Mwanamke niliyezaa nae ananipa majukumu yasiyonihusu

Redpanther

JF-Expert Member
Feb 23, 2019
2,813
3,769
Habari za wakati huu wapendwa na wanajamvi wenzangu wa MMU. Poleni kwa kazi na kwa wale walioenda kusali hongereni kwa ibada.
Nianze mkasa wangu juu ya huyu Baby mama wangu, Hapa juzi kati (wiki iliyopita) mwanadada aliyedai kuwa anaujauzito wangu na kunikabidhi kulea, alijifungua salama na Mtoto wa Kiume Mungu akajalia.

Anaishi kwao na mimi naishi kwangu, mwanzo alitaka aje akae nami tulee mimba pamoja nilikataa kwa sababu zangu binafsi. So ikabidi akae kwao tu, sasa tangu amejifungua nimekuwa nikituma pesa kwa ajili ya mahitaji ya msingi kwaajili ya mtoto na mama mtoto ukizingatia mtoto bado anategemea kila kitu kutoka kwa mama yake.

Kuna baadhi ya mahitaji ananitajia kimsingi mimi nayaona kama sio sahihi mimi kuhudumia kwa maana mahusiano mimi na yeye yaliisha na mimi nikawa nime move on na yeye akawa ame move mwanzoni kabisa mwa ujauzito. Sasa wakati kuna majukumu mengine naona kama napewa mzigo usio wangu, kwa mfano ananiambia nimlipie kodi ya nyumba akaishi kwake, ikiharibika simu hela ya matengenezo anapiga simu kwangu na niliwahi mpatia mara moja akatengeneza ila naona kama anazidi kuleta mazoea anataka nimpatie mtaji au nimfungulie biashara ili asinisumbue ishu ya matumizi ya mtoto , nilikataa nikamwambia nitatoa hela ya matumizi kila mwisho wa mwezi ila sio kukufungulia biashara.

Tokea hapo, ikitokea amepiga simu na nikawa sijapokea labda ikawa iko mbali au sikusikia anatuma mimeseji ya ajabu... Mara naona unakatika mauno juu ya huyo malaya wako ila simu ya mwanamke anayekulelea mwanao hupokei” sikujibu lolote ni nyingi tu mara unatumia pesa na malaya wako ila hela ya mtoto hutoi.! Pesa natoa ila yeye anaiingiza kwenye matumizi yake binafsi so namimi nakaza.

Sasa nimekuja kwenu, wanaume wenzangu ambao tunaohudumia hawa akina mama mnafanyaje ili kufanya hili suala la malezi kuwa rahisi na kupunguza mivutano na huyu mwana mama (Baby mama)

Naomba kuwasilisha, naombeni michango yenu wakuu
 
Habari za wakati huu wapendwa na wanajamvi wenzangu wa MMU. Poleni kwa kazi na kwa wale walioenda kusali hongereni kwa ibada.
Nianze mkasa wangu juu ya huyu Baby mama wangu, Hapa juzi kati (wiki i....
Kipi rahisi sasa kama unaona anakupa mizigo isiyokua yako ambayo ni shelter yake unaonaje akupe mzigo unaokuhusu ambao ni mtoto upambane nao?

Sasa kama hutaki kumlipia chumba mtoto atalala wapi?? Afya ya mama ni muhimu kwa usalama wa mtoto. Utategemeaje nyanya iliyoiva na kupendeza vizuri kwa mche ambao huumwagilii na kupulizia dawa.

Haijalishi ulishamuve on au lah as long as anamwanao huna ujanja hapo mmeunganisha bond ya maisha. Labda kama una dukuduku kua si mwanao..

Be a man.. Be responsible on your duties and act accordingly.
Utafanya wanaume wengine wazidi kuonekana mabwege

SORRY
 
Kipi rahisi sasa kama unaona anakupa mizigo isiyokua yako ambayo ni shelter yake unaonaje akupe mzigo unaokuhusu ambao ni mtoto upambane nao??

Sasa kama hutaki kumlipia chumba mtoto atalala wapi?? Afya ya mama ni muhimu kwa usalama wa mtoto. Utategemeaje nyanya iliyoiva na kupendeza vizuri kwa mche ambao huumwagilii na kupulizia dawa.
Haijalishi ulishamuve on au lah as long as anamwanao huna ujanja hapo mmeunganisha bond ya maisha. Labda kama una dukuduku kua si mwanao..

Be a man.. Be responsible on your duties and act accordingly.
Utafanya wanaume wengine wazidi kuonekana mabwege

SORRY
Done
 
Kipi rahisi sasa kama unaona anakupa mizigo isiyokua yako ambayo ni shelter yake unaonaje akupe mzigo unaokuhusu ambao ni mtoto upambane nao??

Sasa kama hutaki kumlipia chumba mtoto atalala wapi?? Afya ya mama ni muhimu kwa usalama wa mtoto. Utategemeaje nyanya iliyoiva na kupendeza vizuri kwa mche ambao huumwagilii na kupulizia dawa.
Haijalishi ulishamuve on au lah as long as anamwanao huna ujanja hapo mmeunganisha bond ya maisha. Labda kama una dukuduku kua si mwanao..

Be a man.. Be responsible on your duties and act accordingly.
Utafanya wanaume wengine wazidi kuonekana mabwege

SORRY

Sawa nimesoma maandishi yako, itoshe kusema ahsantee kwa kutoa muda wako kunipa ushauri.
 
Kipi rahisi sasa kama unaona anakupa mizigo isiyokua yako ambayo ni shelter yake unaonaje akupe mzigo unaokuhusu ambao ni mtoto upambane nao??

Sasa kama hutaki kumlipia chumba mtoto atalala wapi?? Afya ya mama ni muhimu kwa usalama wa mtoto. Utategemeaje nyanya iliyoiva na kupendeza vizuri kwa mche ambao huumwagilii na kupulizia dawa.
Haijalishi ulishamuve on au lah as long as anamwanao huna ujanja hapo mmeunganisha bond ya maisha. Labda kama una dukuduku kua si mwanao..

Be a man.. Be responsible on your duties and act accordingly.
Utafanya wanaume wengine wazidi kuonekana mabwege

SORRY
Full stop kubwa. Uzi umefungwa hamna mtu ku comment. Mada ushaimaliza mkuu.
 
Kipi rahisi sasa kama unaona anakupa mizigo isiyokua yako ambayo ni shelter yake unaonaje akupe mzigo unaokuhusu ambao ni mtoto upambane nao??

Sasa kama hutaki kumlipia chumba mtoto atalala wapi?? Afya ya mama ni muhimu kwa usalama wa mtoto. Utategemeaje nyanya iliyoiva na kupendeza vizuri kwa mche ambao huumwagilii na kupulizia dawa.
Haijalishi ulishamuve on au lah as long as anamwanao huna ujanja hapo mmeunganisha bond ya maisha. Labda kama una dukuduku kua si mwanao..

Be a man.. Be responsible on your duties and act accordingly.
Utafanya wanaume wengine wazidi kuonekana mabwege

SORRY
Kindly receive my hugs
I wouldnt say any better. Zaid nikiongezea nitaongea maneno mabaya.
 
Full stop kubwa. Uzi umefungwa hamna mtu ku comment. Mada ushaimaliza mkuu.

Naona unapigilia msumari..! Ila kusema ukweli nahudumia ila biashara na Kumangishia itafanyika kama kuna huo ulazima. Anakaa kwao alfu yeye anajipiga kifua kwenda kupanga so mie nifanye nini.! Mmh
 
Kipi rahisi sasa kama unaona anakupa mizigo isiyokua yako ambayo ni shelter yake unaonaje akupe mzigo unaokuhusu ambao ni mtoto upambane nao??

Sasa kama hutaki kumlipia chumba mtoto atalala wapi?? Afya ya mama ni muhimu kwa usalama wa mtoto. Utategemeaje nyanya iliyoiva na kupendeza vizuri kwa mche ambao huumwagilii na kupulizia dawa.
Haijalishi ulishamuve on au lah as long as anamwanao huna ujanja hapo mmeunganisha bond ya maisha. Labda kama una dukuduku kua si mwanao..

Be a man.. Be responsible on your duties and act accordingly.
Utafanya wanaume wengine wazidi kuonekana mabwege

SORRY
Na wote tuseme Amen
 
Matunzo ya mtoto maana yake ni matunzo ya Mama yake in term of food,shelter pamoja na nguo.

1.Mama anahitaji chakula ili aweze kumnyonyesha mtoto.

2.Mama anahitaji nyumba ya kuishi ili mtoto asidhurike na baridi au mvua,mbu,wanyama wakali wa usiku,e.t.c.Kuishi kwa wazazi wake ni ngumu sana kwa sababu kuna mambo ya kunyanyapaliwa na kunyanyaswa kwa sababu ya kuzalia nyumbani.

3.Mama anahitaji nguo kwa sababu hawezi kumlea mtoto akiwa uchi.Imagine Mama anampelekaje mtoto clinic akiwa uchi!.Yaani mtoto kavaa nguo lakini Mama yake yuko uchi!

Kwa hiyo mahitaji yote anayokuambia umpe ni mahitaji sahihi kabisa wala siyo mahitaji hewa.Cha msingi mpe mtaji ili kukwepa mizigo zaidi.
 
polee kwanza kwa hilo unajua tunapitia mateso kwel
Hivi usha jihakikishia kua hiyo ni damu yako!?
tuanzie hapo kwanza

Sijahakikisha..! Na hilo ndio linanifanya niwe nasita hata kuhudumia. Kwa sababu kwa akili yangu na toho yangu, siwezi kamwe kulea mtoto wa mwanaume mwingine. Sema sijapata fursa ya kumuona huyo mtoto maana sasa hivi tunaishi mikoa tofauti tofauti na ni Mbali haswa.
 
Matunzo ya mtoto maana yake ni matunzo ya Mama yake in term of food,shelter pamoja na nguo.

1.Mama anahitaji chakula ili aweze kumnyonyesha mtoto.

2.Mama anahitaji nyumba ya kuishi ili mtoto asidhurike na baridi au mvua,mbu,wanyama wakali wa usiku,e.t.c

3.Mama anahitaji nguo kwa sababu hawezi kulea mtoto akiwa uchi.Imagine Mama anampelekaje mtoto clinic akiwa uchi!.Yaani mtoto kavaa nguo lakini Mama yake yuko uchi!

Kwa hiyo mahitaji yote anayokuambia umpe ni mahitaji sahihi wala siyo mahitaji hewa.Cha msingi mpe mtaji ili kukwepa mizigo zaidi.

Daaah ... sipigi kavu kavu tena. Hii mambo ni kama una mke wa pili kudadeki. Anyway Ahsantee kwa mawazo yako na yote ni ya msingi. Nitafanyia kazi Ahsantee sana tena
 
Back
Top Bottom