Ndugu yangu kaoa kahaba? Tumshauri basi

BABU KIDUDE

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
1,588
904
Mnisamehe sana kama kuna makosa ya Kisarufi /Maana Kwenye Lugha yenu. si mwandishi mzuri sana

Habari zenu

Yupo Ndugu au Mdogo wangu japo si wakuzaliwa nimejuana nae toka 2004 kipindi nipo form 3 kwenye moja ya shule za jeshi jiji Dar tukiwa wanfunzi wa shule Hiyo na ni majilani mtaani kwetu.

Ndugu yangu huyu mwaka 2012 alifanikiwa kupata bint mmoja hapa jiji amabaye ametoka mkoa mmoja hivi maarufu kasikazini mwa Tanzania. na kwa bahati nzuri mwaka juzi 2016 ndo wamefunga ndoa na kupata mtoto mmoja wa Kiume.

Amekuwa na furaha muda wote wa mahusiano kabla ya na hata baada ya ndoa yao bint huyu ni Mzuri sana anasifa zote za bint mrembo kwa kweli shemeji yangu anavutia sana. Sifa yake kubwa kabisa Upole si Muongejai kabisa. sifa nyingine ya kuambiwa na Ndugu yangu huyu ni Mke wake ni Mtaalamu kitandani.

KISA CHENYEWE
Ijumaa ya wiki hii alinipigia simu kuomba kuonana na mimi, kuna kitu angeomba kunishirikisha na nimshauli.
Tuliweka ahaadi ya Kuonana Jumamosi saa 10 jioni Bar moja ya kitaani kwetu huku Baruti kimara, kwani yeye ni mkazi wa Mbezi kwa Yusuph.
Tulifanikiwa kuonana na kunipa Mkanda mzima.

Kwa muda wa week nziima mbaka ananipigia simu siku ya Ijuma hakuwa na masikizano na mke wake ndani na sababu kubwa kabisa ni baada ya kukuta meseji za ajabu kwenye simu ya Mke wake, siku ya jumatautu jioni. meseji hizo zilikuwa zinatoka kwa mmoja wa wa X wa mke wake.
Meseji zilikuwa a kusiafiana huku Jamaa akiomba wawe waniaba siku moja moja kwani Kamiss penzi la Bint huyo, likini bibie akikataa. Pamoja hayo bibie alikimwagia sifa jamaa kuwa anajua kutumia maumbile yake jamaa nae akijibu Bibie kaiva kitandani.
pia walikumbusha mambo kadhaa, moja wapo ni jinsi Binti alivyo mcheat ex wake huyoo na mmoja wa watu mtaani kwao ambaye wanajuana na Jamaaa ahh ahh ahh.

Baada majibizano Jamaa akataka kumtwanga Talaka mke wake huyo siku ya alhamis Lakini mke wake wake huyo alikataa akilia amsahe kwani kapitia maguma mbaka anakutana na jamaal yangu.
Kijitetea bint ilibidi afunguke siku hiyo ya Alhamis usiku.

Mambo yapo hivi
Bint huyoo alianza kwa kumwambia jama Jinsi alivyoishi mbaka kufika wanakutana na jamaaa kukaa kwenye mahusiano kwa miaka 4 na miaka mitatu ya ndoa na mtoto mmoja.

Bint mzaliwa wa mkoa mmoja maarufu sana lugha ni ya, Bint huyu amezaliwa kwenye familia ya masikini kabisa akiwa mtoto wa tatu kwenye familia ya watoto 8, akitanguliwa na dada kaka kisha yeye.
kwenye Familia yao ni yeye peke yake alifanikuwa kufauli kusoma sekondali kwenye moja shule maarufu za vipaji maalumu kwa wasichana.

Kutokana na Shida alikuwa ngumu hata kwenda huko shule. wazo la wazizi wake kuolewa wapate mahali tuu. Mmoja wa mwalimu katika shule yake ya msingi kijijini kwao ailibidi ajitolee kulilipa gharama za vifaa vya shule, alifakiwa kwenda kwenye shule hiyoo ya vipaji maalumu kwa wasichana ni ya bweni kwani binti alikuwa mataalamu wa Hisabati shule ya msingi.

Alisoma kwa tabu ni shida zote unazo zijua, akiwa kitadato cha 3 shuleni hapo, kulikuwa na uendelezaji wa mabweni na majengo kwenye shule yao na kulikuwa muingiliano ya wanafunzi na mafundi kwa kiasi kikubwa. Hivyo basi kwa Bahati nzuri au mbaya moja wa Mabosi wa kampuni hiyo ya ujenzi anatoka kijiji kimoja na yeye so alivyomuona alimfuata na kumsalimia, baada kuhamiana kwa kiasi flani jamaa alikuwa anamtoa kifedha na kumsadia hapa na pale, kila wiki Mzee huyo akitembela site anamletea Sukari, Siagi, Mkate na vifaa vingine huku Shemeji yangu akizania baba huyo ameahumua kumsadia kwani anajua familia yao ilivyo.

Kama ujuavyo hisani za wananume bana jamaa akaanza kumtongoza akaomba mzigo binti akiwa hapo shule na mara nyinge aliporudi rikizo mzee huyo alimfuata mbaka nyumbani kwao ukiachana na pale shuleni. Wakahaidiana akifunga shule wataondoka wote kurudi mjini manaa shule ilikuwa inakribia kwenda rikizo kubwa ya mwezi wa sita . Baada ya kufunga shule ikafanyika mipango jamaa akabeba binti akavunja bikra na Binti Hakarudi nyumbani likizo nzima alikuwa kwa jamaaa, baada ya kufungua tuu shule Boss huyo alimfungashia mahitaji yote ya shule na akamrudisha kuendelea na shule.

Kumbuka mkandalasi huyo Mtu mziama kwani alikuwa na watoto wanne moja ni mkubwa ziadi ya Shemeji yangu huyo, wawili wanafananae kiumri mmoja wa kike na mwingine wa wakiume na nne ni mdogo kiumri.
Mtoto wa kwanza wa kiume wa mzee huyo alikuwa form 4 wanafuata walikuwa form 3 na mdogo yupo shule ya msingi. Mzee alizaa na wanawake watatu tofauti.


Alipo rudi shule Mzee huyo aliendelea kumhudumia na kilawalipo funga shule Boss huyu alimfuata na kwenda nae nyumbani anakula mzigo kisha anapewa nauli mahataji mengine anarudi kijiji, shule ikifunguliwa anapita tena kwa Boss kama week kisha shule so Boss huyo alimfanya kama Mke kwani hakuwa na mke kwa kipindi hiko.

Akafanikiwa kumaliza kidato cha nne kumbuka boss huyo anatoka kijiji kimoja na wao hivyo kwa kiasi flani alikuwa anaisiadia fimilia bila wao kujua boss huyo anatembea na binti amefanya kama mke. baada ya kumaliza kidato cha mzee huyo alimtolea mahali kwa nia ya kumua kuhaidi kumsomesha, alikata sana lakini mwisho wa siku alikubali kwa Sharti la Kundelea kusomeshwa. Nyumbani hao mzee alikuwa na mahouse Girl na mahouse Boy so bint ilkuwa ni kosoma na kipiga show tuu na mzee huyo, japo mzee ilkuwa ya kupepea au mbaka anywe viagra.

Matokeo ya kidato cha yakatoka alipata Div 2 na anatakiwa kwenda shule. Mzee huyo boss akagoma kumsomesha akitaka abaki kuwa mama wa Nyumbani ugomvi wao huo ulipekea kupata kipigo mara kwa mara kila anapo ulizia shule na kumfanya akate tamaa. Imani ikamwingia mzee huyo akampekela shule Binafsi ya day kwani binti alichaguliwa kwenda shule ya bweni ya Serikali ya Wasichana, akaubali akawa anasoma akitokea nyumbni kama Mke na shule mwanfanafunzi kidato cha tano na sita mabaka akamamaliza Matoke yakwa div 3.

Kama Kawaida mzee akagoma kumpeleka chuo akidaia achugue moja shule au Ndoa binti akachangua kusoma, huku akiwa na matumaini hatapata mkopo hata akichwa. Mzee akamfukuza bint akarudi kwao Kijiji.
Akchagulia vyoo vitatu lakini akakosa mkopo ikabidi alime tuu kijini kwao.

Kwa vile mzee huyo alimpenda akubali kumsomesha kwa sharti asome chuo kilichopo mkoa husika na kiwe karibu nao. akafakiwa kupata chuo Husika na mzee akalipa ada ya mwaka wa kwanza.bInt akaubali kuridi kwa mumewake huyo. na mzee alighalamia kila kitu cha chuo safiri za mafunzo na field sijua.

Lakini akiwa chuo kwa urembo wake shemeji yangu huyu mrembo alivutia vijana, walimu, na watu wengi hapo chuo. mzee akapandikiza mashushu wakumfatilia aliwalipa kwa kumpa taarifa. wivu ukazidi mzee akumuliza tena Unapenda shule au Ndoa? binti akurudia Shule jamaa akatoa talaka ndoa akunjika akiwa mwaka wa kwanza semester 2 kumbuka mzee alishalipa ada ya mwaka mzima pamoja na Bweni.

Itaendelea...

Inaendelea

Kwanza Mnisamehe sana Sina Lengo la kurefusha sana hapo nimejaribu sana kuifupisha, Niliomba radhi mimi si mwandishi mzuri msisamehe sana sana. hope nimejaribu kuifupisha kwa sasa. Hii kitu ni ya kweli ninavyoandika hapa Mgogoro umehamia kwenye Familia zao weekend hii wanakutana kwa baba Mdogo wa Binti kama rafiki nimeharikwa pia.
Nimejaribu sana kuuficha uhalisia wao.


Tulishia Pale shemeji yangu anachagua chuo zidi ya ndoa yake hiyo, anamaliza mwaka wa kwanza wa chuo tuendelee…

KIKUBWA KIPO HAPA
Mwaka wa kwanza alimaliza vizuri kabisa bila supp , Kimbembe kilianzia Mwaka wa pili, chuo kilifunguliwa nyumbani Baba na Mama wanatengana. Baba aliondoka nyumbani ana kuwacha Mama na watoto 7 kwani Dadake alibahatika kuolewa na Dereva wa Daladala, Kaka mkulima na fundi Ujenzi, mama mkulima yeye chuo mwaka wa kwanza na ndoa imevunjika.

Mama akapambana akampatia nauli ya kurudi chuo .
alifanikiwa kufika mkoa husika akafikia kwa mmoja wa mama wa mmjini hapo ambaye wanatoka nae kijiji kimoja, mama huyo alikuwa anafanya biashara ya mama ntilie, kesho akareport chuo japo mbali na wapoishi.

Siku ya Kureport wakanza kudai ada hakuwa nayo hivyo ikabidi arudi home kwa yule mama na kumomba kama anaweza kumsaidia kilipa ada ya chuo, mama huyu hakuwa na huwezo huo alichoweza kumasaidia kula na kulala akipewa kazi ya kuosha vyombo. mungu si athumani wakati yupo chuo alikutana na mama mmoja anasoma akitokea kazini mama huyo ni hakimu. Mama huyo hakimu alimuomba Bint akae naye kwani alipanga chumba karibu na chuo na yupo peke yake akitoa ahadi ya kumlipia nusu ya ada, akubali maisha yakaendelea akiwa kama house girl wa mama huyo ambaye ni mwanafunzi mwenzake pia.

Ikawa kusoma, house Girl na muosha vyombo kwa yule mama Ntilie, katika movement hizo alifanikiwa kukutana Jamaa wakawa wapenzi wa kupika na kupakuwa jamaa kazi yake Mganga wa kienyeji.alikuwa mara kadhaa anafikaa kwa mama huyo ntilie kumtibia Mganga huyo aliku tayali anawake wawili hivyo binti akawa kimada na (huyu ndiye aliyesabisha yote haya) . Jamaa huyo hakuwa na huwezo kumsomesha, na kwa bahati mbaya yule mama hakimu alicha tuu chuo, so semaster one ilikwisha akiwana na suppl 2.

Akarudi kijiji kwao, baba hayupo home mama tu na wadogo zake.kumbuka kuna ada na supp mbili.
Aliporudi kijijini kuna Meku muuza duka anawasadiaga sana familia yake kwa kuwakopesha vitu Kwa ahaadi ya dada (Binti) akirudi kutoka mjini atakulipa. Dada aliporudi mangi akadai chake, Moyo ukamshinda mangi bana akaomba penzi kwa binti akapewa deni likafutwa.

Mangi akawa Danga lake kijijini kule town Danga Mganga Kumbuka binti mataalam kweli kitandani
Mangi akapagawa bana kule Mganga pamoja na kuwa na wake wawili alifunga safari kwenda kijijini kumfuta binti, akakuta Mangi ndo mmiliki. ukatokea ugomvi maganga na mangi kijijini. mangi akapiga chini binti Mganga akapiga chini pia.

Muda kurudi chuo mwaka wa pili ukawadia wakauza mazoa, kaka yake ni fundi wa ujenzi nae akapambana wakapata vijisent vya kuanzia japo ada ya semester 2 robo na nauli ya kurudia chuo. Ilikuwa imeabaki siku moja tuu kwenda kufanya Supp na bado yupo kijijini. Kijijini kwao kunashida ya usafiri hivyo basi alibidi zifanyike juhudi asafiri kwenda chuo na kesho yake afanye supp.

Alifakiwa Kupata FUSO saa 10 jioni kwa kulipa nauli elf 15. kama kawa njiani dereva fuso kaimbisha mbaka wanafika mkoa husika binti kalegea Dereva Kalamzigo akamwachia na pesa kidogo binti akafika chuo akalipa ada akapiga supp. chuo kikaendelea

wakati yupo chuo anafanya Supp akakukatana mwanafunzi mwenzie Anatokea mkoani mwingine, alifikia Geto kumbuka yeye alifikia mbali kidogo na chuo wakashawishiana wakalala geto pamoja kilicho andelea jamaa kala mzigo.
badaa ya kukutana hapo basi jamaa huyo ikabidi achukue na kuwa mpenzi wake wa chuo, Kumbuka washaa achana na Mganga, huku kwa yule mamantilie kama kawa jioni kuosha vyombo. katikati ya semester ada akikata akatokea Prof. mmoja akaweka sawa kala mzigo binti akamaliza mwaka wa pili .

Mwaka wa tatu Kahamka na Prof hapo chuo yule mwanafunzi mwenzie akapigwa chini, Prof akatoa ada, kulipa hosteli binti akaseto kidogo. wakati yupo mwaka wa pili semester 2 alifanikiwa kukutana na jamaa kwenye basi akiwa anakwenda chuo wakabadilishana namba za simu, jamaa ni makazi wa Dar maisha yakaenda. wakendelea kuwasiliana kwenye simu huku jamaa akitoa huduma kwa njia ya mtandao prof alishamnunulia simu wakati huo.

Akamaliza chuo akarudi kijiji kwao, Degree kichwani yupo kijiji kazi kubwa huko ni kilimo na hawakuwa na shamba kubwa ni hekali tatu tuu walizopewa na Serikali ya kijiji, na kuwalisina na wanafunzi wenzake kama kuna kazi mahala waunganishiane. Aliporudi kijiji akatokea Kijana mwenzie ni mganga shughuli zake ni Nje ya nchi za Arabuni wakawa wapenzi, kama wiki tu alipondoka tu kijijini na mawasiliano yakakata.

Akiwa kijijini mara yule Mganga wa kwanza (aligombana na Mangi)akaja kijijini kwao kwa nia ya Kuoa kabisa, kuwa mke wa tatu binti akachomoa mganga akashusha laana kwamba hutoolewa maishani na hata ukiolewa hutodumu kwenye ndoa. binti akusikiliza longo longo hizo akapiga moyo konde….

NDANI YA JIJI LA DAR SASA
Baada ya kumaliza chuo Dec 2011 mawasiliano yake na yule jamaa waliyekutana nae kwenye basi mkazi Dar yalikwa yanaendelea. Huku na kule yule jamaa akamwambia aje Dar atamtafutia kazi kwani ana connections nyingi viwandani . Aliaga kwao kapata kazi Dar waka mhruhusu Kumbe anakuja kwa jamaa, hakuwai kufika Dar hii ndo mara ya kwanza. Japo alikuwa anasikia kuna mtoto wa Shangazi yake ( Binamu)anakaa manzese hakuwa na namba zake za simu wala mwasiliano.

Jamaa akamtumia nauli akaja Dsm akampokea Ubungo na kwenda kwenye Makazi yake Kawe Uswahilini huko, kwa Jinsi alivyokuwa anaongea na jamaa kwenye simu akajua Bonge la mfanya biashara, kumbe jamaa anakuchumba kamoja na ni dalali wa mazao sokoni lakini ndo kashafika, kahaadiwa kazi basi akatulia kusikilizia. Wakaishi kama mke na mume maisha yanasonga, Dalali huyo alimsaidia pesa za kwenda internet cafe kutuma barua za maombi na nauli za kwenda hapa na kupeleka barua za kazi wakati mwingine jamaa alibeba barua na kuipeleka mwenyewe.

Baada kama Mwezi alifanikwa pata Kibarua kiwandani kwa malipo la shilingi 4200 kwa siku kwa msaada wa aliyemleta Mjini. alifanikiwa kufanya kwa muda kama mwezi, kiwanda kilikuwa kinatengeneza vyombo vya plastiki ilikuwa kazi ngumu sana na Harufu mbaya sana, huku akiendelea kukaa na huyo jamaa. Ndani ya kiwanda akatokea jamaa msimamizi akaomba penzi kwa ahaadi ya Kumtoa kwenye kazi ngumu na kumweka seheemu nzuri kidogo, Binti akaingalia line akakubali akampa mzigo bana pale pale Nyumbani kwa jamaa aliyempokea wakati jamaa hayupo kasafiri.

Kesho yaka akapewa sehemu nzuri na walau anapata 6500 kwa siku. Jamaa akakolea akataka kutoa posa binti akamwambia subiri kwanza sababu ndo kwanza anaanza maisha.

Akiwa kiwandani hapo kumbuka alikuwa ametuma barua nyingi seheemu tofauti, siku moja akapigiwa simu afike kwenye ofisi moja ya serikali, bila kusita alifaka na kufanyiwa interview kisha kuambiwa kesho aje aanze kazi.
haikuwa ajila bali kama Kujitolea lakini alilipwa elfu 10 kwa siku pamoja na kula, kazi kubwa ilkuwa kupanga mafaili.
alikuta mabint wazie pia kama wanne. Kiongozi wa kitengo alikuwa Mzee, baada ya kama week mzee akaomba mzigo bana wakasumbuana sana akampa mzigo kipindi hicho jamaa wa kiwandani washa achana hila bado anaishi na yule dalali Kawe.

Siku moja yupo ofisini akipanga mafaili alitokea Boss mmoja kutoka manispaa alitembelea kuona kazi zinavyokwenda alimkuta yeye peke yake siku hiyo, alimuhoji kuhusu elimu, anapo tekea na Dini yake katika mahujiono alimuhaidi kumatafutia mahali kwani anafamiana na watu wengi town hapa wakapaena namba za simu.

baada ya wiki akaipigiwa simu na boss huyo wa manispaa aende sehemu kuna kazi apeleke cv zake, alifanya hivyo bila kuchelewa alipofika tu akapewa kazi hapo hapo ya uafisa na mshahala wa 1M toka elf 10 kwa siku, na hii ni ajila ya kudumu ni Idara uapande wa fedha fedha shirikani na anafanya kazi mbaka sasa.

Katika shirika hilo wiki tu baada ya kufika akatokea Mangi mmoja humo akaanza kumtongoza, Mangi huyo alikuwa na mke na katika kutumiana meseji siku moja yule dalali alizikuta bana kumbuka bado anaishi na dalali kama mke,na dalali pia alishakwenda mbaka kwao kupeleka Barua bint huyo alimwambia asubiri kidogo wakae sawa. Kwa meseji hizo alizozikuta bwana Dalali kutoka kwa mangi zilimfanya wapigane sana usiku nakuchukua simu ya binti kisha kumfukuza hapo kawe.

Ndani ya wiki 2 mbili toka aanze kazi serikalini hana kitu na anafukuzwa kwa Dalali aliondoka bila kujua pa kwenda kibaya sana dalali alichukua simu ya Binti huyo ilikuwa usiku saa nne hivi. baada ya kutembea tembea sana usiku huo alikwenda kwenye jumba moja huko kawe kwa nje kulikuwa na mlinzi akaeleza shidah zake mlinzi kwa mlinzi, mlinzi kwa kumasaidia alimruhsu alale kwenye kibanda cha Mlinzi kwenye nyumba moja huko kawe.Kumbuka vyeti nguo, pesa na kila kitu chake kipo kwa dalali huyoo.

Kesho yake asubuhi bwana mlinzi alienda nae nyumbani kwake maeneo ya Manzese alikuwa kavimba kwa kipigwa na dalali, bahati nzuri sana Mzee huyo mlinzi alikuwa na familia yake akawaita akawatambulisha mgeni huyo akapewa na nguo, Mida ya saa 6 mchana Bint akaenda kazini akapiga kazi kisha kurudi kwa Mlinzi huyo.

alikaa kama wiki hivi. siku moja katika pita pita ghafla akautana na Mtoto wa shangazi yake maeneo ya Manzese walikuwa wote kijijini akawa bahati. Mtoto wa shangazi yake huyo alifikia kwa dadake mkubwa Manzese . Wakaongozana mbaka kwa dada yao huyo mkubwa. akaaga kwa Mlinzi kuanza kuishi kwa Binamu yake huyoo.

Siku mmoja yeye na mtoto wa Binamu yake walikwenda kutuma mizigo kijiji kwao kwa madereva wa malori kwa bahati mbaya siku hiyo akakutana ya yule dereva wa aliymsadia miaka 2 nyuma wakapena namba simu dereva huyo akamuomba waonane, kesho yake wakaonana kisha akamfikisha mbaka nyumbani kwakwe bwana Dereva huyoo huko Kigogo, Dereva huyo hakuwa na mke kwani walisha achana hila anawatoto wakubwa wanne wapo hapo nyumbani anaishi na dada na baadhi ya Ndugu. Bibie akaombwa waishi hapo na bwana Dereva.

Alisita kwanza baada ya kama siku mbili akakubali na akahama kwa Binam yake huyo na kwenda kwa Dereva na kuanza kuishi kama mke na muwe. Siku moja alitoka na kwenda kawe kuchukua vitu vyake amabavyo ni nguo pamoja vyeti, hakumkuta jamaa hivyo aliomba namba ya simu kwa wapangaji wenzie akampigia akiomba aje hamfungulie na kumpatia vitu vyake, jamaa huyo aligoma na alimtaka tu arudi nyumbani hapo na warudiane waendelee bibie akagoma , Jamaa huyo dalali akaomba arudishiwe ghalama zote za kumtoa Mkoani na kumtafutia kazi ilifika kama laki mbili hivi bibie akamwambia mwisho wa mwezi akilipwa mshahala basi atamlipa.

Ilipofika mwisho wa mwezi mshahala wake wa kwanza kabisa akampigia jamaa wakakutana manzese akapewa chake na kukabidhi mizigo basi wakaachana kwa hivyo.

wakati huo yule Mangi kule kazini kachamaa visa mikasa kwa binti akiomba mzigo akapewa pia, mapenzi yakawa moto moto mangi akaacha familia akapanga Lodge tabata wakitoka kazini Lodge kisha ndo home, kumbuka binti anaishi na yule Dereva basi akisafiri huku mangi anatwanga maji kwenye kinu. Mke wa mangi akastukia, mangi mkazi wa kimara akafanya utafiti akagundua mwizi wake kupitia simu ya mumewe kwani alikuta meseji zoa.

Mke wangi akaenda job kwa Mangi akamchana sana binti, ikabidi bint aachane na mangi na akaamishwa ofisi kabisa binti akabaki na Dereva wake. Kule nyumbani sasa ndugu wa Dereva hawamtaki binti sababu toka kaja yeye kaka yao kakata huduma kwao huduma na pesa zote anachiwa bibie ugomvi ukaanza huko jamaa akisafiri nyumba haina amani.

Na kipindi hiko jamaa huyo Dereva alikuwa anajenga nyumba nyingine huko Bunju kabla ya hapo msimamizi alikuwa dada wa Dareva so hapo bibie ndo kawa msimamzi ndugu zake na Dereva walimind sana kitendo hiki.

ALIVYOKUTANA NA JAMAA YANGU.
Jamaa yangu huyu anakampuni yake alikuwa akisupply vifaa hapo ofisini kwao. siku moja alifika kufwatilia hati ya madai na kumkuta bibie akiwa peke yake ofisi akilia, akamsalimia na kumuuliza tatizo. Baada ya kumbembeleza sana bibie akafunguka dahh jama akumuliza anacho kifikilia nini ilihamsadie binti huyoo, binti akasema anataka kuhama pale nyumbani kwa dereva na kuanza maisha yake huku akiomba kumsadia kutafuta Nyumba.

Jamaa yangu akamshauli kumtafutia chumba maeneo ya Tabata kwani kuna wastaarabu kidogo , Ndugu akapewa jukumu hilo akamtafutia Chumba na Valanda Tabata, bibie akalipia lakin hakuamia akisubiri Dereva arudi amwambie ukweli tuu aidha waachane au wamie huko kwenye chumba alicholipia.

Kwa Bahati wakati anashi na Dereva walishapeana mawasiliano na Wazazi wa binti hivyo siku moja Bwana Derava alikwenda kijiji kwao alipata wasaa wa kwenda kwa fimilia ya binti na kujitambulisha na kuwaambia anaishi na binti yao taratibu zikikamilika basi watafunga ndoa so ndugu wa Binti walikuwa wanamjua. siku Hiyo Derava alirudi kutoka safari akiwa na mmoja wa wadogo wa Binti aliyekuwa yupo tuu nyumbani kwa nia ya kukaa naye.

Kurudi tuu bibie kaomba kuondoka hapo nyumbani kwani manyanyaso yalizidi toka kwa ndugu na jamaa wa Bwana Dereva na Dereva kashapagawa na penzi la Bibie basi jamaa akakata mipango ya Bibie. akukaa sana akapata safari, alivyo ondoka tuu huku nyuma Bibie akampigia simu Huyu mdogo wangu akawapokee kule tabata kwani ameamua kutoroka tuu. Mwisho na dereva huyo ukafikia japo kidume akikukubali kilisumbua sana na bado anasumbua .

Kwa vile funguo ya chumba kule tabata alikuwa nayo ndugu yangu alibidi atoke Ubungo na kwenda Bima Tabata kuwapokea akawakabidhi funguo akaondoka zake, sasa hapo binti akitaka chochote mjini akawa anamtumia jamaa yangu kununua, Tv, Makoch,kitanda Godoro sijui Redio kila haina ya taka taka, ( binti alimpa pesa ndugu huyu akamnunlie, kama ikipungua jamaa yangu alimuongezea kisha binti alimrudishia) kwa kindi hiko chote 12-13 ndugu yangu hakuwa na demu maalumu.japo alikuwa na demu wa muda mrefu toka O level na hakuwa maalumu lakini. Pia jaama yangu akiwa anataka malipo yake yaende faster ofisini kwa binti akawa anamtumia na ndipo walizoena na kuingia kwenye mapenzi mahaba baadae Ndoa.

Wakiwa kwenye mahusino binti alishawia kumcheat jamaa wanaume watatu, haya yote hakuyajua hila ugomvi huu ndo amejua. Wa kwanza alikwenda field hapo ofisi kwao ni mtoto wa Kiongozi msataafu wa siasa tena mkubwa tuu waliwai kwenda kulala nae Zenji kama siku tatu hivi. Kijana huyo sasa ni mwanasiasa pia na ni mtu mkubwa pia,

Wa pili kijana aliyewai kuwa mpenzi wake kule chuo kama unakumbuka ni yule aliye lalanae Wakiwa anafanya supp.

Watatu ni Mganga wa kienyeji, Kuna kipindi alikuwa ananguka tu ofisi akipelekwa hospitali hawaoni kitu basi Ndugu wakampeleka kwa Mganga Mwarabu toka Tabora akamtibu inasemaka alitupiwa jini kazini, kuna mtu aliondolewa kwenye kitengo hakufurahi anahisi binti huyo ndo kamfanyia ntima nyongo. Ki-ukweli niyeye binti ndo aligundua kunpesa zinapotea na kureport kwa mabosi na maboss kuchukua hatua. Baada ya Matibabu akapona lakini mganga akajikuta anamsumbua shemela mwisho wa siku akala mzigo tena si mara moja.

Baada ya kufunguka hayo yeto basi jamaa ndo anaomba ushauri na weekend tunakikao cha ndugu jamaa na marafiki huku jamaa akiwa ajielewi na kwa sasa nipo nae tuu hata kwa fimila yake aendi,

Kingine katika kila aliyetembea naye hapo wote wapo, na kila mmoja kwa wakati wake wanomba kurudiana na huyo binti, ilibidi Binti amuonyeshe tuu Meseji zote, email, zote whatsapp zote.

Mkurugenzi wake ofisi akiwa kwenye jitaada kali za kumpata
Na kila anyemtongoza Bibie huyo alibidi ampe na kumonyesha namba za simu.
kazini kwao kuna watu watano wanamtongoza.

Kuna wanaotoa huduma (supplyer) sababu yeye ni mhasibu wana mtaka.
Account za Ofisi zao zipo CRDB, NMB huku ndo usisema,
jama kapewa namba na majina ya wanao mtongoza kila siku.

Pamoja na hayo yote alikuwa navimada kibao hila toka kaoa asee katulia sana.
Nina screenshort nyingi sana kama 80 za watu wanaomtaka na kumtongoza jamaa kanionyesha.

—Tujifunze,Tuburudike, Tukosowe na Tumpe ushauri——
Mnisamehe mimi si
Mwandishi mzuri waungwana hila nimejitadi kwa kweli

—— Mwisho ——
 
"Itaendelea..."

Kama huna muda wa kuandika ni bora usiweke stori hapa hadi utapomaliza yote huko uandikako...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom