VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Joshua Nassari,mgombea ubunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki-CHADEMA si chaguo letu watazamaji,wasikilizaji,wafuatiliaji na washabiki wa vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi Arumeru Mashariki bali ni chaguo la wa-Meru wa Arumeru Mashariki.Wanamhitaji sana Nassari.Hawahitaji mbwembwe za kugawa fedha,kofia,fulana,vyakula na matusi.Wanamhitaji Mbunge aliye karibu yao.Wapo wazee walionidokeza kuwa hata Nassari angegombea kwa tiketi ya SAU,wangemchagua tu.
Jumapili,ingawa ni siku ya wajinga Duniani,ni siku muhimu sana kwa wana-Arumeru Mashariki.Wa-Meru watakuwa wajanja siku hiyo.Wako tayari kuwa-Wade CCM.Wamejiandaa vyakutosha.Wamejiandaa kupiga kura za kumtosha Nassari.Shahada zao za kupigia kura hazinunuliki.Wanasonga kwa mwendo wa ushindi..
Jumapili,ingawa ni siku ya wajinga Duniani,ni siku muhimu sana kwa wana-Arumeru Mashariki.Wa-Meru watakuwa wajanja siku hiyo.Wako tayari kuwa-Wade CCM.Wamejiandaa vyakutosha.Wamejiandaa kupiga kura za kumtosha Nassari.Shahada zao za kupigia kura hazinunuliki.Wanasonga kwa mwendo wa ushindi..