LILENDI
JF-Expert Member
- Oct 27, 2013
- 1,400
- 496
Mimi ma-house girl wangu wote wanakaa nao vizuri sana, maana siku MAMA NG'INA akinuna, wananitunuku na kuniondolea stress!
mkuu hatareee
Mimi ma-house girl wangu wote wanakaa nao vizuri sana, maana siku MAMA NG'INA akinuna, wananitunuku na kuniondolea stress!
hawa watu wapo ila cha kufanya unamwambia hapohapo kwamba si sahihi,niliwahi kupata wageni ilikuwa ni familia ya watu sita baba mama na watoto wao wanne,wakakuta mimi na binti yangu wa kazi tunawaandalia chakula ikabidi nitenge watoto wakae dinning na binti yangu akawa anakula nao,huyu mama mgeni hakupata amani gafla akaanza kumtuma binti yule wa kazi kwa vile nilimuelewa nikamwambia aniagize mimi anachotaka kwani yule anakula,hapo pozi lilimuisha na baadae mume wake akashukuru kwamba mke wake atajifunza maana huwa anawatenda vibaya mabinti(mke hakusikia mume alichosema),kipindi kingine tukaenda kwao nikaona amefanya nilivyofanya kwangu sema akawa anajisahau anamwambia "dada acha kula kwanza njoo utoe vyombo" ambapo angeweza kufanya mwenyewe,tuwathamini na kuwapenda wadada wanaotusaidia kazi,
Nilihuzunika sana mama mwenye nyumba alipotamka maneno haya.
Hii imenitokea nilipoenda kwa rafiki yangu niliyesoma naye O level miaka ya 90. Nilishangaa kuona ingawa yeye ndiye aliyeandaa chakula, kilipofika mezani yeye alikuwa ameketi kwa mbali anangojea tumalize kula ili naye aje kusaza mabaki.
Nilishindwa kuvumilia baadae nikauliza-wakati tunaendelea kula - iwaje msichana wa kazi hajajumuika nasi mezani.
Shemeji aliibuka na kujibu, nanukuu 'nani ale chakula meza moja na housegirl? Niliposikia maneno hayo nilikaa kimya, maana shemeji alionekana wazi hapendi kula chakula pamoja na housegirl.
Chondechonde mnaoishi na hawa mugro, jamani tuwachukulie mamugro aka beki tatu kama binadamu, kama anakupikia mlo, anakulelea wanao, na mambo mengine mengi, inakuwaje unamchukulia kama mbwa au paka anayengojea bosi ale halafu yeye atupiwe mifupa au makombo! Tubadilike jamani hasa nyie kina mama wenye nyumba, mweeeeee!
Nimesikia eti kuna wengine wanatumia mikojo kama liquid ya kupikia!
na wengine wanatumia mashine zao kuwanyonyesha watoto (h - boys!)
mmh.. hawa jamaa hawa nao wana vimbwanga vyao jamani!
Nilihuzunika sana mama mwenye nyumba alipotamka maneno haya.
Hii imenitokea nilipoenda kwa rafiki yangu niliyesoma naye O level miaka ya 90. Nilishangaa kuona ingawa yeye ndiye aliyeandaa chakula, kilipofika mezani yeye alikuwa ameketi kwa mbali anangojea tumalize kula ili naye aje kusaza mabaki.
Nilishindwa kuvumilia baadae nikauliza-wakati tunaendelea kula - iwaje msichana wa kazi hajajumuika nasi mezani.
Shemeji aliibuka na kujibu, nanukuu 'nani ale chakula meza moja na housegirl? Niliposikia maneno hayo nilikaa kimya, maana shemeji alionekana wazi hapendi kula chakula pamoja na housegirl.
Chondechonde mnaoishi na hawa mugro, jamani tuwachukulie mamugro aka beki tatu kama binadamu, kama anakupikia mlo, anakulelea wanao, na mambo mengine mengi, inakuwaje unamchukulia kama mbwa au paka anayengojea bosi ale halafu yeye atupiwe mifupa au makombo! Tubadilike jamani hasa nyie kina mama wenye nyumba, mweeeeee!
Kuna watu utafikiri wao ni special sana....wanashindwa kureason kabisa....huyo housegal ndiye unayemuachia nyumba...ndiye anayekutunzia watoto...anawalisha wanao eti leo huwezi kaa naye meza moja.....
Mungu awasamehe wote wenye tabia kama huyu mama...
yaaani mimi najisikia vibaya hawa watu wakiteseka
wamenilea tangu chekekea mpaka leo niko first year
na kwetu ukija huwezi kujua nani dada wa kazi nani binti wa mwenyenyumba
wote tunapendezeshwa kwa usawa kuanzia chini hadi juu
ingawa mimi ni wa mwisho na wa kike pekeee no kudekadeka kazi kama kawa
na kama nipo home dada huwa anapumzika siku ya jumamosi me ndo nashika usukani yaani mpaka uchunguze sana ndo utajua
na binti hata kwenda kwao hataki tuko nae mwaka wa 7 anasema kuacha kwake kazi hadi atakapoolewa