NEC yatangaza Uchaguzi Kata 37. Yateua Madiwani watatu wa viti maalumu

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo katika kata 37 za Tanzania bara zilizopo katika halmashauri 27 nchini, ikieleza kuwa uchaguzi huo utafanyika Oktoba 13, 2018.

Akitangaza uchaguzi huo leo Alhamisi Septemba 13, 2018, mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema fomu za uteuzi wa wagombea katika uchaguzi huo zitatolewa kati ya Septemba 15 hadi 21, 2018.

Amesema uteuzi wa wagombea utafanyika Septemba 21, 2018 na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia Septemba 22 hadi Oktoba 12.

Amebainisha kuwa uchaguzi huo unafanyika baada ya NEC kupokea taarifa ya uwepo wa nafasi wazi za udiwani.

Wakati huo huo, NEC imewateua madiwani watatu wa Viti Maalum kujaza nafasi zilizo wazi.

Jaji Kaijage amewataja madiwani hao kuwa ni Halima Kisenga (CCM) katika halmashauir ya wilaya ya Kigamboni.

Emmy Shemweta kupitia CCM katika halmashauri ya Wilaya ya Lushoto na Nuru Mwalimu Chuma (CUF) katika halmashauri ya manispaa ya Ilala.
 
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi - JAJi... Duh!

Unaweza fikiri kwa vile mkuu wa tume ni jaji, chaguzi zitakuwa za haki..!
 
watanzania hatuitaji uchaguzi usio huru na haki.ili kupunguza gharama ni vyema wangewapitisha wagombea wote wa ccm maana tumeshazoea na tunajua ndivyo itakavyokuwa.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo katika kata 37 za Tanzania bara zilizopo katika halmashauri 27 nchini, ikieleza kuwa uchaguzi huo utafanyika Oktoba 13, 2018.

Akitangaza uchaguzi huo leo Alhamisi Septemba 13, 2018, mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema fomu za uteuzi wa wagombea katika uchaguzi huo zitatolewa kati ya Septemba 15 hadi 21, 2018.

Amesema uteuzi wa wagombea utafanyika Septemba 21, 2018 na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia Septemba 22 hadi Oktoba 12.

Amebainisha kuwa uchaguzi huo unafanyika baada ya NEC kupokea taarifa ya uwepo wa nafasi wazi za udiwani.

Wakati huo huo, NEC imewateua madiwani watatu wa Viti Maalum kujaza nafasi zilizo wazi.

Jaji Kaijage amewataja madiwani hao kuwa ni Halima Kisenga (CCM) katika halmashauir ya wilaya ya Kigamboni.

Emmy Shemweta kupitia CCM katika halmashauri ya Wilaya ya Lushoto na Nuru Mwalimu Chuma (CUF) katika halmashauri ya manispaa ya Ilala.
Wawatangaze tu washindi wagombea wote wa ccm ili kunusuru pesa na watu kuumia kwa vipigo,hizo drama za uchaguzi tumeshazichoka.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo katika kata 37 za Tanzania bara zilizopo katika halmashauri 27 nchini, ikieleza kuwa uchaguzi huo utafanyika Oktoba 13, 2018.

Akitangaza uchaguzi huo leo Alhamisi Septemba 13, 2018, mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema fomu za uteuzi wa wagombea katika uchaguzi huo zitatolewa kati ya Septemba 15 hadi 21, 2018.

Amesema uteuzi wa wagombea utafanyika Septemba 21, 2018 na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia Septemba 22 hadi Oktoba 12.

Amebainisha kuwa uchaguzi huo unafanyika baada ya NEC kupokea taarifa ya uwepo wa nafasi wazi za udiwani.

Wakati huo huo, NEC imewateua madiwani watatu wa Viti Maalum kujaza nafasi zilizo wazi.

Jaji Kaijage amewataja madiwani hao kuwa ni Halima Kisenga (CCM) katika halmashauir ya wilaya ya Kigamboni.

Emmy Shemweta kupitia CCM katika halmashauri ya Wilaya ya Lushoto na Nuru Mwalimu Chuma (CUF) katika halmashauri ya manispaa ya Ilala.

WAMEZUIA WATUMISHI WA UMMA KUPANDA MADARAJA TOKEA MWAKA 2016 .WANALETA WARAKA KUTOKA KWA KATIBU MKUU UTUMISHI ETI MADARAJA YATAPANDA KUANZIA MWEZI APRIL 2018.MAAFISA UTUMISHI WANA UPLOAD MAJINA KWENYE LAWSON BAADA YA MUDA UTUMISHI WANAPIGA CHINI MAJINA YOTE WANALETA TENA WARAKA MPYA KUWA WATAPANDISHA MADARAJA WALE AMBAO WAME SUBMITT VYETI TUU,MAAFISA UTUMISHI WANA UPLOAD MAJINA UPYA UTUMISHI WANA DELETE MAJINA YOTE BAADA YA MUDA WANALETA TENA WARAKA MPYA KWAMBA WASUBIRI MPAKA BAJETI IJAYO.ILA MBUNGE AKIHAMA AMA DIWANI AKIHAMA UCHAGUZI MPYA NI WITHIN A MONTH AMBAPO TUNATUMIA GARAMA ZAIDI YA 1.2 BILION KWA UCHAGUZI MMOJA.


SERIKALI YA AWAMU YA 5 KAULI MBIU YETU NI CHAGUZI NA TEUZI KWANZA LAKINI MASLAHI YA MFANYAKAZI AMBAE NDIO HUYO HUYO MNATUMIA KODI ZAKE KWENYE MAUCHAGUZI NA MAUTEUZI TUPA KULE KWA SABABAU WAFANYAKAZI HAWAKUPIGA KURA WALA HAWAKUICHAGUA VERT PARTI POLITIQUE.

EWE MTUMISHI WA UMMA USIVUNJIKE MOYO MUNGU YUPO PAMOJA NA WEWE NJAA HAIUI ILA INATESA TUU KWA MUDA MFUPI MNO.
 
Hiv hizi chaguzi sisizoisha mwisho wake nini ? maana sasa imekuwa nchi ya uchanguzi kila kukicha..hizo pesa zingefanya maendeleo zitujengee miundombinu ya Maji, Barabara na hata vituo vya afya, inachosha sana kwakweli maana idadi kubwa ni wale madiwani waliohama chama kimoja kwenda kingine na tena hao hao wanapewa fursa za kuwa wagombea
 
Back
Top Bottom