Mzanzibari haswa ni mtu aina gani?

Geza Ulole

JF-Expert Member
Oct 31, 2009
59,226
79,517
Wana JF,

Imefika wakati sasa kuanza kuhoji nani haswa ni Mzanzibari Asilia kihistoria maana tunakoenda sasa si huko na katika kujua haya inatupasa kupitia historia yetu hata kabla Waajemi na Waomani hawajatua Zanzibar yaani wakati huo visiwa hivi vikiwa na majina ya Kiasili ya kiafrika yaani Unguja n.k. na pia kipindi cha Wareno pia kipindi cha Wajerumani hadi Waingereza na pia siasa na utaifa wa Kizanzibari baada ya uhuru na mapinduzi ya Zanzibar

Tuanze na historia ya Unguja kabla ya mwarabu kuja; inasemekana kulikuwa na waafrika (ngozi nyeusi) wakiishi huko wengi wao walikuwa ni wale wavuvi wanaotoka pwani ya Tanganyika wakiienda huko kutokana na shughuli za uvuvi na hata baadhi yao kuwa na makazi yao huko na pwani pia; watu hawa walikuwa na dini za kiasilia wakifanya matambiko na yale yote yanayofanywa na wenzao wa Pwani yaani makabila ya Pwani kiutamaduni.

Haya yote yalianza kubadilika pale Mwarabu toka Oman alipotia nanga katika visiwa vile kwani utawala wa Asili haukuwa na nguvu ya kumzuia Mwarabu kufanya anachotaka maana alikuwa na silaha za kivita yaani bunduki iliyokuwa bora zaidi ya mkuki, mshale au sime. Kwa mantiki hiyo basi uhuru wa Mwafrika halisi ukapotea pale tu Mwarabu alipotia mguu katika visiwa vile. Mbali na hayo biashara haramu kama utumwa ilianzishwa na Mwarabu na pia biashara ya pembe za ndovu zilizomlazimisha kwenda hadi Ujiji kusaka vipusa hivyo. Kutokana na kushamiri kwa biashara hii ya utumwa na ndovu; visiwa hivi vilitamanisha watu wa mataifa mbalimbali haswa Mashariki ya Mbali hata kusababisha Sultan wa Oman kuamishia makazi yake. Na pia wale wa Magharibi kama Wareno, ambao nia na madhumuni yao yalikuwa kuhodhi biashara ile, matokeo yake mikanganyiko wa kujaribu kuhodhi dola ikawa ni jambo linalojirudia rudia katika jamii hii yenye mseto wa asili yaani Uarabu, Ubantu, Uajemi na Uhindi.

Japokuwa watu wa mataifa mbalimbali wamepita au wameweka maskani Zanzibar, Mwarabu mbali ya kufanya biashara alifanikiwa zaidi kusimika tamaduni zake katika visiwa vya Zanzibar kuliko mataifa yoote yaliyopata kuwapo ambayo yaliwekea uzito suala la biashara kuanzia Wareno na pia Wajerumani na Waingereza ikiwemo ya mali ghafi kwa wale wa nchi za Magharibi haswa kipindi cha Mapinduzi ya viwanda huko kwao!

Historia hii itaendelea.....
 
unajua majina ya ubin(surnames) ya wazanibar? mostly ni ya wabantu wa bara,wavuvi na makuli walioenda kukutana na ustaarabu wa kiarabu na kuchanganya damu
 
Mkuu nadhani swala hili linatoafsiriwa na WaZanzibar wenyewe maana hata ukiniuliza Mtanganyika ni nani itakuwa kazi kubwa!.. waache wenyewe wajitambulishe na watagombana wenyewe nani Mzanzibar na nani siye!
 
Wengi wao hawajui hata asili yao, kuna jamaa mmoja anajiita yeye ni mzanzibari nilifanya naye interview katika shirika fulani la Umma hapa Dar na kwa bahati nzuri wote tulipata kazi katika kuja form mbalimbali kuna form mija ilikuwa na sehemu ya kujaza kabila, jamaa hakujaza kwa kuwa hajui kabila lake na hajawahi kubother kutafuta, mpaka leo ile nafasi iko wazi haijajazwa kabila lake, He was very honest kwamba hajui kabila lake.
 
Ukiweza kumjua Mzanzibari bari itakuwa rahisi sana kumjua Mmarekani. Hili ni somo la kihistoria ambalo litakuchukua muongo zaidi ya mmoja kuweza kujua nani ni mzanzibari. Ni somo ambalo litakufanya usafiri kwenye pwani yote ya zanzibari ili uchukue historia na hutaishia hapo itakubidi uende lamu, oman, uajemi, uchina, ujapani, msumbiji, somalia na ureno ili ukatafute historia je hawa watu kutoka sehemu tofauti tofauti walio kuwa wanaenda zanzibar kufanya biashara waliwakuta waenyeji walikuwa ni kina nani? Maani tunaambiwa
When most of the Western world was still sunk in the darkness of the Middle Ages, Zanzibar was already a meeting place for traders from the great Oriental cultures – China, Persia and Arabia. It nestled in the middle of a mercantile civilisation, stretching from Somalia in the north down the coast of East Africa to Mozambique in the south. This kingdom and its inhabitants were known as the Swahili – the people of the coast.

They traded gold, ivory and cloth with visitors from across the Indian Ocean, built handsome stone houses and had well developed systems of government. Envoys, merchants and even pirates from as far away as Japan and Russia came to Zanzibar and its environs in sailing ships, blown across the seas by the northeast monsoon and returning, their holds laden with trade goods, on the southwest wind.

The first Europeans to ‘discover' Zanzibar were the Portuguese, who arrived in the late 15th century. In keeping with their conduct in the rest of their empire, they had little interest in the place beyond keeping it out of the hands of their enemies. They built a fort or two, introduced the sport of bullfighting to Pemba, and added a few choice words to the Swahili language. In fact, the Portuguese words still in use in Kiswahili give a fairly good impression of how the Portuguese spent their time here: Meza - table. Mvinyo - wine. Pesa - money.

Utaona kwenye maelezo ya hapo juu biashara zanzibar ilianza kufanyika kwenye karne ya 15 sijui wakati huo sisi huku kwetu tulikuwa tunafanya nini? kwenye karne ya 15 sijui miji kama dodoma, singida na shinyanga ilikuwaje?

Kikubwa hapa ni kuwa wazaznibar wana historia ndefu sana inambidi mtu alie somea historia afanye thesis ya historia ya zanzibar ili kuweza kumjua nani ni mzanzibari.
 
Wengi wao hawajui hata asili yao, kuna jamaa mmoja anajiita yeye ni mzanzibari nilifanya naye interview katika shirika fulani la Umma hapa Dar na kwa bahati nzuri wote tulipata kazi katika kuja form mbalimbali kuna form mija ilikuwa na sehemu ya kujaza kabila, jamaa hakujaza kwa kuwa hajui kabila lake na hajawahi kubother kutafuta, mpaka leo ile nafasi iko wazi haijajazwa kabila lake, He was very honest kwamba hajui kabila lake.

Shirika fulani la umma halipaswi kuuliza watu kabila zao wala dini zao! hizo details hazisaidii kwenye kuleta tija sehemu ya kazi. Kwa taarifa za mfanyakazi umri, mahali alipozaliwa, mwaka, majina yake, elimu yake na uraia wake ndio vyenye umuhimu.
 
Bila ya kutafuta makabatini, kwa kifupi Mzanzibari ni kila mzaliwa wa Zanzibar. Unaweza kuongeza vizazi viwili vitatu nyuma, kwa maana ya kuwa ikiwa babu na bibi yake mtu alzaliwa Zanzibar, inatosha kumfanya, kwa sifa ya uzawa wake, kuwa huyo ni Mzanzibari.

Kwa maneno mengine, kutokana na historia na jiografia ya Zanzibar, Wazanzibari ni mchanganyiko wa watu wenye asili tafauti (Watanganyika, Wakenya, Wakomoro, Wamakonde wa Msumbiji, Wahindi, Waajemi, Waarabu, Wachina...). Kuhusu hawa mwisho, kule Mkoani Pemba na Malindi Unguja, kuna Wachina wa zamani hata kabla ya kuja Waarabu; kwenye Msitu wa Ngezi/Kiuyu Pemba na Dole Unguja, kuna Wamakonde wa hata kabla ya Wareno. Makunduchi kuna Makumbaro (aina ya Wahindi) hata kabla ya Sultani; Kizimkazi kuna watu wenye asili ya Bagamoyo hata kabla kuja Mjerumani.

Hawa wanazuka leo na kusema asili ya Zanzibar ni Watanganyika au Waarabu, Waislamu au Wakristo, hiki ni kizazi cha watu muflis wa mawazo, kwani Zanzibar ina michanganyiko yote hiyo. Kwa hivyo, ama Zanzibar ni ya wote au si ya yeyote.
 
Wazanzibari wengi wao ni waarabu, hata wale weusi kama mimi wanajitambulisha kama "waarabu"


Nina rafiki yangu Mzenji sijui kama anaifahamu hii forum, ngoja nimtumie hii linki pengine atakuwa na mawili matatu.

Ila nadhani wazanzibari wanaji "nasibisha" zaidi na waarabu kuliko wabantu.

I stand to be corrected.
 
Wazanzibari wengi wao ni waarabu, hata wale weusi kama mimi wanajitambulisha kama "waarabu"


Nina rafiki yangu Mzenji sijui kama anaifahamu hii forum, ngoja nimtumie hii linki pengine atakuwa na mawili matatu.

Ila nadhani wazanzibari wanaji "nasibisha" zaidi na waarabu kuliko wabantu.

I stand to be corrected.
Kitu kimoja ni mtu "kujinasibisha" yeye mwenyewe, kwa utashi, maslahi, mapenzi yake; kitu chengine ni asili ya mtu.

Kunaweza kuwa na ukweli kuwa wengi wao wana asili ya Kiarabu kwa sababu wazee wao walitoka huko, au wana damu ya ya mchanganyiko na Waarabu kutokana na maingiliano ya ndoa. Lakini bado, kwa mtoto/mtu ambaye ana damu asili/damu ya Kiarabu, lakini hajui lugha wala utamduni (hapa naweka dini upande ili nisiingie katika makosa ya kuinasibisha dini ya Kiislamu na Uarabu - wapo Wachina Waislamu) wa Kiarabu, hawa wanaeweza kujinasibisha lakini hakuwafanyi wawe Waarabu per sey. Masikini hawa, hata huko wanakojinasibisha nako hawakujui, hawajawahi kufika, hawajulikani. Ni sawa na Mmakonde (au ethnic group yoyote) wa leo wa Zanzibar kujinasibisha na Msumbiji (au popote pale) wakati huko hawamjui wale yeye hakujui.

Na mimi pia ni mawazo yangu tu, niko tayari kufahamishwa kwa hoja.
 
Bila ya kutafuta makabatini, kwa kifupi Mzanzibari ni kila mzaliwa wa Zanzibar. Unaweza kuongeza vizazi viwili vitatu nyuma, kwa maana ya kuwa ikiwa babu na bibi yake mtu alzaliwa Zanzibar, inatosha kumfanya, kwa sifa ya uzawa wake, kuwa huyo ni Mzanzibari.

Kwa maneno mengine, kutokana na historia na jiografia ya Zanzibar, Wazanzibari ni mchanganyiko wa watu wenye asili tafauti (Watanganyika, Wakenya, Wakomoro, Wamakonde wa Msumbiji, Wahindi, Waajemi, Waarabu, Wachina...). Kuhusu hawa mwisho, kule Mkoani Pemba na Malindi Unguja, kuna Wachina wa zamani hata kabla ya kuja Waarabu; kwenye Msitu wa Ngezi/Kiuyu Pemba na Dole Unguja, kuna Wamakonde wa hata kabla ya Wareno. Makunduchi kuna Makumbaro (aina ya Wahindi) hata kabla ya Sultani; Kizimkazi kuna watu wenye asili ya Bagamoyo hata kabla kuja Mjerumani.

Hawa wanazuka leo na kusema asili ya Zanzibar ni Watanganyika au Waarabu, Waislamu au Wakristo, hiki ni kizazi cha watu muflis wa mawazo, kwani Zanzibar ina michanganyiko yote hiyo. Kwa hivyo, ama Zanzibar ni ya wote au si ya yeyote.

Umenena vema wazanzibari ni wale wazaliwa wa zanzibar bila kujali ametoka wapi
 
Wana JF,

Imefika wakati sasa kuanza kuhoji nani haswa ni Mzanzibari Asilia kihistoria maana tunakoenda sasa si huko na katika kujua haya inatupasa kupitia historia yetu hata kabla Waajemi na Waomani hawajatua Zanzibar yaani wakati huo visiwa hivi vikiwa na majina ya Kiasili ya kiafrika yaani Unguja n.k. na pia kipindi cha Wareno pia kipindi cha Wajerumani hadi Waingereza na pia siasa na utaifa wa Kizanzibari baada ya uhuru na mapinduzi ya Zanzibar

Tuanze na historia ya Unguja kabla ya mwarabu kuja; inasemekana kulikuwa na waafrika (ngozi nyeusi) wakiishi huko wengi wao walikuwa ni wale wavuvi wanaotoka pwani ya Tanganyika wakiienda huko kutokana na shughuli za uvuvi na hata baadhi yao kuwa na makazi yao huko na pwani pia; watu hawa walikuwa na dini za kiasilia wakifanya matambiko na yale yote yanayofanywa na wenzao wa Pwani yaani makabila ya Pwani kiutamaduni.

Haya yote yalianza kubadilika pale Mwarabu toka Oman alipotia nanga katika visiwa vile kwani utawala wa Asili haukuwa na nguvu ya kumzuia Mwarabu kufanya anachotaka maana alikuwa na silaha za kivita yaani bunduki iliyokuwa bora zaidi ya mkuki, mshale au sime. Kwa mantiki hiyo basi uhuru wa Mwafrika halisi ukapotea pale tu Mwarabu alipotia mguu katika visiwa vile. Mbali na hayo biashara haramu kama utumwa ilianzishwa na Mwarabu na pia biashara ya pembe za ndovu zilizomlazimisha kwenda hadi Ujiji kusaka vipusa hivyo

Historia hii itaendelea.....

mkuu,
ukiweza kujua mtanzania ni nani utaweza kujibu swali hili la mzanzibari.
 
Ni Mwanadamu aliye Mwenye rangi ya brown aliyetoka bara, alichukuliwa bara kama Mfanyakazi au Mtumishi au Mtumwa lakini akapendwa na Bwana yake (Kiongozi wa anayewatunza hao watumwa) na kuwabakisha na kuwapa haki kidogo baada ya Mfalme kupewa nchi na Waingereza alihakikisha wanafuata DINI yake ya KIISLAMU na pia kwasababu waarabu walikuwa wachache walitumia system inayoitwa ASSIMILADO - ni ya kofauti uwafanya waafrika wa huko kufikiri kama wao ni waafabu kiutamaduni , kimazingira, kula na hadi jinsi ya kuongea na hadi damu yao na ya kiarabu ni sawa tofauti ni rangi za miili yao kuwa tofauti lakini kila kitu ni sawa huko Zanzibar.

* ASSIMILADO System also inahakikisha unasahau ulikotoka kwahiyo watoto wako kama ulitoka bara hauwaambii historia yako; Wanaishia kutokuwa na makabila, saa nyingine kuwa na kabila inasaidia. Mila za makabila ni nzuri zinakujenga kuwa bora halafu baadaye ni dini zenu.
 
Ni Mwanadamu aliye Mwenye rangi ya brown aliyetoka bara, alichukuliwa bara kama Mfanyakazi au Mtumishi au Mtumwa lakini akapendwa na Bwana yake (Kiongozi wa anayewatunza hao watumwa) na kuwabakisha na kuwapa haki kidogo baada ya Mfalme kupewa nchi na Waingereza alihakikisha wanafuata DINI yake ya KIISLAMU na pia kwasababu waarabu walikuwa wachache walitumia system inayoitwa ASSIMILADO - ni ya kofauti uwafanya waafrika wa huko kufikiri kama wao ni waafabu kiutamaduni , kimazingira, kula na hadi jinsi ya kuongea na hadi damu yao na ya kiarabu ni sawa tofauti ni rangi za miili yao kuwa tofauti lakini kila kitu ni sawa huko Zanzibar.


[video]  http://www.mzalendo.net/habari/video...tu-wa-zanzibar[/video]
 
Back
Top Bottom