Naomba ushauri wa kisheria kuhusu Mwajiri kulazimisha nivunje mkataba

Isaack Newton

JF-Expert Member
Apr 15, 2013
535
224
Habarini wakuu!

Nimeleta suala hili kwenu wataalamu wa sheria ili mnisaidie.

Nafanya kazi kampuni fulani ambayo baada ya tamko la serikali kuhusu kuongezewa mishahara kwa sekta binafsi, kampuni imeshindwa kumudu hilo ongezeko la mishahara.

Mwajiri alichokisema ni kwamba yeye kashindwa kumudu kulipa huo mshahara mpya, sasa anachotaka kukifanya ni kwamba anasajili kampuni yake iwe kama local company na sio international company ili atulipe wafanyakazi kama local, sasa amesema sisi wenyewe TUSITISHE MKATABA.

Sasa je kisheria imekaaje, mtu unalazimishwa kuvunja mkataba afu usaini tena, kwa uelewa wangu mdogo ninaojua ni kwamba mwajiri ndo anisitishie mkataba maana mimi sijataka kusitisha mkataba. Wataalamu wa sheria za mikataba naomba msaada wenu.
 
Habarini wakuu!

Nimeleta suala hili kwenu wataalamu wa sheria ili mnisaidie.

Nafanya kazi kampuni fulani ambayo baada ya tamko la serikali kuhusu kuongezewa mishahara kwa sekta binafsi, kampuni imeshindwa kumudu hilo ongezeko la mishahara.

Mwajiri alichokisema ni kwamba yeye kashindwa kumudu kulipa huo mshahara mpya, sasa anachotaka kukifanya ni kwamba anasajili kampuni yake iwe kama local company na sio international company ili atulipe wafanyakazi kama local, sasa amesema sisi wenyewe TUSITISHE MKATABA.

Sasa je kisheria imekaaje, mtu unalazimishwa kuvunja mkataba afu usaini tena, kwa uelewa wangu mdogo ninaojua ni kwamba mwajiri ndo anisitishie mkataba maana mimi sijataka kusitisha mkataba. Wataalamu wa sheria za mikataba naomba msaada wenu.
pole sana,una mkataba wa muda gani au wa aina gani? umefanya kazi kwa muda gani? usikubali wewe kuvunja mkataba(resignation) labda mvunje mkataba kwa makubaliano ambapo utaweza kupata stahiki zako za msingi kama NSSF pia atalazimika kukulipa kiinua mgongo,notisi,mshahara wa mwezi husika,likizo n.k lakini ukiacha mwenyewe hautaweza kupata hivyo vyote zaidi ya mshahara,likizo na cheti cha utumishi,na kuhusu mwajiri kuwa ajiri tena hiyo ni bahati nasibu,nafikiri kwa hayo machche yatakupa mwanga katika kufanya maamuzi
 
Serikali ilitoa amended minimum wage order yani kwamba sekta tofauti binafsi kuongeza kima cha chini cha mshahara kutoka kile cha mwanzo mfano sekta ya madini ilikuwa 450,000 ikafika mpaka 500,000

Sasa hapa kabla ya kwenda mbele ni vyema kufahamu upo sekta ipi ili ufahamu iyo sekta inapaswa kulipwa bei gani kwa maelekezo mapya hapa ndo msingi ulipo

tuje kwenye suala la kuvunjwa kwa mkataba kwamba muajiri hawezi kumudu viwango vipya

Kwanza lazima tufahamu huo mkataba ulionao sasa ni waina ipi na unaukomo wa muda gani mfano kama ni wa muda maalumu yani fixed term contract hapa kuna 2 kama bado upo hai itapaswa uishe kwanza ndipo malipo mapya kwa mujibu wa ongezeko jipya au mkae chini kujadili kuboresha huo mkataba

Sasa basi mkataba ili uvunjwe na uwe na maslai kwa mfanyakazi ni lazima kifanyike kitu kinaitwa termination by agreement settlement of disputes yani mnakaa mezani pande zote 2 muajiri na muajiriwa alafu mnafikia makubaliano ya kuvunja mkataba sasa

katika makubaliano haya mfano mkataba umebakia miezi 6 muajiri atapaswa kulipia idadi ya miezi iliyobakia kwenye mkataba , notes, likizo na cheti cha utumishi


sasa waajiri wengi wanakwepa iyo kitu sasa kuwa makini na kitu kifuatacho



anaweza akafanya technical retrenchment yani anaweza akapunguza wafanyakazi kwa makusudi kwa sababu labda za kuyumba kiuchumi alafu katika watu ambao wamekataa kupunguziwa maslai ndo wakachaguliwa kupunguza hapa atafata taratibu zote ikiwa

kuitisha kikao cha wafanyakazi wote, kutoa taarifa ya kupunguza watu, kueleza sababu ya kupunguza watu na juhudi mbalimbali za kuokoa iyo hali na mwisho wa siku wakaondolewa wale wasiotaka kupunguza mshahara na kwa macho ya sheria ikawa salama japo sio salama


ushauri wangu usiache kazi mwenyewe wewe omba meza ya mazungumzo ya maridhiano muyamalize muachane kwa amani

kuhusu mafao ya NSSF kama mdau alivyosema hapo juu kama una elimu labda kuanzia diploma na kuendelea sahau kupata ela zote utalipwa asilimia 33% ya mshahara wako kila mwezi kwa miezi sita na kipindi kitafungwa hapo
 
Back
Top Bottom