nami ni mmoja wa wasomaji wazuri wa makala zako.
 
Na Ansbert Ngurumo

BAADHI yetu hatujaelewa ari, nguvu na kasi ya Rais Jakaya Kikwete. Nina hakika naye ameiimba, lakini hajaielewa barabara.

Kaulimbiu hii iliyoasisiwa na kina Samuel Sitta mwaka 2005, ilitumika kumtafutia urais mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya.

Waliomjua vema uwezo na udhaifu wake walidokeza mapema kwamba maisha ya Watanzania chini ya CCM ya Kikwete yangedorora na kuwa magumu zaidi - kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Baadaye, sisi na baadhi ya watani wa CCM tuliifupisha kaulimbiu hiyo, tukaiita ANGUKA. Ni kweli! Miaka mitano baadaye, wameangukia pua.

CCM imeanguka. Rais Kikwete ameanguka. Mtandao wake umeanguka. Na kwa bahati mbaya, hata serikali yake imeanguka, ikaishia kuwa serikali kopa-kopa – hata mishahara ya watumishi – licha ya kodi kubwa tunazolipa.

Kuanguka huku, ndiko kumekuwa chanzo cha kura chache za mgombea urais wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kuanguka huku ndiko kumekuwa kichocheo cha vilio vya wananchi dhidi ya ufisadi. Kuanguka huku ndiko kumesababisha hata usanii mpya wa CCM wa ‘kujivua gamba.'

Kuanguka huku ndiko kumemkosanisha Rais Kikwete na maswahiba wake wa siku nyingi. Kuanguka huku ndiko kumemfanya Rais Kikwete aogope maandamano ya wananchi yanayoratibiwa na CHADEMA hata akalialia kwamba "wanataka kuniondoa kabla ya wakati."

Kuanguka huku ndiko kumemwondoa Yusuf Makamba katika ukatibu mkuu wa CCM, yeye na sekretariati na Kamati Kuu. Kuanguka huku ndiko kumerutubisha na kukuza fitina na vita ya makundi ndani ya CCM.

Kuanguka huku ndiko kumewafanya Watanzania kuikataa CCM waziwazi kuliko wakati wote katika historia, na ndiko kumemwingiza Nape Nnauye (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM) katika migogoro mipya ndani ya makundi ya CCM na kumwandalia anguko lake huko tunakokwenda, hasa baada ya Rais Kikwete kuondoka madarakani.

Anguko hili la ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya limewagusa wananchi wenyewe. Sasa wanakabiliwa na ukali wa maisha usiofanana kabisa na ahadi kemkemu walizopewa na CCM mwaka 2005 na 2010.

Bahati mbaya waliosababisha anguko hili, bado wanajitapa kwamba wameleta maendeleo. Vipofu!

Na kwa sababu ya upofu huu, wanakosa mikakati mipya ya kujikwamua. Wanarudiarudia yale yale yaliyoshindwa kuwanusuru miaka mitano iliyopita.

Kwa mfano, mwaka 2006 mwanzoni, Rais Kikwete aliingia na mbinu ya kutembelea wizara moja moja, kutoa maelekezo na kupiga picha na watumishi wa wizara hizo. Ilikuwa propaganda na mapambo ya magazeti na televisheni.

Baadaye, aliwaita mawaziri na watumishi waandamizi wa serikali (mara mbili) katika semina elekezi kwenye Hoteli ya kifahari, Ngurdoto, Arusha.

Leo tunapotazama nyuma, ni nani anaweza kujivunia semina elekezi za Ngurdoto?

Lakini watu wasiojifunza hawafichiki. Mwaka jana, rais yule yule akagombea kwa kaulimbiu ya ari zaidi, kasi zaidi na nguvu zaidi. Yaani, hawa jamaa hawakuridhika na 'anguko jipya' la 2006. Waliona hilo halitoshi, wakatuandaa "kuanguka zaidi" mwaka 2010!

Haikumwongezea kura mgombea wao. Haikuvuta hisia za vijana wala kina mama. Ili kupata watu wa kuhutubia ilibidi CCM itumie pesa nyingi kuchapisha na kugawa sare, kuwagawia watu na kuwapakia kwenye magari kuwapeleka kwenye mikutano ya mbali.

Haikuwaunganisha watawala wawe na sauti moja, hata baada ya kurejea madarakani. Haikuwasaidia kupata hekima ya kumaliza matatizo ya muda mrefu, kama ukosefu wa umeme ambao umezungumzwa tena na tena bila ufumbuzi.

Sasa kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, watawala wamerudi tena katika semina elekezi, chini ya mwelekezaji yule yule.

Walidhani zile zilishindikana kwa sababu zilifanyika Arusha. Sasa wamekimbilia Dodoma. Kwa wiki nzima, serikali iko Dodoma, imelala; inakula posho. Kazi zinakwama.

Rais naye, badala ya kuwaelekeza kwa hekima na ustadi, "akawananga" wasaidizi wake hadharani, kana kwamba huwa hapati fursa ya kukutana nao – wakati amekuwa akikutana nao kila mwezi katika vikao vya Baraza la Mawaziri. Ndio hao aliowatembelea na kuwasema wizarani kwao miezi miwili iliyopita, hata akawaamuru wengine waache ubabe.

Alitaka kuonewa huruma. Alitaka kuwashitaki kwa wananchi – waonekane wabaya, awe mzuri.

Rais anawasema mawaziri wake kama watoto wadogo wanaohangaika kuelewa kitu kidogo anachowafundisha. Anawaonyesha wananchi kwamba ana mawaziri mizigo, mbumbumbu – ambao kazi pekee wanayofanya ni "kumwangusha" rais.

Anataka turudi kwenye propaganda za kijinga walizoimba miaka mitano iliyopita, kwamba rais pekee ndiye anachapa kazi, bali mawaziri wake wanamwangusha.

Anawaambia mawaziri wake kuwa kama hawawezi kazi "waondoke," kana kwamba hajui uwezo wao, hajui waliingiaje, wakati ndiye aliyewateua na ndiye ana mamlaka ya kuwaondoa.

Anataka "watoke" waende kwa wananchi kufafanua mafanikio ya serikali yake. Haamini kwamba wananchi wana uwezo wa kuona mazuri na mabaya ya serikali – bila kusubiri taarifa za mawaziri.

Haoni kwamba serikali inayofilisika na kulazimika kukopa hata mishahara ya watumishi wake, inahitaji kubana matumizi na kupunguza ziara na posho nono za viongozi hao waandamizi.

Lakini pia, tunapowatazama watu wenyewe aliokuwa anawapa somo, tunabaki kujiuliza: Rais amepata wapi hekima hii ya kudhani ana uelewa mpana kuliko mawaziri wake?

Amesomea wapi huko wasikojua wao, alikopata hicho cha kuwafunda? Tunapowatazama baadhi yao tunagundua kwamba kama rais angekuwa na busara ya kujifunza kutokana na miaka mitano iliyopita, asingewaita mawaziri kuwafunda, bali angewaita ili wakae kama timu, awaombe ushauri, awasikilize, wampe mang'amuzi yao na mipango mkakati; naye baada ya kuwasikiliza na kuongeza maono yake, awapangie kazi na kuwadai matokeo baada ya muda kadhaa.

Au basi angeunda kikosi kazi cha wasomi waliokubuhu kutoka taasisi mbalimbali zinazoheshimika, akawakutanisha na wasaidizi wake, wote pamoja wakavuna maarifa ya ziada katika kuboresha kazi zao na kukosoa kasoro za huko nyuma.

Angejenga mazingira ya kuambizana ukweli, naye akaambiwa kasoro zake; hasa kwamba serikali imekosa mipango mkakati mbadala na hata hiyo iliyopo imekosa msimamizi makini.

Kitendo cha rais kulialia mbele ya wateule wake na wananchi kupitia vyombo vya habari si ishara ya ushupavu anaostahili kuwa nao kiongozi mkuu wa nchi.

Ndiyo! Tuliona wameinama na kushika tama alipokuwa anafoka. Lakini ana uhakika gani kwamba walikubaliana naye? Ana uhakika gani kwamba walimwona shujaa?

Na kwa kiongozi ambaye ameongoza nchi kwa miaka mitano kwa hotuba na matamko yasiyotekelezeka, anadhani mawaziri wake watamwamini na kumheshimu baada ya kufokewa hadharani Dodoma?

Labda, watamshukuru kwa kuwatengenezea mazingira ya kula posho za safari. Lakini naamini mawaziri wenyewe wanajua fika kwamba hawana sababu ya kusafiri hadi vijijini kila mara, maana huko kuna watendaji wa ngazi za chini wanaopaswa kusimamia kazi na kuleta taarifa kwa ngazi za juu.

Sasa kama rais anaagiza mawaziri waende wenyewe vijijini, hao watendaji wa mikoani, wilayani na vijijini kwenyewe watafanya kazi gani?

Hivi waziri aliyekaa katika wizara ile ile kwa miaka mitatu au zaidi, ana kitu gani cha kujifunza kwa rais aliyekaa madarakani kwa miaka mitano bila maono na mafanikio yanayoshikika?

Rais Kikwete ana mfano gani wa utendaji uliotukuka anaoweza kuutumia kuwasuta mawaziri wake? Aliacha urithi gani katika wizara alizowahi kuongoza kabla hajawa rais?

Ni nani anayejua matatizo, changamoto, na suluhisho la matatizo yake, kati ya waziri aliye kwenye wizara hiyo hiyo, na rais "anayeishi kwenye ndege?"
Baadhi yetu tunajua kwamba mkwamo mkubwa wa kiutendaji unatokana na madaraka makubwa ya rais, nidhamu ya woga ya wasaidizi wake na utovu wa uzalendo wa baadhi yao.

Zipo taarifa kwamba siku hizi wasaidizi wa rais wameamua kumwambia yale anayotaka kusikia, kwa sababu anawafokea hovyo hovyo wanapomweleza asiyotaka, au wanapompa mapendekezo magumu.

Wanadai rais hataki kuambiwa asichotaka; nao hawako tayari kupoteza kazi zao.

Kwa mantiki hii, haiwezekani kwamba baadhi ya wasaidizi wa rais wana nafuu kuliko yeye? Kwanini tusiamini, basi, kwamba rais ndiye anawaangusha wasaidizi wake?
 
Ngurumo anatupeleka kusiko huwezi kujadili ajenda ya mtu mmoja kwa muda mrefu kiasi hicho na kuacha mambo mengi ya msingi kwa maslahi ya nchi kwani ajenda ya Ngurumo inaacha mambo kadhaa ambayo tunatakiwa kuyaweka sawa bila kujali Jk tunamkubali au la
Wacha kuleta uhuni wako hapa, huwezi kumuita Jk ni mtu mmoja, JK anawakilisha taasisi mbili yaani Uraisi na Uenyekiti wa CCM, hivyo kujadiliwa kwake kwa muda mrefu ni halali kabisa. Lakini kwa wachumia tumbo mnaojipendeza kwake JK(personaly) mnaona kama anaonewa. Hoja ya msingi hapa mtuonesha wapi Ngurumo alipokosea. Cha ajabu hamfanyi hivyo, mnalia lia tu. Mtuonesheni chuki ya Ngurumo dhidi ya JK wenu basi na sio kujadili urefu wa muda anaokoselewa Kilaza wenu. Mbona atakaa miaka minne zaidi madarakani kuanzia sasa, kwahiyo asijadiriwe na kuchambuliwa kwa udhaifu wake ati kwa sababu miaka minne ni muda mrefu? Ansbart Ngurumo, kaza uzi weka mambo hadharani, ili waandishi uchwara wajifunze.
 
Ngurumo alipolipiwa shule uingereza na mwenyekiti wa chama fulani alipewa jukumu la kummaliza kikwete lakini hataweza atakuwa Rais wake hadi 2015
Kumbe hampo hapa kujadili hoja ila wivu na majungu !!Mwambieni Kikwete wenu, mpaka 2015 atakuwa ametuumiza watanzania kiuchumi kupita kiasi. Watumishi wa umma kupunguziwa mishahara yao kimyakimya halijasababishwa na Ngurumo, wala watu wakawaida kushindwa kununua sukari hawahitaji kuambiwa na Ngurumo, wafanyabiashara kuficha mafuta nakusababisha gharama za usafirishaji kupanda hawa ambiwi na Ngurumo, thamani ya shilingi yetu kushuka kila kukicha na gharama za maisha kupanda kila kukicha hakusubiri kalamu ya Ngurumo. Washenzi wakubwa nyie, msituongezeeni hasira, wachawi msie na huruma nyie, wanafiki msie na mishipa ya aibu. Wasengenyaji msio maana.
 
Yaliyofanywa yepi hayo?

Au ni ile list ndefu ya data za Megawati zitakazojengwa 2014?

Hongera sana Ansbert kwa kuwa mwandishi huru, na kuheshimu fani ya habari!
Mkuu pakajimmy jamaa ni mganga njaa tu. hivi kuna mtu aliekuwa na wasiwasi na silva rwaimamu? si ndo yule aliyekuwa akimwandika mkapa kwa mabaya kila kukicha? sasa mnamwonaje kwenye jamii. Ndo yule unayemfahamu?
Nikijuacho ni kuwa waandishi wengi wahabari ni njaa na ni form4 failier. sijali kutukanwa nikiwa nasimamia ukweli. kwahiyo akipata kanafasi tu anataka apitie hapo. Umesahau akina kibonde walivyokuwa wakimpigia Kikwete kampeni uchaguzi uliopita halafu wakawa wanaongea kwa mafumbo kuwa usishangae mtu hapa mara kaukwaa ukuu wa mkoa? Think twice.
 
sikutegemea kwamba mtu kama Ansbert Ngurumo angaweza kuandika habari za kumchafua Rais Kikwete na kubeza yote yaliyofanywa na serikali ya chama cha mapinduzi

tutakumbuka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, Ngurumo ni mmoja kati ya watu waliotegemea kupata nafasi ikulu kama shukrani toka kwa Jk na chama cha mapinduzi amekuwa akilalamika kwa muda mrefu baada ya kukosa nafasi hiyo na akasema wazi kupitia mtandao huu wa JF kwamba mtu pekee anayeweza kumshambulia ni Rais Kikwete.

Sijaelewa amemshambuliaje? Unapoanza habari eleza kiini cha habari hiyo ili kila mtu awe tayari kuchangia
 
sikutegemea kwamba mtu kama Ansbert Ngurumo angaweza kuandika habari za kumchafua Rais Kikwete na kubeza yote yaliyofanywa na serikali ya chama cha mapinduzi

tutakumbuka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, Ngurumo ni mmoja kati ya watu waliotegemea kupata nafasi ikulu kama shukrani toka kwa Jk na chama cha mapinduzi amekuwa akilalamika kwa muda mrefu baada ya kukosa nafasi hiyo na akasema wazi kupitia mtandao huu wa JF kwamba mtu pekee anayeweza kumshambulia ni Rais Kikwete.

Tupe detailed information to prove your comments,otherwise you will be among stupid people in Tanzania....
 
sikutegemea kwamba mtu kama Ansbert Ngurumo angaweza kuandika habari za kumchafua Rais Kikwete na kubeza yote yaliyofanywa na serikali ya chama cha mapinduzi

tutakumbuka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, Ngurumo ni mmoja kati ya watu waliotegemea kupata nafasi ikulu kama shukrani toka kwa Jk na chama cha mapinduzi amekuwa akilalamika kwa muda mrefu baada ya kukosa nafasi hiyo na akasema wazi kupitia mtandao huu wa JF kwamba mtu pekee anayeweza kumshambulia ni Rais Kikwete.

oh,ina maana ANAZUSHIWA?
 
Wacha kuleta uhuni wako hapa, huwezi kumuita Jk ni mtu mmoja, JK anawakilisha taasisi mbili yaani Uraisi na Uenyekiti wa CCM, hivyo kujadiliwa kwake kwa muda mrefu ni halali kabisa. Lakini kwa wachumia tumbo mnaojipendeza kwake JK(personaly) mnaona kama anaonewa. Hoja ya msingi hapa mtuonesha wapi Ngurumo alipokosea. Cha ajabu hamfanyi hivyo, mnalia lia tu. Mtuonesheni chuki ya Ngurumo dhidi ya JK wenu basi na sio kujadili urefu wa muda anaokoselewa Kilaza wenu. Mbona atakaa miaka minne zaidi madarakani kuanzia sasa, kwahiyo asijadiriwe na kuchambuliwa kwa udhaifu wake ati kwa sababu miaka minne ni muda mrefu? Ansbart Ngurumo, kaza uzi weka mambo hadharani, ili waandishi uchwara wajifunze.
Ngurumo junior...mhhhhh bila shaka ni form4 failure.
 
sikutegemea kwamba mtu kama Ansbert Ngurumo angaweza kuandika habari za kumchafua Rais Kikwete na kubeza yote yaliyofanywa na serikali ya chama cha mapinduzi

tutakumbuka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, Ngurumo ni mmoja kati ya watu waliotegemea kupata nafasi ikulu kama shukrani toka kwa Jk na chama cha mapinduzi amekuwa akilalamika kwa muda mrefu baada ya kukosa nafasi hiyo na akasema wazi kupitia mtandao huu wa JF kwamba mtu pekee anayeweza kumshambulia ni Rais Kikwete.

Wewe mbumbumbu achana na spin zako hizo, hakuna mtu anayemchafua Kikwete bali amejichafua mwenyewe kwa kuleta usanii serikalini;mwandishi wa hadhi kama ya Ansbert Ngurumo hawezi kuomba/kufanya kazi Ikulu ya mkweree kwani hawaendani sawasawa kiakili!! Je unaweza kuwalinganisha Ansbert na watu kama Salva Rweyemamu na Shoo,it is impossible ni sawa nakulinganisha usiku na mchana. Usifikiri kwa uongo huu unaweza kumchafua Ansbert, tunaomfahamu kwa uandishi wake tunamthamini na nyie mkae na umercenary wenu na mwisho mtakujajuta!!
 
Kinachoiangamiza Tanzania ni kila mtu kujifanya anajua hata kama hajui. Wengi wamemshambulia Ngurumo na kuacha kujibu hoja zake. Hii maana yake ni kwamba hawana hoja au ni vihiyo wa kawaida wanaojitia kujua wakati hawajui. Hawa wanaodai wanampenda Kikwete hawana maana zaidi ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kujikomba. Kama si kujikomba basi ni wale nepi zake anazolipa kumsafisha kwa kila uchafu alionao. Kwa wenye akili ni kwamba Kikwete ni mchafu kuliko unavyoweza kudhani. Kila siku utamuona Muhimbili kuwajulia hali wagonjwa. Lakini rais huyo huyo hana muda wa kwenda vijijini kuhimiza na kukagua maendeleao. Wanaojua alivyotolewa mkuku Mbeya wanajua ni kwanini hataki kwenda vijijini ukiachia mbali tabia yake ya kupenda kuzurura nje na mkewe. Sasa wazungu wamemchoka wanataka tigo! Msiseme natukana. Kumwambia rais aandae mazingira mazuri kwa mashoga ni kumwita shoga. Wale wanaodai Kikwete alikataa kumpokea balozi shoga nao wanafikiri kwa masaburi. Kama ni kweli mbona Membe aliyetunga huu usanii hakumtaja zaidi ya kujikomba kwa bosi wake. Pia wanaodai Ngurumo ni mtoto si riziki nina wasi wasi nao. Ngurumo hawezi kufanya kazi ya Salva bali kuandika anachojua na kuamini. Kama kumuandika Kikwete wasivyopenda waramba viatu wake naye mbona tuko wengi. Wale wanaodhani kuandika ni rahisi si waandike yao tuyasome tuwachambue. Nimalizie kwa kusema kuwa Kikwete hachukiwi bali anapendwa kwa kuambiwa ukweli. Sema watanzania huwa wengi hawapendi kuambiwa ukweli kwa vile unauma.
 
Wakuu nadahani ingekuwa vema basi tukaletewa list ya waandishi wanaotakiwa/ wanaofaa kuandika madhaifu ya JK maana imekuwa ni destruri siku hizi kwa baadhi ya watu hasa mashabiki wa CCM kumbatiza kila jina ovu yeyote anayeandika udhaifu wa JK, CCM na serikali yake. Misemo kama "ana njaa", "kutafuta umaarufu" si migeni kutoka kwa mashabiki wa CCM kumtuhumu yeyote anayeanika udhaifu wa JK, CCM na serikali. Hivyo basi ni vema vigezo vya nani anastahili kukosoa na kuonyesha udhaifu vikawekwa wazi.
 
Back
Top Bottom