Mndengereko
JF-Expert Member
- Mar 24, 2011
- 7,280
- 3,345
Dah! kama hivyo ndivyo
ulivyoamua basi umefikia kikomo cha kufikri, nashangazwa sana na hoja
zako kiasi kwamba naona kama unafanya mzaha humu ndani, toka lini
ukafanyia kazi hisia '' Eti unahisi kuachika'' kumbe huna uhakika kama
umeachika,afu kama hivi ndivyo unavyopanga, utafute mwanaume legelege
asiyekuwa msomi, kwani nani alikueleza vigezo vya mapenzi bora na makini
ni elimu au kujazia misuli? kumbe hutafuti mwanaume wa kufanya naye
maisha ila unatafuta mwanaume kama kifaa cha '' VIBRATOR'' kwa ajili ya
kukidhi haja zako za kimapenzi tu, afu mwanaume anakupenda kwa dhati
hawezi kuzuzuka na mwanamke mwingine je, mara ya mwisho lini ulitafakari
kama wewe mwenyewe sio sababu ya mambo yanayokusibu?
Umekata tamaa sana na maisha kiasi kwamba umejiweka kuwa duni eti ''
IKIWA NTAACHIKA NTATAFUTA MAN ASIYEMSOMI,NOT HANDSOME, MWENYE ROBO YA
KIPATO CHANGU,ALIYEVUSHA UMRI WA KUOA, ETHNICAL MAN'' kumbe wewe ndo
unatafuta sio kutafutwa! au wewe sio mtanzania hujui mila na desturi
zetu? toka lini wewe ndo ukatafuta mwanaume? kwa mtizamo huu tayari
naona una kasoro maana sio kawaida, afu kitu kingine. Napenda
nikuhakikishie kama hivyo ndivyo unavyofikiri kamwe hutakuja upate
furaha ya mapenzi duniani, kaa chini tulia, usitake papara, unasema
unahisi kuachika kumbe bado hujaachika sasa unataka nini? amekutamkia
hakutaki? hata kama ingekuwa hivyo kwanini ukate tamaa kiasi hicho? ni
vile tu sijui umri wako pengine ningeelewa kwanini unapanga mambo kama
hayo.:A S 114:
duhh hii lecture na zaidi ya ambayo angeipata stationary