Wakunyuti
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 380
- 13
Natafuta kazi Usalama wa Taifa,hata leo naomba mnipe tena naomba mnipe mapema
Nahitaji kazi ambayo nitaifanya kwa malipo madogo ila kwa ajili ya wanajamii
Nataka kuwasaidia kuwajua kwa undani wale waliochukua Pesa za EPA ili wajulikane
Nataka niajiliwe ili nionane na Rais na nimwambie yaliyo moyoni mwa watanzania
Nataka kazi usalama ili na mie nichukue pesa za EPA na niwagawie watanzania Masikini
Nataka tu sababu najua nikiwaomba pesa kwa njia ya kawaida hawatanipa.
Nafuta kazi ili niwape watanzania habari wanazotaka kujua
Niko tayari kufanya nao kazi kwa masharti ya uwazi na ukweli
Nataka Rais Ajue kwamba watu wanafanya ufisadi wa khali ya juu kwasababu ni rafikize
Nataka nimwambie Rais jinsi wachache wanavyowadharau walio wengi
Nataka nimwambie Rais ni watu wangapi mpaka sasa ni mafisadi wakubwa
Nataka kazi usalama ili nimjue vizuri rais wetu na tabia yake ya maamuzi
Nataka kazi usalama ili nifanye uchunguzi kuhusu BOT,
Nataka nimjue mmiliki wa Kagoda alipewa shilingi ngapi ?
Nataka niwajue waliorudisha Pesa za EPA mpaka sasa
Nataka kazi Usalama ili niwaambie watanzania ukweli ni wapi alipo Balali
Nataka kazi Usalama wa taifa ili nitoe majibu kuhusu Chenge
Natafuta kazi usalama ili niwaambie jinsi Dili ya RDC ilivyosukwa
Natafuta kazi ili nijue je Rais anawachukuliaje walihsuika na Richmond
Nataka kujua ni kwanini serikali hawatoi majibu ya Ripoti ya Richmons na EPA
Natafuta kazi siyo kwa ajili ya kumlinda Kada wa CCM wala kiongozi
Natafuta kazi ili kulisnda heshima ya nchi yetu
Natafuta kazi ili nchi hii iwathamini wafanyakazi na wakulima
Niko tayari kwa mshahara mdogo ila niwe huru kuwaambia wananchi
Ndiyo nataka Kazi Usalama wa Taifa na nataka Nafasi ya Ukurugenzi ndiyo ninayo itaka
Mzee hilo shairi limetulia...tutakusaidia kulifikisha kwa Pinda