Mwambusi, Yanga ni timu kubwa, kula kwenye VIHOTEL UCHWARA kunakupunguzia heshima yako

Mimi ni Mwanasimba mwenye matarajio ya kuongoza timu , wala sina kolabo yoyote na Yanga , lakini nimesononeka sana kwa huyu shujaa wa timu yenu kumuona mara nyingi akila uswahilini , kama shida ni hela basi alipwe malimbikizo yake , hawa makocha wa yanga na simba wanavumilia mengi sana ambayo wewe huyajui .
Hahahaha...simba makini mpo?
 
Hivi simba mmelipa malimbikizo ya mishahara ya wachezaji ya miezi minne mliyokuwa mnadaiwa?

Vipi lile deni la Msoti, au mpo tayari kushuka Daraja....mtukoseshe point sita zetu.?
 
Ujumbe huu ametumiwa Mwambusi. Ni juu yake mwenyewe (kama ni mwana-JF) kuamua kumjibu au kutomjibu mwanzisha mada. Na ni juu yake kupima ushauri aliyopewa hapo utampofikia (kupitia kwa wana-JF ikiwa yeye siye) na kuchukua hatua mwafaka kwake. Mengine yote ni kuendeleza mjadala usiotuhusu.
 
Nimekuona si mara moja ukipata lunch kwenye kihoteli cha wasomali mtaa wa kongo , kariakoo .

Hiki kihoteli kisichokuwa hata na feni achilia mbali a/c si sawa kwa hadhi yako , hakuna haja ya wewe kocha msaidizi wa Yanga afrika kwenda kubanana na wamachinga kwenye foleni ya wali nyama wa 3500 /, pondamali atakupoteza , mbona yeye hali kwa wasomali ?

Ingekuwa simba tusingeshangaa lakini yanga mbona shida hizo hakuna ? Jiangalie mkuu na ikiwezekana jirekebishe .

.....Itaendelea ikibidi .

Bolded hapo ndio ujumbe uliokusudia, sasa wenyewe wanakuja
 
Hivi simba mmelipa malimbikizo ya mishahara ya wachezaji ya miezi minne mliyokuwa mnadaiwa?

Vipi lile deni la Msoti, au mpo tayari kushuka Daraja....mtukoseshe point sita zetu.?
Aulizwe Hanspope .
 
Sometimes vya kuandika huwa vinaisha nafikiri.Sadly watu wanataka waandike tu hata kama hawana cha kuandika.Ndo unajikuta unaandika hata kocha wa yanga amekula wapi
 
Umefuatilia mafanikio yake weee umeona cha ku mkosoa huna

Umeamua kuongelea anapo kula

Duuh!!
 
Sometimes vya kuandika huwa vinaisha nafikiri.Sadly watu wanataka waandike tu hata kama hawana cha kuandika.Ndo unajikuta unaandika hata kocha wa yanga amekula wapi
Lengo ni kuwakumbusha viongozi wa yanga umuhimu wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wake .
 
Umefuatilia mafanikio yake weee umeona cha ku mkosoa huna

Umeamua kuongelea anapo kula

Duuh!!
Hivi ukisikia Mwambusi amewekwa karantini Tandale kwenye kambi ya kipindupindu utajisikiaje ? Kinga ni bora kuliko tiba .
 
Nilikuwa duka fulani la mpemba maeneo ya Bunju, Dar es Salaam.

Ghafla nikaona basi la Simba SC likisimama na wakashuka wachezaji wakaja dukani kununua Maji ya Kandoro.

Mmoja aliamua kununua maji 6, kaweka kwenye mfuko wa rambo.
Bunju utakuwa umewafananisha uwanja wa Simba haujanza kutumika, ungesema Yanga angalau maana kuna kipindi waliweka kambi yao Bagamoyo.
 
Huyu mleta mada ndio wale wanaokula lunch pale samaki samaki samora then usiku anaenda kulala kwake maji matitu..
Hata hivyo wapo wanaolala huko Mikoche B, Masaki, Mbezi beach, kwenye mazingira magumu sana. Kula mtu anaweza kula popote pale, Mwambusi kula hapo sioni ubaya wake, kulala ndipo penye matatizo ndio maana watu wanafanya kazi Dar usiku wanaenda kulala kwa Moro.
 
Unataka aishi maisha unayotaka wewe wakati yeye sio wewe? Ukubwa wa Yanga rangi ya njano na kijani au uwanja au kuifunga Simba na Azam au kubebwa kwao?
 
Eti yanga ni timu kubwa!Timu ambayo haijawahi kufika hata nusu fainali ya mashindano yoyote ya afrika..ingekuwa samba iliyofika nusu fainali klabu bingwa afrika na fainali kombe la wawakilishi ungesemaje?
 
Tatizo la watanzania tunapenda kuwalazimisha icon wetu waendelee kuishi maisha duni yasiyoendana na hadhi yao ili tu watufurahishe,ukweli ni kuwa baada ya muda mfupi tunawadharau,tunawaona ni wakawaida mwishowe tunawapotezea,ukishakuwa icon jaribu kulinda hadhi ili heshima iwepo,hata kina Ronaldo wamezaliwa na kukulia kwenye maisha ya kimaskini sana lakini hiyo haimaanishi sasa kila wakati ndo ashindie kwenye vijiwe vya masela na kugongeana fegi.TZ ethic za kazi bado sana wengi tunaishi kwa kuogopa maneno ya masela.
 
Back
Top Bottom