Nataka kuwekeza katika maeneo haya nje ya jiji la Dar kabla ya mwaka huu kuisha, wenyeji wa maeneo haya naomba tuwasiliane

Parabora

JF-Expert Member
Jul 6, 2019
1,504
2,180
Wakuu nina Kibiashara changu hapo mjini dar kinachonipatia ridhiki, lakini kwa mda mrefu nimekuwa nikitafiti sehemu za kupata eneo kubwa la kuweza kufanya shughuli zangu kiupana zaidi na hapa Dar ibaki tu kama mmojawapo ya sehemu ya hivi vibiashara vyangu, nimebase katika biashara za mazao karibia yote ya nafaka na mifugo pamoja na samaki ambapo nauza jumla na rejareja, kwenye mifugo hapa nauza walio hai na pia nachinja nauza nyama kwa wenye mabucha na zinazobaki nasambaza kwenye Meat House zangu mwenyewe na kwa vile Mimi sipo huko nchini lakini biashara bado zinaendelea vizuri.

Nilikuwa nafikiria nipate eneo kubwa kwenye mikoa ambayo ni rafiki na hizi biashara zangu maeneo ambayo yamechangamka kibiashara yatakayoniwezesha kufungua vituo vingine vya biashara za aina hii pia niwe nakukusanya malighafi kirahisi na kuzituma Dar zichakatwe ziingizwe sokoni kama bidhaa tayari kwa kuuzwa.., maeneo ambayo nitahitaji kwa ajili ya kujenga miundombinu yangu ya ufugaji atleast yawe 15km kutoka center ya mji husika na pawe na umeme na usalama wa kutosha na shamba lenye ukubwa usiopungua heka 20 mpaka 30

Miji na sehemu ninazofikiria
1. Morogoro
2.Singida (Iguguno)
3.Geita (Katoro)
4. Shinyanga (Kahama)

Sina uzoefu wa kutembelea maeneo yote haya japo si sana kulingana na mda wangu kunitinga huku ng'ambo kwa waliopo maeneo haya naombeni tuwasiliane ikiwemo kunipa ushauri wa sehemu ambayo nitapata maeneo mazuri yatakayonifaa kwa ajili ya shughuli zangu.

Ahsanteni
 
Fikiria kwenda Gairo nikipata mawasiliano na mwenyeji wangu nitakupa number update mawili matatu kutoka huko
 
Kuanzia kibaha huko utapata tu maeneo makubwa tu. Na moro sawa,nako utapata eneo kubwa. Nafikiria usiende kuwekeza mbali sana ksbb. 1. Shughuri zako zingine ziko dar,ili kupunguza gharama za kwenda kuona shughuri zako sehemu zingine na kwa haraka bora usizidi moro. 2. Moro kwenda mbele charinze au kibaha, kwa hiyo biashara yako unayotarajia kufungua ni rahisi kuwa karibu na soko,ambalo ni dar

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuanzia kibaha huko utapata tu maeneo makubwa tu. Na moro sawa,nako utapata eneo kubwa. Nafikiria usiende kuwekeza mbali sana ksbb. 1. Shughuri zako zingine ziko dar,ili kupunguza gharama za kwenda kuona shughuri zako sehemu zingine na kwa haraka bora usizidi moro. 2. Moro kwenda mbele charinze au kibaha, kwa hiyo biashara yako unayotarajia kufungua ni rahisi kuwa karibu na soko,ambalo ni dar

Sent using Jamii Forums mobile app
nina watu nimeajiri wanafanya hiyo kazi mdada mimi mara nyingi huwa naenda kusimamia kwa masaa machache na sio siku zote
 
pamechangamka mkuu?
Tinde pame changamka sana mkuu.
Ni pale njia panda ya kuelekea kahama na shinyanga.maana hata izo nafaka pale waweza kuzikusanyia kirahisi.

Ukikaa apo una kuwa karibu na kahama, shinyanga, nzega na igunga.
Kwaiyo hata kama unakusanya mazao toka wilaya izo itakuwa virahisi kwako.

Alafu papo njiani gari za kwenda dar, mwanza,Kigali ziko mda wote.

Pia unakuwa karibu na centre kubwa zile za kahama kama isaka na kagongwa pia
 
Tinde pame changamka sana mkuu.
Ni pale njia panda ya kuelekea kahama na shinyanga.maana hata izo nafaka pale waweza kuzikusanyia kirahisi.

Ukikaa apo una kuwa karibu na kahama, shinyanga, nzega na igunga.
Kwaiyo hata kama unakusanya mazao toka wilaya izo itakuwa virahisi kwako.

Alafu papo njiani gari za kwenda dar, mwanza,Kigali ziko mda wote.

Pia unakuwa karibu na centre kubwa zile za kahama kama isaka na kagongwa pia
ahsante mkuu
 
Back
Top Bottom