wananchi walikuwa wanamtaka mama Kaboyoka "mama maendeleo" baada ya kumchoka Ndhira Yona lakini CCM na mama Kilango wakamfanyia mizengwe. wananchi walifikia mpaka kupeperusha bendera za CCM nusu kuonyesha kukasirishwa kwao na mizengwe ya CCM. vitisho na mizengwe ilitumika kuwalazimisha wana CCM wa same mashariki kumchagua mama Kilango.
mama kilango amekuwa fundi wa kupiga makelele ya ufisadi na kutafuta umaarufu katika vyombo vya habari. huku same mashariki ameshindwa kabisa kusimamia na kuhamasisha shughuli za maendeleo.
ELIMU IMEDORORA: kwa kipindi cha miaka mitano, mama Kilango ameshindwa kulikwamua jimbo letu toka kushika mkia mkoani Kilimanjaro katika matokeo ya mitihani ya kitaifa.
KILIMO,MAJI,na MAZINGIRA: kuna ufisadi wa kutisha katika ukataji miti na uchimbaji udongo ktk maeneo ya misitu na vyanzo vya maji vya wilaya ya Same. hali hii inatishia kuua kilimo cha umwagiliaji na kusababisha balaa kubwa la njaa wilayani Same. wakati wananchi wamekuwa wakimhitaji nyumbani kuongoza vita vya kupambana na ufisadi huu, yeye amewatupa mkono na badala yake kupigana vita ya kiini macho ya EPA.
wananchi tunamtaka chaguo letu la mwaka 2005 Naghenjwa Kaboyoka "mama maendeleo."
mama kilango amekuwa fundi wa kupiga makelele ya ufisadi na kutafuta umaarufu katika vyombo vya habari. huku same mashariki ameshindwa kabisa kusimamia na kuhamasisha shughuli za maendeleo.
ELIMU IMEDORORA: kwa kipindi cha miaka mitano, mama Kilango ameshindwa kulikwamua jimbo letu toka kushika mkia mkoani Kilimanjaro katika matokeo ya mitihani ya kitaifa.
KILIMO,MAJI,na MAZINGIRA: kuna ufisadi wa kutisha katika ukataji miti na uchimbaji udongo ktk maeneo ya misitu na vyanzo vya maji vya wilaya ya Same. hali hii inatishia kuua kilimo cha umwagiliaji na kusababisha balaa kubwa la njaa wilayani Same. wakati wananchi wamekuwa wakimhitaji nyumbani kuongoza vita vya kupambana na ufisadi huu, yeye amewatupa mkono na badala yake kupigana vita ya kiini macho ya EPA.
wananchi tunamtaka chaguo letu la mwaka 2005 Naghenjwa Kaboyoka "mama maendeleo."
Wanaomhujumu mgombea ubunge wa CCM Same waonywa
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya same, Bw. August Kessy amesema kuanzia sasa viongozi wa ngazi zote wanaomhujumu mgombea Ubunge wa Jimbo la same Mashariki kupitia Chama hicho, Bi. Anne Kilango, wataondolewa.
Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Shule ya Msingi Kambene Kata ya Miamba Bw. Kessy alisema kuna viongozi ambao wamekuwa mwiba mkali kwa kampeni hizo, kutokana na kuchochea uasi.
Bw. Kessy alisema kutokana na hali ya kampeni kudorora katika Kata nyingi, ameamua kupeleka taarifa mkoani, kuelezea tatizo hilo.
Nimeshapeleka taarifa mkoani wameniruhusu kumuondoa kiongozi yoyote, ambaye ataleta vurugu na mgawanyiko wa kichama wakati wa kampeni, hata kama kiogozi huyo anaondolewa na vikao kwa mujibu wa katiba, lakini mimi nitamuondoa kwa muda hadi kampeni zimalizike, ndipo vikao vikae, sasa hivi hatuna muda,alisema Mwenyekiti huyo.
Alisisitiza kwamba viongozi hao, ni wale ambao hawakufarahishwa na mgombea ubunge aliyeteuliwa na CCM.
Alisema viongozi hao pamoja na wananchi, wamekuwa wakisusia mikutano ya kampeni ya mgombea huyo wa CCM.
Jamani kura za maoni sasa hivi ni historia, lakini kwa Jimbo la Same Mashariki, bado kura za maoni ni tatizo. Matokeo yake yamesababisha kudorora kampeni zetu bila sababu za msingi,alisema Bw. Kessy.
Mwenyekiti huyo, alitoa karipio hilo, baada ya kupita kwa maandamano na kukuta bendera za CCM zinapeperushwa nusu mlingoni, kama ishara ya maombolezo.
Alisema kwa vyovyote hatua hiyo, ina mkono wa viongozi, jambo ambalo lilipingwa vikali kwa kiapo na Mweneykiti wa Kata hiyo Bw. Pagu Mkulu.
Tangu kuanza kwa kampeni za mgombea huyo, wananchi wamekuwa wakisusia mikutano yake, kuzomea na kurusha mawe kwa sababu zinazoelezwa kwamba chanzo chake ni kura za maoni, ambapo mgombea anayekubalika na wananchi wengi Bi. Naggy Kaboyoka alitemwa.
Hata hivyo, Bw. Kessy alisema hata kama wananchi hawampendi Bi. Kilango ni vema wakaja kumsikiliza, badala ya kususia mikutano yake.
Pale Mjema na Bombo Kata nzima walikuja watu saba kwenye mkutano, hapa kuna tatizo, pia kuna kukosa uungwana kwa viongozi na wanachama wa CCM,alisema.