Naomba msaada wa TENDE misikiti ya Rufiji

HM Hafif

JF-Expert Member
Aug 16, 2009
1,359
20
Assalamu alaykum.

Kwa waislamu wanaoweza kutoa msaada wa tende ili tutoe kwa waislamu wenzetu wa wilaya ya Rufiji, kuanzia jaribu mpakani, Bungu, Kibiti, Ikwiriri, Nyamwage, Chumbe mpaka Muhoro. na huku kuelekea mpaka nyamisati na salali, mpombwe, bila kusahau mkongo, kilimani, kipo ,mwaseni mpaka Nyaminywili.

Huko hali mbaya sana.
Tunaomba msaada.
 
Kwa waislamu wanaoweza kutoa msaada wa tende ili tutoe kwa waislamu wenzetu wa wilaya ya Rufiji, kuanzia jaribu mpakani, Bungu, Kibiti, Ikwiriri, Nyamwage, Chumbe mpaka Muhoro. na huku kuelekea mpaka nyamisati na salali, mpombwe, bila kusahau mkongo, kilimani, kipo ,mwaseni mpaka Nyaminywili.

Huko hali mbaya sana.
Tunaomba msaada.
.

hakika nazifahamu vizuri sehemu hizo, nilikuwa napita kwenda kuwinda Selou na Kingupira. kuna jama zangu pale Mkongo, Utete diwani na Ikwiriri na Mohoro.

Ok all in all, tuwasiliane kwenye mail na ubainishe unahitaji kiasi gani cha Tende tuangalie uwezekano.

Nakuomba sana usije ukatumia msaada huo kwa madhumuni ya kisiasa.

Dr Hamza Yousuf Al Naamani.
Doha
 
Dr hamza,
nimeshukuru kwa reply yako. Nimekutumia namba yangu ya simu ili tuweze fanikisha mambo haya haraka iwezekanavyo.

natanguliza shukurani. karibu sana Ikwiriri

hakika Allah atakulipa .
 
Nashukuru nimeipata Insh'Allah nitakupigia jioni baada ya magh'ribi.

swaumu njema
 
..siyo mnapeleka tende wakati wa Ramadhani halafu mnatokomea hadi Ramadhani nyingine.

..wananchi wa Rufiji na mikoa ya kusini kwa ujumla wanahitaji msaada mkubwa ktk masuala ELIMU.

..wasaidieni ktk kuboresha mazingira ya elimu pia.
 
hivi kweli tende ndio kitu cha kuomba na kusisitiza kwamba huko hali ni mbaya, hivi watu wanafungia tende au, hii msg au ombi halina maana na linadhalilisha uislamu
 
..kipindi hiki kitumike kugawa tende pamoja na vitabu vya masomo kama hisabati.

..kipindi hiki yafanyike mashindano ya kusoma Quran, na mashindano ya hisabati na chemsha bongo, uandishi wa insha na utunzi wa mashairi, Kaswida etc.

..HII NI KARNE YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.
 
..siyo mnapeleka tende wakati wa Ramadhani halafu mnatokomea hadi Ramadhani nyingine.

..wananchi wa Rufiji na mikoa ya kusini kwa ujumla wanahitaji msaada mkubwa ktk masuala ELIMU.

..wasaidieni ktk kuboresha mazingira ya elimu pia.
Mkuu....aisee kweli kabisa..na hiyo elimu sio madrassa kwa saaana...
 
..siyo mnapeleka tende wakati wa Ramadhani halafu mnatokomea hadi Ramadhani nyingine.

..wananchi wa Rufiji na mikoa ya kusini kwa ujumla wanahitaji msaada mkubwa ktk masuala ELIMU.

..wasaidieni ktk kuboresha mazingira ya elimu pia.
nafikiri Tanzania kuna sera maalum za Ilmu na wengi tunachangia hilo kupitia TEA, na halmashauri.

lakini suala la njaa halina mbadala. Ndio maana ukisoma magazeti ya leo ya huko Tanzania unaelezwa rais JK katembelea Longido kujionea hali ya Ukame.

Hakika vyote ni muhimu. kama waislam tuna wajibu mkubwa sana kuhakikisha kuwa Mwezi huu mtukufu wa ramadhani watu wote tunapata futari iwe tajiri au maskini.

Hiyo ni sera ya dini , ndio maana unaona walionacho wanatoa kwa wasionacho ili wote wafunge kwa furaha.

HM Hafif, tueleze bayana unahitaji kiasi gani? tupe data kamili.

Dr Hamza
 
nafikiri Tanzania kuna sera maalum za Ilmu na wengi tunachangia hilo kupitia TEA, na halmashauri.

lakini suala la njaa halina mbadala. Ndio maana ukisoma magazeti ya leo ya huko Tanzania unaelezwa rais JK katembelea Longido kujionea hali ya Ukame.

Hakika vyote ni muhimu. kama waislam tuna wajibu mkubwa sana kuhakikisha kuwa Mwezi huu mtukufu wa ramadhani watu wote tunapata futari iwe tajiri au maskini.

Hiyo ni sera ya dini , ndio maana unaona walionacho wanatoa kwa wasionacho ili wote wafunge kwa furaha.

HM Hafif, tueleze bayana unahitaji kiasi gani? tupe data kamili.

Dr Hamza

maneno yako Kuntu. Sisi Rufiji tuna UMAKURU ( Umoja wa maendeleo ya kujitolea Rufiji) Chini ya Uenyekiti wa Col Matope, na Prof Idrisa Mtulia, Idi Simba na wengine.hawa wanashughulikia mambo yote ya Elimu na mengineyo.

Sisi wengine ni wachangiaji wakubwa wa Elimu huko. Suala la Futari ni nyeti sana hususan mwezi huu. kwani mwezi huu utokea mara moja tu katika mwaka.

mahitaji yetu ni kama katuni 100 hivi za tende za kilo 20 each. hapo tutaweza kutoa swadaka kwa misikiti mingi sana huku.

lakini Dokta Hamza kama itapatikana ziada haitakuwa mbaya tutawapa waislam wengine wa jirani kama kilwa na mkuranga.

nakupigia simu naona upokei najua labda una swali. tuwasiliane dokta
 
maneno yako Kuntu. Sisi Rufiji tuna UMAKURU ( Umoja wa maendeleo ya kujitolea Rufiji) Chini ya Uenyekiti wa Col Matope, na Prof Idrisa Mtulia, Idi Simba na wengine.hawa wanashughulikia mambo yote ya Elimu na mengineyo.

Sisi wengine ni wachangiaji wakubwa wa Elimu huko. Suala la Futari ni nyeti sana hususan mwezi huu. kwani mwezi huu utokea mara moja tu katika mwaka.

mahitaji yetu ni kama katuni 100 hivi za tende za kilo 20 each. hapo tutaweza kutoa swadaka kwa misikiti mingi sana huku.

lakini Dokta Hamza kama itapatikana ziada haitakuwa mbaya tutawapa waislam wengine wa jirani kama kilwa na mkuranga.

nakupigia simu naona upokei najua labda una swali. tuwasiliane dokta

As discussed in the phone. wasiliana na Islam kesho atakupa kila kitu.

Nimefurahi sana kusikia Col Mzee matope, Huyu bint yake Fatma matope alisoma na mke wangu jangwani sec na zanaki high sch. Bint alikuwa rafiki sana wa mke wangu na alikuwa na akili sana darsani. Prof Idrisu Mtulia yeye ni jirani yangu sana pale Upanga. yeye yupo mazengo mimi Alikhan.

Nilipata kusikia kidogo kuhusu hii UMAKURU kupitia balozi wa Tanzania nchini saudi Arabiya jaji Hamisi Msumi.
 
hivi kweli tende ndio kitu cha kuomba na kusisitiza kwamba huko hali ni mbaya, hivi watu wanafungia tende au, hii msg au ombi halina maana na linadhalilisha uislamu

Mkuu kipindi hiki cha toba Tende ni muhimu sana tena mno.
 
Dokta Hamza na Mkeo na Familia yenu, napenda kutoa shukrani zangu za dhati, mzigo nimepata katuni 117 za tende aina ya hanees jioni ya leo ila tu nilikuwa sikuwa na usafiri wa kuzichukua. Namshukuru pia Sheikh Islam yeye anatoa usafiri wa kuzipeleka mpaka Ikwiriri kisha mimi nitazisambaza.

Kwa Kweli Allah atawalipa zaidi na zaidi sheikh.

Shukrani sana sana
 
assalamu alaykum.

Kwa waislamu wanaoweza kutoa msaada wa tende ili tutoe kwa waislamu wenzetu wa wilaya ya rufiji, kuanzia jaribu mpakani, bungu, kibiti, ikwiriri, nyamwage, chumbe mpaka muhoro. Na huku kuelekea mpaka nyamisati na salali, mpombwe, bila kusahau mkongo, kilimani, kipo ,mwaseni mpaka nyaminywili.

Huko hali mbaya sana.
Tunaomba msaada.

hebu fanya harambee ya maana bana,wasaidiwe kwa kusomesha watoto wao na sio kuwapa tende,
 
Assalamu alaykum.

Kwa waislamu wanaoweza kutoa msaada wa tende ili tutoe kwa waislamu wenzetu wa wilaya ya Rufiji, kuanzia jaribu mpakani, Bungu, Kibiti, Ikwiriri, Nyamwage, Chumbe mpaka Muhoro. na huku kuelekea mpaka nyamisati na salali, mpombwe, bila kusahau mkongo, kilimani, kipo ,mwaseni mpaka Nyaminywili.

Huko hali mbaya sana.
Tunaomba msaada.

Kweli hiki ni kipindi kigumu sana kwa Waislam ambao ni maskini hakika wanateseka sana,
Wanaitaji kusaidiwa juzi nilikuwa Tilapia nikaona jamaa wamekuja kubalizi na kula vitu nikajiuliza kwa wale wenye kipato cha chini inakuwaje maana muda wakutoka kazini unapungua mahitaji yanaongezeka na matumizi na pia mwili unakuwa hauna nguvu kutokana na kushinda njaa.

Miogo ipo juu viazi kila kitu kiko juu Kwakweli wenye uwezo wawasaidie hawa ndugu zetu.

Poleni sana kwa hiki kipindi
 
Hivi lazima mgeze hata kula matunda ya kiarabu? Au ndio usilamu kusujudu uarabu?

Tanzania imejaa matunda kede kede, lakini hawa jamaa lazima waweke umanga. Sasa wanombana tende kwenye mtandao. Huko rufiji kumejaa mabibo, kule hayo.

Hii si dini ya wote bali inaonyesha kwa hali kubwa sana kuwa ni ya waarabu.

Kaazi kweli kweli
 
Hivi lazima mgeze hata kula matunda ya kiarabu? Au ndio usilamu kusujudu uarabu?

Tanzania imejaa matunda kede kede, lakini hawa jamaa lazima waweke umanga. Sasa wanombana tende kwenye mtandao. Huko rufiji kumejaa mabibo, kule hayo.

Hii si dini ya wote bali inaonyesha kwa hali kubwa sana kuwa ni ya waarabu.

Kaazi kweli kweli

waafrika especially wa waTz wana pombe zao za asli kama mbege, dengerua, ulaka, tembo, ulanzi, chimpumu,lubisi nk. sasa vipi kule kanisani wanapewa DIVAI ambayo ni ya kizungu.
Hii si dini ya wote bali inaonyesha kwa hali kubwa sana kuwa ni ya wazungu.
kazi kweli kweli
 
Dokta Hamza na Mkeo na Familia yenu, napenda kutoa shukrani zangu za dhati, mzigo nimepata katuni 117 za tende aina ya hanees jioni ya leo ila tu nilikuwa sikuwa na usafiri wa kuzichukua. Namshukuru pia Sheikh Islam yeye anatoa usafiri wa kuzipeleka mpaka Ikwiriri kisha mimi nitazisambaza.

Kwa Kweli Allah atawalipa zaidi na zaidi sheikh.

Shukrani sana sana
.

Mashuur ya Hafif,
Naelewa sana wagalatia inawauma sana kupewa huu msaada wa Tende. lakini hata ikiwauma lakini lengo letu limefanikiwa watu wapate futari nzuri wakati huu ramadhani.

unajuwa sana mwezi wa ramadhani watu wanapoteza sana nguvu hivyo wanapofungua wanahitaji glucose kwa wingi sana kurejesha nguvu. sasa kwenye tende unapata glucose kwa wingi sana.

hata mkichukia lakini watu watakula tende.
 
Kwa waislamu wanaoweza kutoa .....jamani ambao si waislamu hawawezi kujumuika?samahani kama nimewakwaza.
 
waafrika especially wa waTz wana pombe zao za asli kama mbege, dengerua, ulaka, tembo, ulanzi, chimpumu,lubisi nk. sasa vipi kule kanisani wanapewa DIVAI ambayo ni ya kizungu.
Hii si dini ya wote bali inaonyesha kwa hali kubwa sana kuwa ni ya wazungu.
kazi kweli kweli

Kwenye Biblia imeandikwa (Luka 22:18) kuwa divai itakayotumika kwenye misa au ibada inatakiwa iwe ni mvinyo unaotokana na "tunda la mzabibu". Isitoshe Divai ni sehemu ya ibada kwenye Ukristo.

Jee, kula tende ni sehemu ya ibada ya Kiislamu? Wapi kwenye Kurani imeandikwa Waislamu wanatakiwa kula tende pamoja na futari?
 
Back
Top Bottom