Mwanamke Afungwa Jela ya Wanaume Kwa Miezi Sita

Mar 6, 2010
74
0
Mwanamke Afungwa Jela ya Wanaume Kwa Miezi Sita
4262810.jpg

Tuesday, March 23, 2010 3:15 AM
Skendo limeikumba kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini ambapo mwanamke aliyakamatwa kwa makosa ya ujambazi anadaiwa kufungwa kwenye jela ya wanaume kwa kipindi cha miezi sita na kupelekea mwanamke huyo abakwe na kulawitiwa na wafungwa wa kiume.Denise Wilson au maarufu kwa jina la Abbah wa mji wa Isipingo nchini Afrika Kusini amekifungulia mashtaka kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini kwa kumweka kwenye jela ya wanaume kwa miezi sita wakati alipokuwa akisubiria kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ujambazi, kujaribu kuua na kuteka watu.

Denise anadai fidia ya rand 100,000 kwa madhila aliyoyapata wakati alipokuwa kwenye jela ya wanaume.

Katika nyaraka za mahakama, Denise alisema kuwa alikamatwa septemba 24 mwaka 2002 na kupelekwa kwenye jela ya wanaume.

Alisema kuwa kitendo chake cha kupinga kuwekwa jela moja na wanaume kilisababisha avuliwe nguo mbele ya wanaume huku akizomewa na kuchekwa.

Wakati wa kipindi chake cha miezi sita kwenye jela ya wanaume, Denise anadai kuwa walinzi wa jela walikuwa wakimlazimisha afanye matendo ya ngono bila ya idhini yake.

Alidai pia kuwa wafungwa wa kiume walikuwa wakimpapasa mara kwa mara kwenye sehemu zake za siri bila ya idhini yake.

Denise pia hakusita kusema kuwa alibakwa na kulawitiwa katika kipindi cha miezi sita kwenye jela ya wanaume.

Alisema kuwa ingawa maafisa wa jela walikuwa wakijua kuwa yeye ni mwanamke, waliendelea kumweka jela moja pamoja na wanaume.

Alisema kuwa hata daktari wa wilaya alipomfanyia uchunguzi wa kuthibitisha jinsia yake, aliendelea kuwekwa kwenye jela hiyo.

Kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini kimeamua kukaa kimya kikisubiria kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani.
 
hawakumtendea haki....unyama mkubwa sana huo
...amekifungulia mashtaka kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini kwa kumweka kwenye jela ya wanaume kwa miezi sita wakati alipokuwa akisubiria kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ujambazi, kujaribu kuua na kuteka watu.

...huwezi jua bana, labda naye ni 'semenya' mwingine, na hasa hayo makosa yake yenye muelekeo wa matendo ya kiume.
BTW, kitengo ni kwa ajili ya kurekebisha tabia, inaonekana 'lengo' limetimia.
 
Itakuwa ana mushkeri ndio maana wakashindwaa wamuweke wapi!!hata daktari alichemsha hahaha duniani kuna mambooo!!
 
Lakini ni lazima tuelewe kuwa yule bado ni binaadamu kama sisi na ana haki, waliomuweka jela ya pamoja na wanaume wataambulia walichokuwa wanakitaka, lakini humu JF nawaombeni jamani tusimuone kakosea saaaaana kwa vitendo vyake hatujui yaliyokuwa yanamsibu jamani, plz MBU, MAJOR MKANDALA please jamani ubinaadamu kwanza!
 
Mwanamke Afungwa Jela ya Wanaume Kwa Miezi Sita
4262810.jpg

Tuesday, March 23, 2010 3:15 AM
Skendo limeikumba kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini ambapo mwanamke aliyakamatwa kwa makosa ya ujambazi anadaiwa kufungwa kwenye jela ya wanaume kwa kipindi cha miezi sita na kupelekea mwanamke huyo abakwe na kulawitiwa na wafungwa wa kiume.Denise Wilson au maarufu kwa jina la Abbah wa mji wa Isipingo nchini Afrika Kusini amekifungulia mashtaka kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini kwa kumweka kwenye jela ya wanaume kwa miezi sita wakati alipokuwa akisubiria kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ujambazi, kujaribu kuua na kuteka watu.

Denise anadai fidia ya rand 100,000 kwa madhila aliyoyapata wakati alipokuwa kwenye jela ya wanaume.

Katika nyaraka za mahakama, Denise alisema kuwa alikamatwa septemba 24 mwaka 2002 na kupelekwa kwenye jela ya wanaume.

Alisema kuwa kitendo chake cha kupinga kuwekwa jela moja na wanaume kilisababisha avuliwe nguo mbele ya wanaume huku akizomewa na kuchekwa.

Wakati wa kipindi chake cha miezi sita kwenye jela ya wanaume, Denise anadai kuwa walinzi wa jela walikuwa wakimlazimisha afanye matendo ya ngono bila ya idhini yake.

Alidai pia kuwa wafungwa wa kiume walikuwa wakimpapasa mara kwa mara kwenye sehemu zake za siri bila ya idhini yake.

Denise pia hakusita kusema kuwa alibakwa na kulawitiwa katika kipindi cha miezi sita kwenye jela ya wanaume.

Alisema kuwa ingawa maafisa wa jela walikuwa wakijua kuwa yeye ni mwanamke, waliendelea kumweka jela moja pamoja na wanaume.

Alisema kuwa hata daktari wa wilaya alipomfanyia uchunguzi wa kuthibitisha jinsia yake, aliendelea kuwekwa kwenye jela hiyo.

Kitengo cha kurekebisha tabia cha Afrika Kusini kimeamua kukaa kimya kikisubiria kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani.
Kuna baadhi ya binadamu huwahukumu wenzao kuwa wana hatia hata kabla
ya mahakama kufanya hivyo.nina imani atapata haki yake
 
alipokuwa akisubiria kufikishwa mahakamani kwa makosa ya ujambazi, kujaribu kuua na kuteka watu.
Lakini ni lazima tuelewe kuwa yule bado ni binaadamu kama sisi na ana haki, waliomuweka jela ya pamoja na wanaume wataambulia walichokuwa wanakitaka, lakini humu JF nawaombeni jamani tusimuone kakosea saaaaana kwa vitendo vyake hatujui yaliyokuwa yanamsibu jamani, plz MBU, MAJOR MKANDALA please jamani ubinaadamu kwanza!

:eek: ???
...am speechless na hizi tafsiri za "Human Rights!" ungeniambia ni mtuhumiwa i.e Innocent until proven Guilty, kidogo ningekuelewa!
 
Hata kama alitenda kosa gani hakutakiwa kuwekwa jela moja na wanaume!! Haki za binadamu zichukue mkondo wake na asilimia mia moja hiyo kesi atashinda. Kila mtu ahukumiwe kwa kosa lake, after all she is innocent until proves otherwise!!! Huyo Bwana jela ajiandae!!!
 
Kweli hii si haki. Waliofanya kitendo hiki wanapaswa kuwajibika. Everybody's rights should always be respected.
 
Ukifanya kazi ya kiume lazima uchangamane na NYAMAUME sioni tatizo la yeye kuwekwa kundi moja na hao aliowekwa nao kwani hata akiwa uraiani anchangamana nao kazini. Huku ndiko kurekebisha tabia; sidhani kama atarudia tena ubaradhuli wake
 
Back
Top Bottom