Mwenyekiti wa CCM Rufiji apigwa risasi na kufariki dunia

shida ya rufiji ni kuwa na idadi kubwa sana ya watu wanao miliki silaha kiholela,na wengi sn walikuwa wanajihusisha na ujangili wa meno ya tembo na mazao ya misitu ktk mapori ya selous vijiji km mkongo,mloka,kilimani,ruwe na delta ya rufiji.ss kudhibitiwa kwa ujangali na biashara ya magogo pamoja na kukamatwa kwa baadhi ya majangili naona wahanga wamegeuzwa viongozi wa chama na serikali wanaosimamia kwa dhati na pia labda waliotoa habari luganikisha vita ya ujangili.
Hapa umenena inawezekana kabisa au kuna wenzao walikamatwa au kuuliwa na wao wanaamua kulipiza kisasi police hawajaamua tu wangefanya msako usiku na mchana wangewakamata
 
Ujinga wa hao unaowashauri wanaenda kusimama barabarani na kuangalia kila mwenye ndevu na kisuruali kifupi wanakamata wanatesa nankuwaweka ndani.

Sasa jiulize mtu mwenye kanzu anaweza kuwa na stamina yakuendesha pkpk na kupiga risasi za kichwa? Wataenda na mihemko yakukamata watu hovyo wakitoa kisogo wanasikia chairman kapukuchuliwa macho.

Wakae na wananchi kwa urafiki kama unavyoshauri sio ubabe, na wengine wanaenda kwenye mikutano yao wanawasoma namba jua likizama vichwa kule


Mkuu jeshi la polisi linakosa mbinu kabisa, hivi mtu akiua anaweza kuzurura barabarani na pikipiki?
 
Tuendako siko, tusiingize itikadi za kichama hapa.Tuungane katika kutokomeza mauaji haya. Taabu inakuja pale chama fulani kinaona kinahaki kuliko wengine. Hivyo kupekea watu mwenye grievances za kuonewa kuamua kurespond kimya kimya. This is very dangerous to our country.
Ndo mujue na sisi hatujaribiwi .maana mikwara na kuua ndo munaita kasi ya ccm
 
Binafsi naona suala hili limechukua muda mrefu sana sana kupatiwa ufumbuzi!! Summary excution of some Govt officials and Ruling Party leaders siyo jambo la kupuuzia hata kidogo,sikumbuki katika historia ya Taifa letu tangu tupate Uhuru kama tumewahi kupitia mambo hatarishi kama haya, save Vita ya Kagera!

Ukijaribu ku-analyse kwa umakini matukio haya ya kutisha/kusikitisha, actually yanaonekana kama ni masuala ya kisiasa zaidi kuliko ujambazi/ugaidi, Wizara ya mambo ya ndani na TISS wajaribu kukaa chini na wenyeji/wakazi wa kanda ya Pwani wawasikilize wana maoni/ushauri/malalamiko gani, tumieni lugha ya kidiplomasia kujua undani wa tatizo hili, mkienda kwa vitisho hamtapata ushirikiano kutoka kwa wenyeji.

Kumbukeni wanao fanya vitendo hivi viovu bila shaka wanaishi kwenye Kaya za wenyeji na watakuwa wanajulikana - si rahisi watu ambao si wenyeji wa sehemu hizo waweze kuwapiga risasi Govt Officials na Polisi alafu wawambie raia wachukue mkaa kutoka kwenye ghara/store, yaani waharifu mpaka wanapata muda wa kufanya dialogue na raia nini la kufanya i.e wanashauri raia wachukue mkaa!! - hii imekaa vipi? Hivi sasa inaonekana as days goesby trend ya uharifu huu unaendelea with impunity!! Who knows kama uharifu huu utakuwa contained na kuishia ndani ya Coastal belt tu au watatokea ma copycats. Natoa ushauri tu kama raia.
 
Jeshi la polisi lijizatiti kwenye ulinzi badala ya kuhangaika na kina Ney na Lisu na vikesi vya uchochezi...ni vikesi vya kipuuzi
 
sio kiusalama tu, hata kijiografia mkoa wa Pwani unatakiwa ugawanywe. Hii inaweza kusaidia kupunguza matukio ya namna hii. RIP mwenyekiti.
 
Unaacha kuzungumzia mada husika unaleta ushamba wa kisiasa, tangu umeanza kumtaja huyo bashite umefanikiwa nini? umemtoa madarakani au? Mauaji ya Rufiji na bashite wako huyo wapi na wapi?

Mkulu alishasema ASIPANGIWE
Nawe usimpangie mtu cha kuandika.
Vumilia tu kwani Bashite akitajwa wewe inakuuma nini?
 
Kwani uongo, tendeni haki kwa Bashite jamii ijue laasivyo raia wataendelea kutoa hukumu wenyewe
IMG_20170331_141036.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom