kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
BAADHI ya vurugu za kisiasa zinazotokea hapa nchini zimedaiwa kuchochewa na wafadhili wa nje kwa kutoa fedha nyingi.
Akizungumza Dar es Salaam jana Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utawala Bora na Maendeleo Tanzania (CEGODETA), Thomas Ngawaiya aliwataka wafadhili hao kuheshimu uamuzi wa Watanzania vinginevyo wanaweza kusababisha machafuko.
Uchaguzi mkuu umekwisha na Watanzania wameshafanya uamuzi, tunawaomba wafadhili wa nje hususani wa Ulaya na Marekani, waache kuingilia mambo ya ndani ya nchi yetu ikiwa ni pamoja na kutuchagulia viongozi, alisema.
Alitoa mwito kwa Serikali kuangalia namna ya kuchukua hatua kwa wageni wanaotoa fedha kwa ajili ya vurugu za kisiasa na washirika wao ili kulinda heshima na amani ya nchi.
Pia aliwataka Watanzania kuwa makini kwa kukataa kushawishiwa na watu hao wenye nia ovu ili kudumisha amani, utulivu, umoja na mshikamano kwa maslahi ya Taifa na vizazi vijavyo.
Kuhusu Polisi, alilitaka Jeshi hilo kutumia mbinu za kisasa wakati wa kuzuia maandamano na kuepuka kutumia nguvu kupita kiasi hali ambayo inasababisha mauaji kwa watu wasiokuwa na hatia.
Aidha mwanasiasa huyo ameishauri Serikali kutolipa deni la Kampuni ya Dowans kwa sababu si deni halali na endapo litalipwa linaweza kufilisi nchi na wananchi wakakosa huduma muhimu.
Tanzania ingejiondoa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Biashara kwani Mahakama hiyo mara kwa mara hutoa hukumu mbaya dhidi ya nchi yetu kama ilivyofanya kwenye suala la IPTL ambapo hadi leo tunalipa zaidi ya Sh bilioni nne kila mwezi, alisema Ngawaiya.
Akizungumza Dar es Salaam jana Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utawala Bora na Maendeleo Tanzania (CEGODETA), Thomas Ngawaiya aliwataka wafadhili hao kuheshimu uamuzi wa Watanzania vinginevyo wanaweza kusababisha machafuko.
Uchaguzi mkuu umekwisha na Watanzania wameshafanya uamuzi, tunawaomba wafadhili wa nje hususani wa Ulaya na Marekani, waache kuingilia mambo ya ndani ya nchi yetu ikiwa ni pamoja na kutuchagulia viongozi, alisema.
Alitoa mwito kwa Serikali kuangalia namna ya kuchukua hatua kwa wageni wanaotoa fedha kwa ajili ya vurugu za kisiasa na washirika wao ili kulinda heshima na amani ya nchi.
Pia aliwataka Watanzania kuwa makini kwa kukataa kushawishiwa na watu hao wenye nia ovu ili kudumisha amani, utulivu, umoja na mshikamano kwa maslahi ya Taifa na vizazi vijavyo.
Kuhusu Polisi, alilitaka Jeshi hilo kutumia mbinu za kisasa wakati wa kuzuia maandamano na kuepuka kutumia nguvu kupita kiasi hali ambayo inasababisha mauaji kwa watu wasiokuwa na hatia.
Aidha mwanasiasa huyo ameishauri Serikali kutolipa deni la Kampuni ya Dowans kwa sababu si deni halali na endapo litalipwa linaweza kufilisi nchi na wananchi wakakosa huduma muhimu.
Tanzania ingejiondoa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Biashara kwani Mahakama hiyo mara kwa mara hutoa hukumu mbaya dhidi ya nchi yetu kama ilivyofanya kwenye suala la IPTL ambapo hadi leo tunalipa zaidi ya Sh bilioni nne kila mwezi, alisema Ngawaiya.