Nashindwa kulipa kupitia Vizacard mtandaoni

upangaj

Member
Aug 21, 2016
7
4
Ndugu zangu nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nimepatwa na changamoto ya kushindwa kulipia malipo mtandaoni kupitia visa card, nimetumia card ya TIGO,VODA na CRDB lakini nimeshindwa kufanikiwa kwa muda wa wiki moja sasa hata hivyo mwanzoni malipo yalikuwa hayasumbui kabisa nimefika ofisi zote hizo naambiwa hawana tatizo, Je kuna aliyepata changamoto hii kama mimi na tufanyaje kukwamuka hapo?
 
Je kuna aliyepata changamoto hii kama mimi na tufanyaje kukwamuka hapo?
Ni kweli hakuna changamoto.

Malipo huwa yanakataa iwapo tu salio ni dogo.

Fanya hivi: mfano unataka kulipia kitu cha TZS 50,000, kwenye simu yako umeweka asilimia 10 au zaidi ya kiwango kinachotakiwa, ili watoa huduma waweze kukata asilimia zao za huduma kabla ya kufanikisha muamala wako. Sababu ni viwango vya rate kati ya USD-TZS kubadilika mara kwa mara.
 
Ndugu zangu nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nimepatwa na changamoto ya kushindwa kulipia malipo mtandaoni kupitia visa card, nimetumia card ya TIGO,VODA na CRDB lakini nimeshindwa kufanikiwa kwa muda wa wiki moja sasa hata hivyo mwanzoni malipo yalikuwa hayasumbui kabisa nimefika ofisi zote hizo naambiwa hawana tatizo, Je kuna aliyepata changamoto hii kama mimi na tufanyaje kukwamuka hapo?
Unataka kulipia kwenye mtandao gani au huduma gani
 
Ni kweli hakuna changamoto.

Malipo huwa yanakataa iwapo tu salio ni dogo.

Fanya hivi: mfano unataka kulipia kitu cha TZS 50,000, kwenye simu yako umeweka asilimia 10 au zaidi ya kiwango kinachotakiwa, ili watoa huduma waweze kukata asilimia zao za huduma kabla ya kufanikisha muamala wako. Sababu ni viwango vya rate kati ya USD-TZS kubadilika mara kwa mara.
Hilo ninalifahamu nimetaka kulipa tsh362,700 na kwenye cm kuna 450,000 visa card ya benk account ina 3m lakini bado ni shida
 
visa card ya benk account ina 3m lakini bado ni shida
Fika tawi la benki yako la karibu, Waambie waongeze limit( By default limit huwa ni ndogo, kiusalama wa fedha zako). Mfano waweza kuwaaambia waweke limi ya 10,000,000 kwa miamala utakayoweza fanya ndani ya saa 24..

Ushauri: Pia omba wakufungulie account ya pili, Hii itakuwa si ya kuwekea fedha bali itakuwa maalum kwa manunuzi mtandaoni, Mfano unataka kulipia 500,000 basi unafanya kuhamisha kutoka account yako ya kawaida.

Karibu.
 
Back
Top Bottom