Mwandishi wa habari joseph ngilisho anaswa na takukuru

ngurdoto

Member
Aug 19, 2010
58
23
Wadau, nawasilisha kwenu; Jana mchana Januari 29, 2013 anayejiita mwandishi wa habari Joseph Ngilisho wa magazeti takribani yote ya UDAKU, ZANZIBAR LEO, DIRA YA MTANZANIA, SEMA USIKIKE, REDIO WAPO, REDIO SUNRISE N.K ambazo amekuwa akiziandikia kwa kutishia watu hatimaye amekamatwa na PCB kwa kuomba RUSHWA ya Sh. Milioni 2.

Hivi karibuni Ngilisho aliandika habari DIRA YA MTANZANIA akidai jengo la Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha linavuja kama mti wa muembe, kuta za kumbi mbalimbali zimechanika vibaya. Hata hivyo kabla ya hapo tayari alishaomba apewe Sh. Milioni 2 ili asiandike habari hizo.

Sasa jana ameweka mtego akanaswa hata hivyo alipojaribu kijinusuru na mikono ya DOLA alijikuta akikimbia na kutumbukia tena kwenye mikono ya DOLA yaani Ofisi za Usalama wa Taifa.

Hivi sasa amesomewa mashitaka yake na anatakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao ni wafanyakazi wa Serikali.

Nawasilisha.
 
Hawo ndiyo dizaini ya waandishi wa habari makanjanja wanaoivunjia tasnia ya habari heshima. Naomba sheria ichukue mkondo wake.
 
Wadau, nawasilisha kwenu; Jana mchana Januari 29, 2013 anayejiita mwandishi wa habari Joseph Ngilisho wa magazeti takribani yote ya UDAKU, ZANZIBAR LEO, DIRA YA MTANZANIA, SEMA USIKIKE, REDIO WAPO, REDIO SUNRISE N.K ambazo amekuwa akiziandikia kwa kutishia watu hatimaye amekamatwa na PCB kwa kuomba RUSHWA ya Sh. Milioni 2.

Hivi karibuni Ngilisho aliandika habari DIRA YA MTANZANIA akidai jengo la Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha linavuja kama mti wa muembe, kuta za kumbi mbalimbali zimechanika vibaya. Hata hivyo kabla ya hapo tayari alishaomba apewe Sh. Milioni 2 ili asiandike habari hizo.

Sasa jana ameweka mtego akanaswa hata hivyo alipojaribu kijinusuru na mikono ya DOLA alijikuta akikimbia na kutumbukia tena kwenye mikono ya DOLA yaani Ofisi za Usalama wa Taifa.

Hivi sasa amesomewa mashitaka yake na anatakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao ni wafanyakazi wa Serikali.

Nawasilisha.

hapo kwenye nyekundu sijakupata vizuri ...

sasa mbona hiyo taarifa haijaandikwa kwenye magazeti kama anavyoandika za wenzake??
 
Wadau Ipad inasumbua ushamba; Ni kwamba huyu jamaa alikamatwa jana Januari 28, Mwaka huu mchana maeneo ya Hotel ya African Tulip jirani na ofisi za Barclays Bank alipoanza kufuatiliwa ndio akala mbio akiwa na Milioni 2 mfukoni, sasa alipoonza PCB wanazidi kumfuata akaona mbele kuna geti la nyumba ipo wazi kumbe ilikuwa ni Ofisi za USALAMA WA TAIFA akaingia ndani na kuzitupa M 2 humo humo ndani. Jamaa walipofika wakamnasa kama kuku wa kisasa.

Amepandishwa kizimbani leo Januari 29, mchana kama ni habari ina maana zitaanza kutolewa kesho na waandishi wenzake kama watamuandika mimi nilichokiona na kukisikia mahakamani ndio hicho. Nawasilisha
 
Huyu ndio mwandishi Joseph Ngilisho wa magazeti ya udaku, Zanzibar Leo, Sema Usikike,Dira ya Mtanzania na mengine mengi. Jana alikamatwa kwa kuomba rushwa ya Sh. Milioni 2 pale EAC. Leo Januari 29 amepandishwa kizimbani kusomewa mashitaka yake.Mbali na tuhuma hizo mwandishi huyo alikuwa anatumia kalamu yake kuwatishia waandishi wa habari wanawake kwamba wasipokuwa tayari kufanya nao tendo la ndoa angeandika habari zao ikiwa ni pamoja na kutengenezea mitego ili waingie kwenye majanga, na pindi wanapoona hali ngumu basi wampatie chakula cha usiku MWANDISHI GWIJI WA RUSHWA ARUSHA-NGILISHO.jpg
 
Nyie shitukeni,ulisha wahi kuona takukuru ikakamata mtoa rushwa? Hawa wamemtafutia mtego maana hua anawachana live na ndie alie ipa heshima na mashabiki weng sanreys radio iliopo arusha kwani kunakipindi cha saa mbili usiku hua ni moto sana hua anaichana selikali sana.jiulize yule mbunge walio mkamata iliishia wapi? Takukuru hawafai wao ndio wala rushwa wakubwa eti walimkamata sikumoja mchina kua ametoa rushwa ya laki tano! Hivi ndani ya nch hii hakuna watu wanao kula rushwa ya milioni zaid ya mia? Yaani takukuru?siikubali hata
 
Yule mwandishi wa habari mashuhuri sana humu jamvin A.K.A Mzee wa vibahasha ameipata hii maneno kweli?
 
Wadau Ipad inasumbua ushamba; Ni kwamba huyu jamaa alikamatwa jana Januari 28, Mwaka huu mchana maeneo ya Hotel ya African Tulip jirani na ofisi za Barclays Bank alipoanza kufuatiliwa ndio akala mbio akiwa na Milioni 2 mfukoni, sasa alipoonza PCB wanazidi kumfuata akaona mbele kuna geti la nyumba ipo wazi kumbe ilikuwa ni Ofisi za USALAMA WA TAIFA akaingia ndani na kuzitupa M 2 humo humo ndani. Jamaa walipofika wakamnasa kama kuku wa kisasa.

Amepandishwa kizimbani leo Januari 29, mchana kama ni habari ina maana zitaanza kutolewa kesho na waandishi wenzake kama watamuandika mimi nilichokiona na kukisikia mahakamani ndio hicho. Nawasilisha

asante kwa kutupa ufafanuzi vizuri
 
Wadau Ipad inasumbua ushamba; Ni kwamba huyu jamaa alikamatwa jana Januari 28, Mwaka huu mchana maeneo ya Hotel ya African Tulip jirani na ofisi za Barclays Bank alipoanza kufuatiliwa ndio akala mbio akiwa na Milioni 2 mfukoni, sasa alipoonza PCB wanazidi kumfuata akaona mbele kuna geti la nyumba ipo wazi kumbe ilikuwa ni Ofisi za USALAMA WA TAIFA akaingia ndani na kuzitupa M 2 humo humo ndani. Jamaa walipofika wakamnasa kama kuku wa kisasa.

Amepandishwa kizimbani leo Januari 29, mchana kama ni habari ina maana zitaanza kutolewa kesho na waandishi wenzake kama watamuandika mimi nilichokiona na kukisikia mahakamani ndio hicho. Nawasilisha

hiyo fani yao imeshakuwa kimeo sana, siku nilipoishusha hadhi kabisa ni siku nilipojua Ngilisho ni mhandishi, pweeeh, kuna mkutano nilihudhuria Naura Spring hawa waandishi walitia aibu mpaka basi, Ngilisho akiwa mmoja wao., pole zake.
 
mahakama ifanye kazi yake, ngoja nikafatilie hilo jengo la EAC yanayovuja na gharama za ujenzi wa jengo hilo lililozinduliwa na JK.
 
Nina wasiwasi na huyu mleta mada, inawezekana kweli kachukua mlungula, au ni issue ya kutengenezewa kama ile ya JERRY MURO.
 
Hawo ndiyo dizaini ya waandishi wa habari makanjanja wanaoivunjia tasnia ya habari heshima. Naomba sheria ichukue mkondo wake.

Wale wengine waliokamatwa kule Monduli kesi yao imeishia wapi? Nadhani Pasco ataelewa hatima ya wale waliokamatwa kule Monduli wanaomba mshiko kwani alijitambulisha kwa maandishi yake kuwa alikuwa anawafahamu!!
 
Ni kweli kabisa huyu jamaa kanaswa na taarifa zilizotufikia hivi punde ni kwamba amekosa wadhamini wawili wafanyakazi wa serikali hivyo amepelekwa mahabusu ya kisongo ( aka kurusha ndege), hadi hapo atakapokamilisha taratibu za dhamana.
 

Attachments

  • 168969_106646229413733_5941634_n.jpg
    168969_106646229413733_5941634_n.jpg
    6.9 KB · Views: 413
Kama ang'ekuwa hajafichua maovu ya Serekali zaifu hiyo rushwa hata kama ang'ekuwa ameenda kuichukulia pale kwenye ofisi za Takukuru wasing'emkamata.
 
Back
Top Bottom