Prakatatumba abaabaabaa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2022
- 1,465
- 4,675
Fikiria hupo chama Cha chakuhawata alafu inatokea tu chama kingine (CWT) wanapitisha makato yako na umeshajitoa, Unaenda kwa afsa utumishi ( Hapo umeshamtafuta mwezi mzima hayupo ofsini) anakujibu short tu kwa dharau kwamba nenda huko CWT wakuandikie kwamba wewe sio Mwanachama wao uniletee hapa nikutoe, anasema hivyo anajua fika wewe kwenda CWT sio jukumu lako maana huo ni mshahara wako sio wa CWT na anajua fika kwamba CWT hawawezi kukusaidia kitu, unaenda huko CWT hawakupi ushiriakiano wowote, unarudi kwa afsa utumishi anakujibu Sasa "Mimi nifanyaje/nikusaidiaje?"
Unarudi shuleni na mawazo. Nafundisha physics na Mathematics form one mpaka form four, nitapata morale ya kufanya kazi? Itoke wapi? Mimi ni mtaaluma majukumu ya kitaaluma nitayatimizaje huku nikiwa na mawazo?
Dharau! Dharau! Dharau sio kitu kizuri, ukimletea mtu dharau sehemu ambayo anaona ni haki yake basi jiandae kuchukua matokeo ya dharau. Huyo Afsa utumishi anadharau kwa sababu Sina power,Sina hela na Sina heshima ndio ni ukweli, Ukiwa maskini lazima udharililike tu. Mshahara wa kwangu Mimi ndio na mamlaka nijiunge chama a au b, mtu anakataa kukuondoa kwa faida gani? Yeye anafaidika kwa lipi mtumishi kukatwa vyama viwili?
Walimu wanapambana sana kazi wanazozifanya ni nyingi mnoo, hawana allowance zozote, wanakaa Shule mpaka saa 11:30 jioni kwa malipo ya elfu 3-6 (remidial) yote ni kwa ajili ya kutimiza majukumu yao, ni sawa hatuna shida na hizo allowance tumeshakubali, Lakini? Wapeni malimbikizo yao ya mishahara (mshahara wangu wa kwanza sijawahi kulipwa Hadi Leo), Wapande madaraja kwa wakati, wakienda huko halmashauri/manispaa na matatizo yao wajibiwe kwa staha na ustaarabu maana huko halmashauri ndio sehemu pekee ya kutatuliwa changamoto, Lakini ajabu ni kwamba walio kwenye position ya kukusaidia hawakusaidii (hawaoni umuhimu wa kukusaidia) kumbuka hata hao Ma-afsa utumishi walikua walimu kabla wakaenda kujiendeleza.
Nimegundua huku ni changamoto kwakweli na Sioni kama nitakuepo kwa muda huku, hiki kijiti nitawaachia wengine wakikimbize na kulijenga taifa. Lakini WAJUE walimu wote sio fairule, tulifaulu vizuri form six tumezaliwa kwenye umaskini mkubwa sana tumekimbilia huku atleast tuanze kujitegemea mapema. Sasa ni wakati wa kuandaa mifumo kwa hasira kubwa na umakini mkubwa hata hiyo siku ikifika isiwe majuto bali ni ushindi.
Unarudi shuleni na mawazo. Nafundisha physics na Mathematics form one mpaka form four, nitapata morale ya kufanya kazi? Itoke wapi? Mimi ni mtaaluma majukumu ya kitaaluma nitayatimizaje huku nikiwa na mawazo?
Dharau! Dharau! Dharau sio kitu kizuri, ukimletea mtu dharau sehemu ambayo anaona ni haki yake basi jiandae kuchukua matokeo ya dharau. Huyo Afsa utumishi anadharau kwa sababu Sina power,Sina hela na Sina heshima ndio ni ukweli, Ukiwa maskini lazima udharililike tu. Mshahara wa kwangu Mimi ndio na mamlaka nijiunge chama a au b, mtu anakataa kukuondoa kwa faida gani? Yeye anafaidika kwa lipi mtumishi kukatwa vyama viwili?
Walimu wanapambana sana kazi wanazozifanya ni nyingi mnoo, hawana allowance zozote, wanakaa Shule mpaka saa 11:30 jioni kwa malipo ya elfu 3-6 (remidial) yote ni kwa ajili ya kutimiza majukumu yao, ni sawa hatuna shida na hizo allowance tumeshakubali, Lakini? Wapeni malimbikizo yao ya mishahara (mshahara wangu wa kwanza sijawahi kulipwa Hadi Leo), Wapande madaraja kwa wakati, wakienda huko halmashauri/manispaa na matatizo yao wajibiwe kwa staha na ustaarabu maana huko halmashauri ndio sehemu pekee ya kutatuliwa changamoto, Lakini ajabu ni kwamba walio kwenye position ya kukusaidia hawakusaidii (hawaoni umuhimu wa kukusaidia) kumbuka hata hao Ma-afsa utumishi walikua walimu kabla wakaenda kujiendeleza.
Nimegundua huku ni changamoto kwakweli na Sioni kama nitakuepo kwa muda huku, hiki kijiti nitawaachia wengine wakikimbize na kulijenga taifa. Lakini WAJUE walimu wote sio fairule, tulifaulu vizuri form six tumezaliwa kwenye umaskini mkubwa sana tumekimbilia huku atleast tuanze kujitegemea mapema. Sasa ni wakati wa kuandaa mifumo kwa hasira kubwa na umakini mkubwa hata hiyo siku ikifika isiwe majuto bali ni ushindi.