omtiti
JF-Expert Member
- Jun 19, 2019
- 1,022
- 1,590
Nakumbuka wakati tuhuma na hatimae kesi iliowahusu Babu Seya na Mwanae Papii kocha, ilisemekana kesi yao ilikua ni ya kutengenezwa(uonevu),na baadhi ya raia walilalamika Sana, hata hivyo walipigwa (life sentence imprisonment) ,kifungo cha maisha.
Katika watu wenye vyanzo vingi vya kupata habari ni rais wa nchi.
Rais Magufuli aliposamehe wafungwa hapo siku zilizopita, aliwasamehe pia Babu Seya na mwanae Papii Kocha ,na kosa ambalo liliwatia hatiani kina Babu Seya, ukiliangalia ni kama halikustahili msamaha. Japo rais ndio mwenye mamlaka ya kila kitu nchini kwa mujibu wa katiba (final say).
Rais Magufuli naamini kabla ya kuwaachia alijiridhisha pasi na Shaka kuhusu kesi ya Babu Seya.
Nani waliokua nyuma ya dhulma waliotendewa hawa raia, kiasi imefanya wapotee katika fani ya muziki wa Rhumba ya kikongo ilioimbwa kwa kiswahili na kubamba watanzania wengi Sana ?
Na wako wapi kwa sasa,?mbona hawasikiki?. anaejua taarifa zahawa watu tujuzane
Katika watu wenye vyanzo vingi vya kupata habari ni rais wa nchi.
Rais Magufuli aliposamehe wafungwa hapo siku zilizopita, aliwasamehe pia Babu Seya na mwanae Papii Kocha ,na kosa ambalo liliwatia hatiani kina Babu Seya, ukiliangalia ni kama halikustahili msamaha. Japo rais ndio mwenye mamlaka ya kila kitu nchini kwa mujibu wa katiba (final say).
Rais Magufuli naamini kabla ya kuwaachia alijiridhisha pasi na Shaka kuhusu kesi ya Babu Seya.
Nani waliokua nyuma ya dhulma waliotendewa hawa raia, kiasi imefanya wapotee katika fani ya muziki wa Rhumba ya kikongo ilioimbwa kwa kiswahili na kubamba watanzania wengi Sana ?
Na wako wapi kwa sasa,?mbona hawasikiki?. anaejua taarifa zahawa watu tujuzane