Nahitaji mwanamke wa kuzaa naye

Duh hii kali sana na ni mtihani mkubwa mno ndugu. Pole sana ila sasa kuzaa tu halafu usioe itakuwa ngumu kidogo mkubwa
 
Nahitaji mwanamke wa kuzaa naye. Nina mke lakini kwa bahati mbaya kwa majaaliwa ya Maanani hakujaaliwa kupata kizazi na baada ya kuhangaika kwa muda mrefu nchini na nje madaktari wametuambia kuwa si rahisi kuweza kuzaa kulingana na tatizo alilonalo. Baada ya kulitambua hilo, na kwayeye kuthamini juhudi zangu za kumshughulikie yeye kwa ghrama zote kote duniani na kushindikana hatimaye tumekubaliana kuwa nitafute mwanamke nizae naye. Si hitaji kuoa kwakuwa siwezi kuwa na wanawake wawili na siwezi kumwacha niliyenaye kwakuwa hastahili kuachwa. Niko tayari kumtunza mwanamke atakayekubali hilo kwa 100% kwa kila kitu chake na kizazi chake atakapojaaliwa kwakuwa uwezo upo, nia ipo na sababu ipo. Ningependa kuadopt pia lakini kama binadamu ningependa nione damu yangu pia kila mtu analifahamu hili. Ni maamuzimagumu kufanya lakini tumefanya pamoja. Aliyetayari juu ya hili twaweza wasiliana. Niko makini juu ya hili.

Pole sana na dilema hii. But, on the other hand, you should seriously consider that what is happening to you might be a mesage that God did not want you to have children. So, nakushauri usilazimishe kuwa na mtoto
 
Ndugu zangu nawashukuruni sana kwa jinsi mlivyonifariji, sikutarajia hata kidogo kupata positive and constructive ideas. Mliusoma ujumbe wangu kwa makini, mkautafakari, mkauelewa, mkaingiwa na huruma na kisha mkakubali kutumia muda wenu kuniandikia kwa lengo la kunishauri, kunipa pole, kunifariji na kisha kunipa matumaini mapya na mori kwamba kwake yeye Muweza hakina kinachoshindikana panapopatikana mapenzi yake. Nawashukuruni tena kwa hayo yote. Kuna walioniandikia kwa wazi na walioniandikia kwa siri, nyote nawashukuru sana. Mawazo yenu na ushauri wenu ni hazina kubwa sana kwangu. Kwakutilia maanani umuhimu wa kila lililosemwa nanyi nimeamua kutengeneza matrix ila kila wazo lililotolewa nilizingatie katika kufanya maamuzi magumu. Kwa mujibu wa jumbe nyingi tofauti nilizopokea wazini na sirini, nimejifunza kwamba UKWELI UNALIPA kwakuwa niliyowaeleza ninyi hayakuwa jokes za net bali ni dhahiri yaliyonifika na nimejifunza kuwa ya KHERI HUENDA KIKHERIKHERI. Mmenikumbusha baadhi ya methali zisemazo MFICHA UCHI HAZAI na MSEMA KWELI NI MPENZI WA MUNGU ili mradi tu ukweli huo hauathili your personal family life, maana nisingesema kidagaubaga nisingeyapata niliyoyapata toka kwenu. Wabillah tawfiq, Mungu awabariki sana.
 
Dena, unachosema ni sahihi si kitu rahisi sana. Kuna mmoja kati ya mia asiyetaka kuolewa kwa sababu zake na akataka labda kuwa a caerrer woman kwa hiyo kuwa na mume kwake ni mzigo. Huenda akapatikana huyo. Bado naomba
 
Ndugu yangu Mpita njia, Msiba kwa jirani si kwako. Usiombe ufikwe na hili. Sirahisi kusema kwamba nimeamua sizai wakati ninauwezo wa kuzaa. Customs na traditions za Wazungu nitofauti kidogo na za kiswahili. Nimeona umuhimu wa mtoto pale mimi nilivyoweza kubadilisha maisha ya wazazi wangu na kuwatunza katika umri waliokuwa nao. Ninapopata picha hiyo huwa najiuliza kulikoni mimi nitakapokuwa nahitaji msaada kama huu unohitajika na wazazi wangu sasa? Ingawa nafahamu kuzaa si kupata na unaweza kustrugle usifanikiwe lakini huwezi kufanikiwa bila kustrugle. Nafanya kazi sana na kutafuta pesa kwa juhidi sana je ni kwa ajili ya nini, ni mimi tu na mke wangu je na baada ya sisi kuondoka ni nani? Sitaki kuadopt kwakuwa ninashida ya mtoto bali katika mipangilio yangu nita adopt hata kama nikipata mtoto kwa ajili ya kutoa mchango wangu kwa jamii ya watu wasiojiweza na kutokuwa na matarijio ya future. Lakini si kuacha kwakuwa Mungu ametaka iwe hivi bali ni kutafuta ufumbuzi uliomakini wajinsi gani ya kuweza kupata bila kukarahisha nafsi zinazonizunguka. Si kweli kwamba watoto wote wakambo ni wabaya, ninamifano mitatu hai ya rafiki zangu wakaribu ambao wanawaleo mama zao wa kambo kwa kiwango cha hali ya juu sana kulingana na malezi waliyopata kutoka kwa mama zao hao wakambo. Kwa mtaji huo ninaimani inaweza kuhold kwangu pia ingawa si lazima sana. This is a very complex issue particularly for an educated person who nalyses issues in depth.
 
Pamoja na yote kabla hatujakusaidia; mlete shemeji atujulishe kuwa huu mpango ameshirikishwa vilivyo! Isije kuwa tunabariki mpango KANDO!
 
Pamoja na nia yako, na hamu yako kubwa ya kupata mtoto (kitu ambacho ni chema) nakushauri uone pia imani yako ya dini inasemaje kuhusu hicho unachotaka kukifanya. Je, kinakubalika? Kama kinakubalika songa mbele. Kama hakikubaliki, pokea mapenzi ya Mungu, nawe utaishi kwa furaha na amani hata bila kuwa na mtoto. Usilazimishe mambo ndugu!
 
umeongea pointi sana dearest kwa kusali kwa imani inawezekana kabisa kizazi kikaachia na mkeo akapata mtoto ila unatakiwa uwe unaomba halafu hata usisubiri we endelea tu na maisha siku itakayotiki hata hutoamini macho yako. ila unapoanza kumwambia awashrikishe kina rev masanilo naona unaleta utani sasa

Certainly prayers turns Impossibles. God who created your wife knows every detail, every fault and failure, hence He is able to RESTORE her.
Go to servants of God who will pray for you (both) and the blessing of children will come to pass. I have seen some friends without children for about 20 years, going to all best doctors and witchdoctors and failed but as they realized that God may do it, they went to His servants for prayers and certainly it was their breakthrough. Do that and you will live your dream before going to your conflicting and thoughts which will lead your family "scattered" for generations.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom