Ndugu Zangu,
Pichani ni ' Chifu' wa mtandao wa Tanzanet, Mzee Yussuf Kalala. Nilikutana nae Dar jana. Tuliongea kwa kirefu. Mzee Kalala ana mengi ya kuelimisha, ikiwamo maarifa ya kihistoria. Ameishi Washington DC kwa miaka mingi. Tumefahamiana tangu enzi za mtandao wa Tanzanet ya miaka 1998 na kuendelea. Nakumbuka nilivyoingia Tanzanet kwa mara ya kwanza ni pale Ben Mkapa alipotembelea Sweden mwaka 1998.
Watanzania tulialikwa nyumbani kwa Balozi Samson Kasekka jioni moja, kwa chakula na vinywaji. Na hapo alikuwepo Mkapa na Waziri wake wa Mambo ya Nje, Jakaya Kikwete.
Mkapa aliongea machache sana, kisha akaondoka zake na hatukumwona tena, nyuma alimwacha Kikwete akiongea na Watanzania. Na katika machache aliyosema Mkapa nakumbuka alitamka; " Na kule kwenye mtandao wa Tanzanet kuna watu kazi yao ni kusema mambo ya umbea umbea tu!". Kwa kufanya hivyo, Mkapa akawa ameitangaza Tanzanet ambayo hata mimi sikuijua wakati huo.
Nilipofika nyumbani tu , cha kwanza ni kuitafuta Tanzanet na kujiunga nayo, si kwa sababu wanasema umbea umbea, bali ni kufahamu kuwa wanaosema umbea ni wengi, lakini ukimwona Rais anakasirika hadharani juu ya umbea wa watu fulani, basi ujue, ndani yake kuna yasiyo ya umbea. Ni ya ukweli. Na mwanadamu siku zote awe na kiu ya kuutafuta ukweli.
Na wanadamu tumejaliwa akili ili tuweze kufikiri. Na kufikiri ndio njia mojawapo ya kuiteka kweli. Kufikiri kunahamisha milima na hata kuiweka kando kuruhusu mwanga upite. Inakuwaje basi mwanadamu anapoacha kufikiri?Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid,
Dar es Salaam
Jumatano, Mei 18, 2011
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo
Pichani ni ' Chifu' wa mtandao wa Tanzanet, Mzee Yussuf Kalala. Nilikutana nae Dar jana. Tuliongea kwa kirefu. Mzee Kalala ana mengi ya kuelimisha, ikiwamo maarifa ya kihistoria. Ameishi Washington DC kwa miaka mingi. Tumefahamiana tangu enzi za mtandao wa Tanzanet ya miaka 1998 na kuendelea. Nakumbuka nilivyoingia Tanzanet kwa mara ya kwanza ni pale Ben Mkapa alipotembelea Sweden mwaka 1998.
Watanzania tulialikwa nyumbani kwa Balozi Samson Kasekka jioni moja, kwa chakula na vinywaji. Na hapo alikuwepo Mkapa na Waziri wake wa Mambo ya Nje, Jakaya Kikwete.
Mkapa aliongea machache sana, kisha akaondoka zake na hatukumwona tena, nyuma alimwacha Kikwete akiongea na Watanzania. Na katika machache aliyosema Mkapa nakumbuka alitamka; " Na kule kwenye mtandao wa Tanzanet kuna watu kazi yao ni kusema mambo ya umbea umbea tu!". Kwa kufanya hivyo, Mkapa akawa ameitangaza Tanzanet ambayo hata mimi sikuijua wakati huo.
Nilipofika nyumbani tu , cha kwanza ni kuitafuta Tanzanet na kujiunga nayo, si kwa sababu wanasema umbea umbea, bali ni kufahamu kuwa wanaosema umbea ni wengi, lakini ukimwona Rais anakasirika hadharani juu ya umbea wa watu fulani, basi ujue, ndani yake kuna yasiyo ya umbea. Ni ya ukweli. Na mwanadamu siku zote awe na kiu ya kuutafuta ukweli.
Na wanadamu tumejaliwa akili ili tuweze kufikiri. Na kufikiri ndio njia mojawapo ya kuiteka kweli. Kufikiri kunahamisha milima na hata kuiweka kando kuruhusu mwanga upite. Inakuwaje basi mwanadamu anapoacha kufikiri?Na hilo ni Neno La Leo.
Maggid,
Dar es Salaam
Jumatano, Mei 18, 2011
MJENGWA - Picha, Habari & Matangazo