Ndugu zangu nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nimepatwa na changamoto ya kushindwa kulipia malipo mtandaoni kupitia visa card, nimetumia card ya TIGO,VODA na CRDB lakini nimeshindwa kufanikiwa kwa muda wa wiki moja sasa hata hivyo mwanzoni malipo yalikuwa hayasumbui kabisa nimefika ofisi zote hizo naambiwa hawana tatizo, Je kuna aliyepata changamoto hii kama mimi na tufanyaje kukwamuka hapo?