Burkinabe
JF-Expert Member
- Feb 12, 2023
- 1,893
- 3,200
Kwa kweli pasipo kupoteza muda, ninayo furaha ya dhati toka moyoni kwa hiki ambacho nimekiona kwa bunge la leo!
Yaani ni kama mgonjwa mahututi ambaye ghafla ameanza kupiga chafya!
Chafya ni dalili ya uhai.
Hongereni sana wabunge wote mliohusika kukemea vibaka walioko kwenye wizara mbalimbali ambao kazi yao ni kuiba na kuiba na kuiba tena!
Rais Samia Suluhu Hassan aliwaambia wajitathmini, lakini hadi sasa hatujaona mtendaji yeyote serikalini akijihudhuru au hata kuomba radhi tu kwa kile kilichotokea!
Wabunge naomba msiishie tu kutufurahisha wananchi wenu kwa maneno mazito mazito mnayoyasema huko, bali hakikisheni wahalifu wote wanachukuliwa hatua ili kuinusuru nchi yetu na hawa mchwa wanaokula kila kitu hadi vyuma wao wanakula tu!
Yaani ni kama mgonjwa mahututi ambaye ghafla ameanza kupiga chafya!
Chafya ni dalili ya uhai.
Hongereni sana wabunge wote mliohusika kukemea vibaka walioko kwenye wizara mbalimbali ambao kazi yao ni kuiba na kuiba na kuiba tena!
Rais Samia Suluhu Hassan aliwaambia wajitathmini, lakini hadi sasa hatujaona mtendaji yeyote serikalini akijihudhuru au hata kuomba radhi tu kwa kile kilichotokea!
Wabunge naomba msiishie tu kutufurahisha wananchi wenu kwa maneno mazito mazito mnayoyasema huko, bali hakikisheni wahalifu wote wanachukuliwa hatua ili kuinusuru nchi yetu na hawa mchwa wanaokula kila kitu hadi vyuma wao wanakula tu!