Natafuta ajira ndani na nje ya Tanzania, nina shahada na uzoefu na kazi za bandari

Oct 21, 2022
15
29
Habarin Wana JF heshima yenu wote 🙏🏾 natumaini wote ni wazima kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa uzima anao tujaalia kila siku itwapo Leo.

Ndugu zangu mbele yenu ni kijana mtanzania nina ishi dar es salaam nime hitimu bachelor degree in shipping and logistics management mwaka 2022

Nina experince ya miaka miwili nime fanya kazi part-time mle bandarini (TPA) lakin nilikuwa silipwi ilikuwa najitolea from 2020-2022 April )nime fanya kazi maeneo ya container terminal ,MP shed pamoja na export

Nina uzoefu wa kutumia cargo systerm and tancis systerm ,pia container inspection, container handling na storage ndugu zangu

Wana JF naomba niende direct kwenye point kama Uzi unavyo jieleza nime kuja kwenu nina omba msaada wa kazi Kwa yeyote anae weza kunisaidia kupata kazi ndani ya field yangu hiyo pia nje ya hapo nita shukuru sana lakin pia mwenye connection ya kazi NJE YA TZ nipo tayar pia kuja kufanya kazi huko njee ya nchi

Passport ya kusafiria ninayo nipo tayar wakati wowote ule kusafiri kama ikipatikana nafasi nina shida sana ndugu zangu hapa nilipo

Mim binafsi ndio mtoto wa mwisho kwetu lakin ndio mtoto pekee ambae ame pata degree na ame graduate kwahio mama yangu mzazi na ndugu ambao wame kazana kunisomesha wapo Wana niangalia...

Wana hitaji msaada wangu ndugu zangu hapa nilipo nina ishi kwa rafik dar es salaam Nina ishi mazingira magum mnoo maana chakula najitafutia na sina kazi zaidi ya kuomba omba hela ya Kula

Kwa wadau ambao nao ime fika time Wana choka kunisaidia ndugu zangu nime teseka kuomba kazi mnoo nime peleka CV mle jay mo posta kwenye makampuni ya maritime lakin wapi sija itwa mle bandarin pia nime omba nirudi at least wanilipe kidog lakin wapi ime shindikana

Ndugu zangu Wana JF naiman humu kuna ma expert wa muda sana naombeni jaman mnisaidie nina tamani Sana kwenda nje ya nchi pia Nika fanye kazi huko maana pasi ya kusafiri ninayo

Wana JF wote nawapenda na kuwashemu Sana kijana wenu mtanzania nipo mbele yenu naombeni connection ya kazi napitia mateso mnoo kutafuta kazi ninacho shukuru Mungu huwa sikati tamaa kila siku nasali na kuomba ..

Lakin pia Nina chacharika kutafuta kazi ...Kwa yeyote atakae uwiwa kunisaidia kunipa connection ya kazi either ndani ya nchi au nje ya nchi Nita shukuru saana MTU huyo ata kuwa ame nisaidia Mim na ngudu wote Wana tarajia matunda kutoka kwangu

Naombeni yeyote ambae ata guswa na hali yangu anisaidie kama vile ana msaidia ndugu yake wa damu Naimani Mungu ata mzidishia sana yeye pamoja na vizazi vyake ..ndugu zangu wana jf nina wakilisha ombi langu kwenu 🤲🏾🤲🏾....

Kwa yeyote mwenye ushauri,wazo anisaidie yote mtakayo niambia Nita yapokea Kwa mikono miwili na Kwa moyo mweupe ...na popote nilipo onyesha mapungufu

Either kuwa kera au kuwa boa au kuwa udhi naombeni mnisamehe sana mim ni binadamu wa kawaida sana na sija kamilika hata ...

Ndugu zangu Imani yangu kubwa kutoka kwenu I hope I'll get a positive response Naimani mta nisaidia nashukuru sana na Mwenyezi MUNGU awa bariki wote. Amina
 
Back
Top Bottom