Mzizima, Tanga: Watu 8 wauawa kwa kuchinjwa shingo na watu wasiojulikana

Watu 8 wamechinjwa na miili yao kutenganishwa na vichwa akiwemo mjumbe wa serikali ya mtaa kufuatia vikundi vya uhalifu kuvamia nyumba za wakazi wa mtaa Kibatini uliopo kata ya Mzizima jijini Tanga hatua ambayo imeleta hofu kubwa kwa wananchi wa maeneo hayo.



Wakizungumza katika eneo la tukio baadhi ya waathirika ambao ndugu jamaa na zao wamechinjwa majira ya saa saba usiku wamesema kundi la watuhumiwa wanaokadiriwa kuwa walikuwa watu nane na kuvalia nguo nyeusi walipofika katika nyumba zao waliwaamuru akina baba watoke nje kisha kuwapeleka hadi katika vichaka kisha kuwachinja.





Tukio hilo limekuja wiki mbili tu baada ya vikundi hivyo vya uhalifu vinavyodaiwa kujificha katika mapango ya Amboni Mleni Maji moto kuchinja mbuzi 48,ng'ombe wawili na kuku zaidi ya 12 lakini Kamanda wa Polisi amekiri kuwa tukio hilo ni kubwa na kwamba jitihada za polisi zinafanywa ili kuhakikisha kuwa watuhumiwa wanakamatwa na kutiwa mbaroni.




Hata hivyo ndugu wa mjumbe wa serikali ya mtaa wa Kibatini ambaye naye ni miongoni mwa waliochinjwa amesema chanzo cha kundi hilo kuwafanyia unyama huo inatokana na kukamatwa kwa watoto wa watuhumiwa ambao ndio waliokuwa wakitumwa kabla makundi hayo hayafanya uhalifu.



Chanzo-ITV


#‎Habari‬
:Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yalaani mauaji ya watu nane waliouawa kwa kukatwa na mapanga katika Mkoa wa Tanga na kutaka serikali ichukue hatua za kuhakikisha usalama wa watu.
Imesema mwezi uliopita watu 20 wameuawa katika matukio tofauti na kuleta wasiwasi katika jamii hizo.
 
Taarifa ya Polisi Tanga kuhusu Watu 8 kuuwawa kwa kukatwa mapanga saa saba usiku

Kamanda wa Polisi Tanga Leonard Paul amesema ilikua saa saba usiku wa kuamkia May 31 2016 kwenye kitongoji cha Kibatini kata ya Mzizima wilaya ya Tanga umbali wa kilomita 40 – 45 kutoka Tanga mjini sehemu ambako kuna msitu kabla ya kukuta nyumba zipatazo 20 Majambazi walivamia wakiwa na visu na mapanga.

Walivamia nyumba tatu na kuua watu wote hao 8 kwa kuwakata mapanga shingoni pia waliiba biskuti, mchele na sukari na baada ya wizi huo walitokomea msituni maeneo ya Amboni ambayo yanazungukwa na kitongoji hicho cha Kibatini.

Kwa kumalizia Kamanda Leonard Paul amesema >>> ‘Jeshi la Polisi linashirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuwasaka wauaji hao, hakika tutawakamata….. ndugu Waandishi nisingependa kusema mengi sasa kwani yanaweza kuingilia upelelezi wa shauri hili’
 
Usalama wa nchi ni haba sana!ni presha kila kukicha ukirudi na kuamka salama unamshukuru Muumba. tahadhari chukua hatua! !!
 
Mh Mh mh........

Am speechless, Maumivu ya kichwa huanza taratibu, na baadaye kusambaa mwili mzima then husababisha kifo..!!! Mara kadhaa Serikali imekanusha juu ya uwepo wa kikundi hiki cha kigaidi huko Tanga. Haya yanathibitisha nini?

Hivi ile Intelijensia ya Polisi iko wapi kwa Matukio kama haya? Wenzetu Nigeria walianza namna hii, huko Kenya hali ilikuwa kama hii. Sisi Tanzania si Malaika kiasi yasitupate mambo haya...Kikubwa tujifunze kung'amua hatari na viashiria vya Ugaidi kama hivi. Polisi, Jeshi la Wananchi washirikiane kwa pamoja kutokomeza vikundi hivi kabla havijamea mizizi

Otherwise tutalia na kusaga meno.

BACK TANGANYIKA
 
Mh Mh mh........

Am speechless, Maumivu ya kichwa huanza taratibu, na baadaye kusambaa mwili mzima then husababisha kifo..!!! Mara kadhaa Serikali imekanusha juu ya uwepo wa kikundi hiki cha kigaidi huko Tanga. Haya yanathibitisha nini?

Hivi ile Intelijensia ya Polisi iko wapi kwa Matukio kama haya? Wenzetu Nigeria walianza namna hii, huko Kenya hali ilikuwa kama hii. Sisi Tanzania si Malaika kiasi yasitupate mambo haya...Kikubwa tujifunze kung'amua hatari na viashiria vya Ugaidi kama hivi. Polisi, Jeshi la Wananchi washirikiane kwa pamoja kutokomeza vikundi hivi kabla havijamea mizizi

Otherwise tutalia na kusaga meno.

BACK TANGANYIKA

Nasema hivi, kwa kuwa kabla ya mauuaji waharifu waliulizia/hoji ni sehemu hipi waharifu wanzao walipo fichwa na Polisi - hapo ndipo pa kuanzia - Polisi iwahoji kwa kina vijana ambao walitiwa mbaroni waseme nani kiongozi wao, nani anawapa mafunzo na kuwafadhili, je, lengo lao ni nini hasa, kumbuka wakati mwingine wanatumia silaha za moto, kuna mwana kijiji alisema sura za wengi wao si wenyeji wa pale kama hiyo nikweli wanatoka wapi?

Wasichukulie vitendo hivi kama ni uharifu wa kawaida, haiwezekani Polisi na jwtz wafanye operation ya kuwatokomeza alafu baada ya mwenzi mmoja wakahibuka tena, ujasiri huo wanaupata wapi i.e wanajiamini nini?

Majambazi gani yanaweza kuwa na ubavu wa kutaka kushindana na vyombo vyetu vya Dola, nani anawapa an inside information ya kujua wazalendo wanao wapa taarifa za kintelijinsia jeshi la Polisi alafu watoa taarifa wakajikuta wanageuziwa kibao na waharifu - there's something seriously wrong down the line in Tanga Region - securitywise, that is!
 
Nasema hivi, kwa kuwa kabla ya mauuaji waharifu waliulizia/hoji ni sehemu hipi waharifu wanzao walipo fichwa na Polisi - hapo ndipo pa kuanzia - Polisi iwahoji kwa kina vijana ambao walitiwa mbaroni waseme nani kiongozi wao, nani anawapa mafunzo na kuwafadhili, je, lengo lao ni nini hasa, kumbuka wakati mwingine wanatumia silaha za moto, kuna mwana kijiji alisema sura za wengi wao si wenyeji wa pale kama hiyo nikweli wanatoka wapi?

Wasichukulie vitendo hivi kama ni uharifu wa kawaida, haiwezekani Polisi na jwtz wafanye operation ya kuwatokomeza alafu baada ya mwenzi mmoja wakahibuka tena, ujasiri huo wanaupata wapi i.e wanajiamini nini?

Majambazi gani yanaweza kuwa na ubavu wa kutaka kushindana na vyombo vyetu vya Dola, nani anawapa an inside information ya kujua wazalendo wanao wapa taarifa za kintelijinsia jeshi la Polisi alafu watoa taarifa wakajikuta wanageuziwa kibao na waharifu - there's something seriously wrong down the line in Tanga Region - securitywise, that is!
Fact!
 
Mi nafikiri nguvu kubwa ingeelekezwa mahali hapo. Miezi kadhaa ya patrol na aerial surveillance yeyote aliyejificha hapo atatoka mwenyewe kwa njaa. Shida ni yawezekana bado tunaona ni mzaha
Uko sahihi mkuu. Hawa wahalifu watakuwa wanakaa huko huko kwenye mapango. Na inaelekea sababu ya kuondoka na mchele, sukari na biskuti baada ya kuwa wamewachinja hao wahanga ni kwa ajili ya kujikimu kwa muda mrefu wakiwa huko huko mapangoni.
 
Usishushie Jeshi la Polisi lawama zisizo za msingi wala ushahidi, askari wapo well trained hawawezi kufanya kitendo kama hicho tena kwa RAIA wema nachoona kutoka kwako ni chuki iliyo wazi kwa Jeshi, ni kwamba hao watu wame suspect tu kuwa kuna mtu kawa chongea kwa wanausalama.

Una point nzuri ya kudumisha uhusiano uliotukuka kati ya Jeshi na Raia wema ili kutokomeza uhalifu but the way una present UZI wako ni kama una widen the gap na kujaribu kuonyesha kuwa Jeshi halijui majukumu yake kitendo ambacho sio sahihi, vijana wanapambana usiku na mchana kudumisha amani ya nchi we upo kitandani unadondosha tu povu.

Maswala ya kiusalama unaandika ovyo utafikiri upo kwenye jukwaa la mapenzi, urafiki na uhusiano, hujui ulitendalo endelea kubwabwaja kwenye mitandao.

Fanya utafiti sio una kurupuka, nina wasiwasi JF imeingiliwa na mapopoma.
Povuuu linakuchomoka mkuu,tulia usipanic bro!waonee huruma hao waliondokewa na ndugu zao alafu ujitafakari na weledi wenu kwy kazi za ulinzi.Kwani nani alikuomba uchague kutulinda sisi?hata mm nafanya kazi ambayo unategemea sana wewe kuishi kwa hiyo kabla ya Kuanza kujifanya mjuaji sana tafakari,angalai kwa undani?kwa nn mauwaji kila kukicha?wapi mumepwaya?je mafunzo ni hafifu?qualification zenu je? Au tatizo ni rushwa? Suggest improvement plan sio povuu jingiii wkt watu wamepoteza ndugu yao na sio mara moja kwy hiyo sehemu.Jeshi la police linahitaji kufumuliwa na kuundwa upya,mambo yakuchukua form four failed hatututaki tena,si unaona jwtz walivyotulia kwanza wapewe hayo maeneo korofi walinde wao,nyie endeleeni kukaa barabarai muwasaidie tra kukusanya ushuru wa road linces nk,hope umenisoma.
 
si wote, na hao wachache wataondolewa soon!
Kesi za namna hii zipo nyingi sana. Na watu wameshajua polisi sio wasiri pindi wanapowapelekea ushahidi.

Ndio maana watu wanaona ni bora kujinyamazia kuliko kuja kufa kama hivi au kuja kutengwa na jamii.
 
Watu kadhaa wa kijiji cha Mikocheni karibu na Mapango ya Amboni mkoani Tanga wameuawa usiku wa kuamkia leo kwa kile kinachodaiwa kufichua vitendo vya uhalifu vya baadhi ya watu kijijini hapo.

================
Jana nilikuwa nasikiliza taarifa ya habari, sasa huko Kigoma wanakijiji wanalalamika kuwa kila watoapo taarifa kama watu wema, askari waendapo kuwakamata wahalifu usema ''Asingekuwa fulani sisi tusingejua kama una bunduki/silaha''

Kauli hizo zimesababisha matatizo ya uhasama na wanakijiji wamesema endapo polisi wataendelea kutoa siri za wafichua uovu basi hawatashirikiana nao.

Hapo nilishindwa kuelewa ufanyaji wa kazi wa hao polisi, hawajui huo upuuzi wao unaongeza uhasama kwa wanakijiji na kupelekea mauji na uhalifu usiokuwa na msingi.

Tukirudi Tanga, naona itakuwa vile vile tu (Kumradhi),

Ombi langu kwa polisi: Sisi Raia wema tunapotoa taarifa kama hizi za uhalifu lazima mjua tumechoshwa na vitendo hivyo, tunajua majambazi na wahalifu wengine wana mitandao mikubwa, mnapotoa utambulisho wetu mnatuweka kwenye mazingira ya hofu zaidi. Ni nyema mkafanya kazi kwa weledi mkubwa na sio kutafuta sifa.
Hili Suala Jeshi la Polisi na usalama kwa ujumla wabadilike.
Lipo kila sehem mpaka watu tunakosa imani na jeshi hili,Jeshi la Polisi aliondoka nalo Nyerere,ila kwa sasa naona kila mmoja badala ya kukimbilia polisi ndio kwanza anakimbia.
Wanafanya siku hizi watu wajilinde kwa kutumia Waganga wa Kienyeji,maana hakuna jinsi.
Hii ya kutajana ipo sana tena sana,na hii itawafanya hata hao pilisi wawe hatarini zaidi wao,maana mtu itakuwa akiona tukio au kuhisi anakaa kimya,sasa polisi wanakuja kustukia kwamba wao ndio wanabakia wametengwa na raia
Polisi mbadalike,
Mwanzo ilikuwa ni kwa wauza madawa ya kulevya,yaani ukimtaja ujue unafuata.Sasa hivi inakuwa kwa hawa wahalifu tena wengine hata mateja tu eti unataja mtu aliemtaja.
Mbaya sana hii
 
Mi nadhani hayo mapango yazibwe tu matobo yake yote yamwagwe zege la nguvu maana yanatugharimu zaidi.
Wazo lako zuri sana mkuu.

Wanyunyizie kwanza gesi ya sumu then wazibe matundu yote.
 
Kwa nn IGP aijiuzulu kwa kushindwa kusimamia usalama wa raia? Ndani ya mwezi mmoja si chini ya matukio manne (4). Nadhani ni uungwana kuachia ngazi na kupisha wengine wenye uwezo wa kusimamia usalama wa raia.
 
Back
Top Bottom