Hemed Maronda
Senior Member
- Oct 27, 2010
- 138
- 43
Ni jambo la kusikitisha kidogo lakini ndiyo ukweli wenyewe.
Leo asubuhi nimetoka Bagamoyo kuelekea Jijini,nikiwa kwenye shughuli zangu za kawaida za kibiashara,baada ya kuona nimeshindwa kumaliza shughuli zangu kwa leo nikaamua kulala. Jambo nililokutana nalo ndilo limenilazimu kuleta uzi huu angalau na wenzangu muchangie.
Nimezunguka Mbagala - Zakhieem ili nipate Guest House nipumzike,cha ajabu nilichokutana nacho! Nimetembelea Guest House 10 zote nakuta vibao pale nje vinanielekeza kuwa Vyumba Vipo lakini nikiingia ndani na kuwaona Wahudumu naambiwa kuwa hakuna Chumba kwa Mgeni anaetaka kulala,ila kuna vyumba kwa wale wanaohitaji huduma ya muda mfupi ama "short time" mwanzo sikuamini nilichokuwa naambiwa ila kila nikiondoka kutoka Guest moja mpaka nyingine bado majibu niliyokuwa nayapata ni hayohayo. Nilizidi kuwa mdadisi nifahamu nini kilichojiri mpaka kupelekea hali hii? Bahati nzuri wakati naifikia Guest House ya 11 nikamkuta dada mmoja ambae ni Mhudumu kwenye Guest hiyo,nikamuuliza kulikoni nimekosa chumba cha kulala kwenye Guest 10 pamoja na hiyo ambayo nilikuwapo? Yule dada hakuwa na hiyana akaanza kunipa maelekezo kwa nini kuna hali kama hiyo,alichonieleza kuwa toka pale DAR LIVE ilipofunguliwa pale Mbagala - Zakhiem mauzo ya Guest zote ambazo ziko karibu na Dar Live yameongezeka tena hasa hasa siku za Jumamosi na Jumapili,tena si kwa wateja wa kulala bali wateja wa "short time" ambao kwa chumba kimoja tu wanaweza kutumia mpaka watu 10 kwa siku na kila matumizi ya mara moja gharama ni Tshs 5,000/= sasa wamiliki wa Guest wanaona ni heri siku za wikiendi wafanye biashara za muda mfupi kuliko kumpa chumba mtu wa kulala,jambo ambalo siyo sahihi ni kinyume na madhumuni ya kutolewa Leseni za biashara hiyo,pia tujiulize kuna ngono salama inayoendelea huko ndani?
Nawasilisha wadau tujadili.
Leo asubuhi nimetoka Bagamoyo kuelekea Jijini,nikiwa kwenye shughuli zangu za kawaida za kibiashara,baada ya kuona nimeshindwa kumaliza shughuli zangu kwa leo nikaamua kulala. Jambo nililokutana nalo ndilo limenilazimu kuleta uzi huu angalau na wenzangu muchangie.
Nimezunguka Mbagala - Zakhieem ili nipate Guest House nipumzike,cha ajabu nilichokutana nacho! Nimetembelea Guest House 10 zote nakuta vibao pale nje vinanielekeza kuwa Vyumba Vipo lakini nikiingia ndani na kuwaona Wahudumu naambiwa kuwa hakuna Chumba kwa Mgeni anaetaka kulala,ila kuna vyumba kwa wale wanaohitaji huduma ya muda mfupi ama "short time" mwanzo sikuamini nilichokuwa naambiwa ila kila nikiondoka kutoka Guest moja mpaka nyingine bado majibu niliyokuwa nayapata ni hayohayo. Nilizidi kuwa mdadisi nifahamu nini kilichojiri mpaka kupelekea hali hii? Bahati nzuri wakati naifikia Guest House ya 11 nikamkuta dada mmoja ambae ni Mhudumu kwenye Guest hiyo,nikamuuliza kulikoni nimekosa chumba cha kulala kwenye Guest 10 pamoja na hiyo ambayo nilikuwapo? Yule dada hakuwa na hiyana akaanza kunipa maelekezo kwa nini kuna hali kama hiyo,alichonieleza kuwa toka pale DAR LIVE ilipofunguliwa pale Mbagala - Zakhiem mauzo ya Guest zote ambazo ziko karibu na Dar Live yameongezeka tena hasa hasa siku za Jumamosi na Jumapili,tena si kwa wateja wa kulala bali wateja wa "short time" ambao kwa chumba kimoja tu wanaweza kutumia mpaka watu 10 kwa siku na kila matumizi ya mara moja gharama ni Tshs 5,000/= sasa wamiliki wa Guest wanaona ni heri siku za wikiendi wafanye biashara za muda mfupi kuliko kumpa chumba mtu wa kulala,jambo ambalo siyo sahihi ni kinyume na madhumuni ya kutolewa Leseni za biashara hiyo,pia tujiulize kuna ngono salama inayoendelea huko ndani?
Nawasilisha wadau tujadili.