Hahaha.....umenikumbusha kuna mmoja nilimwona amesomewa hiyo Albadiri baada ya kuiba ng'ombe kijijini, Tumbo lilijaa kama mtungi wa maji hatimaye alipoteza maisha.Mtu anayeuza Mtungi wenye Gas Mara nyingi hii mitungi inakuwa ni ya kupiga. Sasa basi ukute Mtungi umeibwa sehem halafu aliyeibiwa kaenda kusoma albadiri.
Jirani yangu anafanya Biashara ya Gas,alitoka kununua Gas mitungi 52, usiku wakaja vijana wa kazi wakamuibia mitungi yote. Mtaji wote ulikuwa ni 7m.
Alilia kama Mtoto, haikuishia hapo, akaenda ZnZ kusoma albadiri kwa aliyeiba na yoyote aliyenunua. Ilikuwa kimbembe. Walionunua ndo waliokuja kulipa, tena walimlipa zaidi ya Mara Mbili.
Tuwe makini na hivi Vitu Vya Dili, sio vzuri hata kidogo.