Kulipa kodi ni wajibu wa kila mtanzania.
Hakika Mtsweni
Kulipa kodi ni wajibu wa kila mtanzania.
Maskini kijana wa watu Diamond kachumia juani sasa wanataka kumtoa mbuzi wa kafara.
Si bure huyu kuna kitu kagombana na CCM..
Nilikuwa najaribu kuonyesha hata wanamziki wakubwa walivoonekana kukerwa na mambo ya kodi!! Huyo dube aliwahi kuulizwa kuwa anapinga watu wasilipe kodi? akajibu.....nataka kujua tu pesa yangu inaenda wapi na inafanya kweli lichokusudiwa! (au ndio zinakusanywa apewe Chenge?)
Team kiba Leo wanajifanya wazalendo
Ivi unaweza ukawa mtupu kiasi iki?
Nashangaa kwasababu ni diamond watu mnajidai wazalendo sana.
Wakati nchi hii hakuna anayelipa kodi halali zaidi ya waajiriwa tu.
Na hata kama wewe ni mjasiriamali nina uhakika hulipi kodi inayotakiwa
Serikali dhaifu hufukuzana na machinga kudai kodi huku ikiwaacha wafanyabiashara wakubwa wakitesa. Sasa Sethi na Diamond ni yupi wa kukabwa koo?
Tunashindwa kuelewa tu kutokana na umaarufu wa dlamond ndio uliofanya jambo ili kujulikana lakini ukwel ni kwamba kulipa kodi ni jukumu la kila raia katika nchi yoyote kinyume chake usipolipa kodi utatoa faini au kifungo jela!!! Tusiingize siasa kwenye mambo ya msingi
Mkuu zipo shughuli nyingi tu zenye kipato na haukatwi kodi kisheria
nyiingi tu......
Na kama sheria bado inakataza muziki kuwa ni shughuli ya kibiashara basi Diamond akipata mwanasheria mzuri halipi hata senti moja
kumbuka wakati wa Nyerere ilikatazwa muziki kuwa shughuli ya kibiashara
Thubutu, kwa sheria ya kodi ya sasa kila kipato lazima kilipiwe kodi, kwa sasa hata pesa ya kustaafu inakatwa kodi
Hoja yako ni General Sana, kwa mantiki hii hata bakhresa anahaki ya kuuliza makato ya kodi toka kwenye miradi yake inafanya kazi gani?......
esma ni nani??
mbona mkuu wa nchi na mzee pinda hawakatwi kodi yyte kwenye mishahara yaoNimesikitishwa sana na baadhi ya watu mnaowashangaa TRA kwa maamuzi hayo badala kuwapongeza.
Mimi binafsi naona wamechelewa, walitaliwa wafanye hili suala zamani sana.
Kimantiki, mtanzania yeyote anayepata kipato ni lazima alipe kodi.
Yaani mwl anaelipwa laki nne analipa kodi halafu mnashangaa TRA kufuatilia kodi za Diamond?
Tuwekeni mapenzi na itikadi pembeni, kodi ni lazima ilipwe.
Hapa sitaki kuzungumzia hzo kodi wanazosamehewa wakezaji, cziungi mkono hata kwa dawa, ila hazina uhusiano na ulipaji kodi wa Diamond
Sheria za nchi ndio zinzoongoza kazi za TRA. Kama Mkapa na Kikwete wameona wachimbaji wakubwa wa Madini wasilipe kodi, TRA haziwezi kufanya chochote.
Lakini kama ipo ndani ya sheria kumdai Diamond lazima alipe kodi. Mfanyakazi mwenye kipato kidogo kwa mwaka kuliko Diamond analipa kodi. Kwa Diamond asilipe?
Biashara pekee ya serikali popote ni kutoza kodi stahiki!
mbona mkuu wa nchi na mzee pinda hawakatwi kodi yyte kwenye mishahara yao