NEC imekiuka kanuni za uteuzi wa viti maalum

helu

Member
Feb 28, 2015
86
124
Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Cuf limesikitishwa na hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kujidhalilisha na kujishushia hadhi kwa kushiriki katika hujuma za Dola dhidi ya CUF.

Mbali na kasoro kadhaa, hata kama ingekuwa kufukuzwa Wabunge hao wa CUF kulikuwa ni halali na kumefanywa na chombo halali cha Chama, basi Kanuni walizojiwekea wenyewe Tume katika uteuzi wa watu wa kujaza nafasi hizo huo unafuata mpangilio wa majina kama ulivyokuwa umewasilishwa na Chama husika wakati wa uteuzi wa wagombea wa ubunge wa viti maalum wakati wa uchaguzi mkuu uliopita.

CUF ilipeleka orodha yake ambayo haihusishi majina yaliyotangazwa. Hivyo ndiyo kusema hata kama hicho kinachoitwa kufukuzwa uanachama Wabunge hao kingekuwa halali (jambo ambalo si halali), basi kwa Kanuni za Tume yenyewe, watu wa kujaza nafasi hizo wasingekuwa hao waliotangazwa.

Kwa maelezo haya, Baraza Kuu linaweka bayana kuwa kitendo kilichofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kimezidi kuidhalilisha na kuishushia hadhi Tume hiyo na kwamba kwa kushiriki kwake katika hujuma hizi chafu ni ushahidi mwengine kwamba Tanzania hatuna Tume huru ya Uchaguzi.
 
Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Cuf limesikitishwa na hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kujidhalilisha na kujishushia hadhi kwa kushiriki katika hujuma za Dola dhidi ya CUF. Mbali na kasoro kadhaa, hata kama ingekuwa kufukuzwa Wabunge hao wa CUF kulikuwa ni halali na kumefanywa na chombo halali cha Chama, basi Kanuni walizojiwekea wenyewe Tume katika uteuzi wa watu wa kujaza nafasi hizo huo unafuata mpangilio wa majina kama ulivyokuwa umewasilishwa na Chama husika wakati wa uteuzi wa wagombea wa ubunge wa viti maalum wakati wa uchaguzi mkuu uliopita. CUF ilipeleka orodha yake ambayo haihusishi majina yaliyotangazwa. Hivyo ndiyo kusema hata kama hicho kinachoitwa kufukuzwa uanachama Wabunge hao kingekuwa halali (jambo ambalo si halali), basi kwa Kanuni za Tume yenyewe, watu wa kujaza nafasi hizo wasingekuwa hao waliotangazwa. Kwa maelezo haya, Baraza Kuu linaweka bayana kuwa kitendo kilichofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kimezidi kuidhalilisha na kuishushia hadhi Tume hiyo na kwamba kwa kushiriki kwake katika hujuma hizi chafu ni ushahidi mwengine kwamba Tanzania hatuna Tume huru ya Uchaguzi.
Jenga hoja na uhahidi, weka vifungu (provision) inayosema hivyo. Kwa namna hii utaonekana huna ushahidi! Niko upande wako NEC ni majanga lkn ukiwa na ushahidi unauweka hapa ndiyo kuelimishana.
 
Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Cuf limesikitishwa na hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kujidhalilisha na kujishushia hadhi kwa kushiriki katika hujuma za Dola dhidi ya CUF. Mbali na kasoro kadhaa, hata kama ingekuwa kufukuzwa Wabunge hao wa CUF kulikuwa ni halali na kumefanywa na chombo halali cha Chama, basi Kanuni walizojiwekea wenyewe Tume katika uteuzi wa watu wa kujaza nafasi hizo huo unafuata mpangilio wa majina kama ulivyokuwa umewasilishwa na Chama husika wakati wa uteuzi wa wagombea wa ubunge wa viti maalum wakati wa uchaguzi mkuu uliopita. CUF ilipeleka orodha yake ambayo haihusishi majina yaliyotangazwa. Hivyo ndiyo kusema hata kama hicho kinachoitwa kufukuzwa uanachama Wabunge hao kingekuwa halali (jambo ambalo si halali), basi kwa Kanuni za Tume yenyewe, watu wa kujaza nafasi hizo wasingekuwa hao waliotangazwa. Kwa maelezo haya, Baraza Kuu linaweka bayana kuwa kitendo kilichofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kimezidi kuidhalilisha na kuishushia hadhi Tume hiyo na kwamba kwa kushiriki kwake katika hujuma hizi chafu ni ushahidi mwengine kwamba Tanzania hatuna Tume huru ya Uchaguzi.
CUF umefika wakati sasa wa kumnyamazisha lipumb kwa njia yoyote ile
 
Umeishia kusema kwa Kanuni za Tume yenyewe lakin umeshindwa kuonesha ni Kanuni namba ngapi na inasemaje!
Jenga hoja na uhahidi, weka vifungu (provision) inayosema hivyo. Kwa namna hii utaonekana huna ushahidi! Niko upande wako NEC ni majanga lkn ukiwa na ushahidi unauweka hapa ndiyo kuelimishana.
Na kinacho staajabisha ni kwanini vilazwa wa ccm ndio nambari moja kwa ushadadiaji kwenye hili? Hapo ndio utajua shetani ni yupi.
 
Na kinacho staajabisha ni kwanini vilazwa wa ccm ndio nambari moja kwa ushadadiaji kwenye hili? Hapo ndio utajua shetani ni yupi.
Najua shetani ni CCM, CUF waende mahakamani. Court of appeal bado haki inatendeka.
 
Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Cuf limesikitishwa na hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kujidhalilisha na kujishushia hadhi kwa kushiriki katika hujuma za Dola dhidi ya CUF. Mbali na kasoro kadhaa, hata kama ingekuwa kufukuzwa Wabunge hao wa CUF kulikuwa ni halali na kumefanywa na chombo halali cha Chama, basi Kanuni walizojiwekea wenyewe Tume katika uteuzi wa watu wa kujaza nafasi hizo huo unafuata mpangilio wa majina kama ulivyokuwa umewasilishwa na Chama husika wakati wa uteuzi wa wagombea wa ubunge wa viti maalum wakati wa uchaguzi mkuu uliopita. CUF ilipeleka orodha yake ambayo haihusishi majina yaliyotangazwa. Hivyo ndiyo kusema hata kama hicho kinachoitwa kufukuzwa uanachama Wabunge hao kingekuwa halali (jambo ambalo si halali), basi kwa Kanuni za Tume yenyewe, watu wa kujaza nafasi hizo wasingekuwa hao waliotangazwa. Kwa maelezo haya, Baraza Kuu linaweka bayana kuwa kitendo kilichofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kimezidi kuidhalilisha na kuishushia hadhi Tume hiyo na kwamba kwa kushiriki kwake katika hujuma hizi chafu ni ushahidi mwengine kwamba Tanzania hatuna Tume huru ya Uchaguzi.
LIPUMBA amedharirisha sana Uprofesa wake
 
Jenga hoja na uhahidi, weka vifungu (provision) inayosema hivyo. Kwa namna hii utaonekana huna ushahidi! Niko upande wako NEC ni majanga lkn ukiwa na ushahidi unauweka hapa ndiyo kuelimishana.

Helu is right SOMA 78(4) ya katiba kuhusu uteuzi wa viti maalum huo ndio utaratibu ambao umekuwa ukifuatwa na Tume kuteua wabunge wa ziada endapo mbunge atafariki au kujiuzulu utaratibu ambao tume yenyewe imeshautamka mara kadhaa hata wkt wa kifo cha mbunge wa chadema juzi juzi wakasema wanakwenda kwy list iliyowasilishwa kwao wkt wa uchaguzi(2015) kwa sababu watu hao wamepigiwa kura kwy maeneno yao ndani ya vyama vyao.

Nitakwambia kwanini NEC imekwenda kuchukua majina kwa Prof Lipumba ni kwa sababu kuna uwezekano mkubwa watu waliokuwa kwenye list ya awali walishiriki kwy chaguzi za ndani na kushirikiana na ukawa kwy uchaguzi mkuu kwahiyo hawamuungi mkono Lipumba kwahiyo kufukuza wabunge kusingetosha endapo wangekuja kurithiwa na wapinzani wengine wa lipumba kwahiyo ndio maana this time NEC wamejivua nguo kwa kitendo chao cha kwenda kuchukua majina kwa Lipumba.

CUF inabidi iitishe press conference iivue nguo NEC kwa ku release majina yote ya wabunge kwy ile list ya awali
 
Helu is right
huo ndio utaratibu ambao umekuwa ukifuatwa na Tume kuteua wabunge wa ziada endapo mbunge atafariki au kujiuzulu utaratibu ambao tume yenyewe imeshautamka mara kadhaa hata wkt wa kifo cha mbunge wa chadema juzi juzi wakasema wanakwenda kwy list iliyowasilishwa kwao wkt wa uchaguzi(2015) kwa sababu watu hao wamepigiwa kura kwy maeneno yao ndani ya vyama vyao. nitakwambia kwanini NEC imekwenda kuchukua majina kwa Prof Lipumba ni kwa sababu kuna uwezekano mkubwa watu waliokuwa kwy list ya awali walishiriki kwy chaguzi za ndani na kushirikiana na ukawa kwy uchaguzi mkuu kwahiyo hawamuungi mkono Lipumba kwahiyo kufukuza wabunge kusingetosha endapo wangekuja kurithiwa na wapinzani wengine wa lipumba kwahiyo ndio maana this time NEC wamejivua nguo kwa kitendo chao cha kwenda kuchukua majina kwa lipumba. CUF inabidi iitishe press conference iivue nguo NEC kwa ku release majina yote ya wabunge kwy ile list ya awali

Manenoooo meeengi, ungeyafupisha kwa kuweka kanuni iliyokiukwa!
 
Umeishia kusema kwa Kanuni za Tume yenyewe lakin umeshindwa kuonesha ni Kanuni namba ngapi na inasemaje!

n hizo kanuni za NEC zinawatambua makatibu wakuu wawili maalimu na sakaya sijui vyama vingine kupo hivyo nchi ya ajabu SNA hii ni ya kusadikaka tu kila kitu hovyo hovyo tu alafu MTU anaomba aombewe ili kupunguza ukichaa.
 
n hizo kanuni za NEC zinawatambua makatibu wakuu wawili maalimu na sakaya sijui vyama vingine kupo hivyo nchi ya ajabu SNA hii ni ya kusadikaka tu kila kitu hovyo hovyo tu alafu MTU anaomba aombewe ili kupunguza ukichaa.

Sakaya ni Kaimu Katibu Mkuu wa CUF sio Katibu Mkuu, Prof kateua Kaimu Katibu na kajulisha Mamlaka za Kisheria kwa kuwa Katibu Mkuu haendi ifisini sasa ulitaka kazi zisiende?

Suala la Seif Sharif kutoteua Mrithi wa Prof alipojiuzulu mpaka akaamua kurudi ni Suala la Seif na CUF wenyewe inakuaje lawama apewe Rais kwani Rais ndie aliewaambia wachelewe kuitisha Uchaguzi wa Mwenyekiti Miezi minane tangu ajiuzulu?
 
Amesema anaandika barua kwa katibu wa chama kumtaarifu kupokea barua kutoka kwa spika ikimjulisha nafasi ya mbunge iliyo wazi. Je? Maalim Seif aliipokea hiyo barua?
 
Back
Top Bottom