Mwalimu Nyerere Foundation ipo?

Mzawa Halisi

JF-Expert Member
Feb 25, 2009
637
361
Miaka michache kabla ya kifo cha Nyerere, ilianzishwa taasisi iliyoitwa Mwalimu Nyerere Foundation (MNF), taasisi hii iliendelea hata baada ya kifo cha mwalimu ikiwa chini ya uenyekiti wa Salim Ahmed Salim, na mtendaji mkuu Joseph Butiku. Kwa taarifa ambazo nimeshindwa kuzithibitsha, ni kuwa taasisi hii iko chali kiuendashaji hata ilishindwa kulipa wafanyakazi wake mishahara. Na kwa kiasi kikubwa kuanguka kwa taasisi hii kumechangiwa na uzembe na kiburi cha uongozi wa juu ukiongozwa na Bw. Butiku. Inasemekana kuwa wahisani ikiwa ni pamoja na GOT waliokuwa wanaisaidia taasisi hii walishindwa kuendelea kutoa misaada baada ya viongozi wa MNF kuanza kutumia misaada hiyo nje ya malengo yaliyokusudiwa.

Kama kuna member ana taarifa za uhakika juu ya majaaliwa ya taasisi hii naomba anifahamishe.
 
Mheshiwa Mzawa Halisi,

Majibu ya swali lako ni kwamba Mwalimu Nyerere Foundation ingalipo; bali kutokana na uongozi wake, hususan Salim Ahmed Salim na Joseph Butiku, kuwa wakweli, calling a spade a spade, GOT inasita kutekeleza ahadi zake za ruzuku. Uongozi wa MNF ni wazalendo wa kweli, jasiri na waadilifu, na hawawezi ku-adopt mbinu za kifisadi ili kuendeleza taasisi inayomuenzi Muasisi wa Taifa letu. Hata Muasisi mwenyewe angekuwa hai, angepinga ufisadi unaolenga kukipatia mapato chombo hicho.

Ni matarajio ya wale wanaopenda maendeleo thabiti ya nchi yetu kwamba, punde si punde, mabadiliko ya kweli yaletwa na Watanzania wa kizazi kipya, wakifuata nyayo za Salim na Butiku, ili taasisi hii ya kihistoria kwa taifa isiendelee kulegalega.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Last edited:
MNF ipo na inaendeshwa kama taasisi nyingine sizizo za kiserikali. Kwa kawaida wanakuwa na wafanyakazi kunapokuwa na miradi inayoendelea na kila inapokamilika wale wote waliokuwa wakifanyi project hiyo huondoka.

Miradi yao ya hivi karibuni ni usuluhishi wa 'MUAFAKA' wa Zanzibar, hapo nyuma walishughalika sana na harakati za kupatanisha waRundi.
 
Juzi juzi wamesaini mktaba wa ujenzi wa jengo refu Dar, nadhjani litakuwa ndicho kitegauchumi chao
 
Mambo mengi MNF yanakwama kwa sababu ya Mkurugenzi wao. Alitakiwa astaafu toka mwaka jana au mwaka juzi lkini bado kang'ang'ania tu kile kiti. Ni kweli hawana pesa hata za kulipa wafanyakazi.
 
Paul Kagame na Museveni wameahidi kuhakikisha kuwa Nyerere Foundation inasalimika. Butiku is over 70 and he should not be an issue. And so is Salim. Kunatafutwa uongozi mpya utakaoweza kuendeleza pale Butiku na Salim walipofikia. Jengo la Foundation likimalizika litakuwa mradi mzuri wa kuiendesha Foundation sustainably.
 
Paul Kagame na Museveni wameahidi kuhakikisha kuwa Nyerere Foundation inasalimika. Butiku is over 70 and he should not be an issue. And so is Salim. Kunatafutwa uongozi mpya utakaoweza kuendeleza pale Butiku na Salim walipofikia. Jengo la Foundation likimalizika litakuwa mradi mzuri wa kuiendesha Foundation sustainably.
Hivi ahadi ya Rwanda na Uganda zilitekelezwa?
 
Hiyo MNF imegoma kukipigia magoti kikundi cha utekaji ndani ya ccm kilichojivika koti la uzalendo. Taasisi hiyi imegundua kikundi hicho cha utekaji kinatumia nafasi za wadau wake kuhujumu yoyote anayewakosoa, kikundi hicho kimefikia mahali kinahakikisha mgombea yoyote wa ccm anatangazwa mshindi bila kujali idadi ndogo ya wapiga kura. Taasisi imeamua kujiweka mbali na hujuma za hicho kikundi.
 
Ninachojua ni kwamba MNF ipo na wala haina matatizo na Mtu yoyote na tena kama kuna Mtu ambaye anaibeba na kuiheshimu hiyo Taasisi ni Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli na Serikali yake ya Tanzania tofauti na Watu wengi ambavyo mmedhani kuwa ' Wametengwa ' na Utawala wa Awamu hii ya Gwala / Tano.

Wafadhili wakubwa wa MNF ni Serikali ya Tanzania, Uganda, Rwanda na China na hilo Jengo lao jpya likikamilika basi hiyo Taasisi itaweza kuwa na ' Miradi ' yake mingi tu na itajiendesha vyema ila bila kutoka nje ya dhumuni ' Mama ' la Taasisi ambalo ni ' Kuyaenzi ' yale mema yote ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na ' Fikra ' zake zilizotukuka kwa Bara zima la Afrika.

Kuna Mchangiaji mmoja hapo juu nadhani labda ni kwa ' Kukurupuka ' tu au kwa ' Upopoma ' wake amesema kuwa Mzee Joseph Butiku ni nani na sijui hana faida ndani ya MNF. Ni vyema Watu wengine kabla ya ' Kuzuka ' tu humu Kimaelezo basi muwe pia kidogo mnapitiapitia hata ' Historia ' tu za Watu ili mkiwa mnakuja Kuchangia humu angalau muwe na a,b,c's.

Kama kuna Mtu aliyekuwa wa karibu na pengine ndiyo ' Msiri ' wa mambo mengi wa Hayati Baba wa Taifa kwa Kipindi Kirefu bali alikuwa ni Mzee Joseph Butiku. Achilia mbali ' Undugu ' wake wa damu na Baba wa Taifa ila Mzee Butiku aliaminiwa sana na Mwalimu na ndiyo maana hata ' Majukumu ' mengi ya Kifamilia ( ya Mwalimu aliachiwa Yeye ) na mpaka leo hii mnaona hiyo MNF imefikia hapo ilipo basi ni 90% juhudi zake Binafsi Mzee Butiku akishirikiana na Wazee wengine wawili ( Kimaadili na kwa nafasi zao Nyeti walizokuwa nazo ndani ya nchi hii sitoweza Kuwataja hapa kwa sasa )

Kwa ' Hulka ' yetu Watanzania iliyojaa Wivu / Husuda na Kupenda ' Majungu ' ningeshangaa kutokusikia kwamba Mzee Joseph Butiku hahusishwi na ' Upigaji / Ufujaji ' hapo MNF. Na bahati mbaya wengi wetu hata hatujui ' Structure ' nzima ya Uongozi wa MNF na pengine kwanini hadi hivi leo Mzee Butiku bado yupo hapo. Bado nasisitiza tuwe tunajikita Kwanza katika Kufuatilia Jambo husika / fulani kabla ya Kuja Kuzoza / Kupayuka hovyo hapa Jamvini.

Kuhusu suala la Wafanyakazi wake kutokupata Mishahara ya miezi kadhaa sina uhakika nalo na nitakuwa pia wa mwisho kuliamini hilo ila hata kama ikiwa hivyo bado pia MNF haitokuwa Taasisi ya Kwanza nchini Tanzania Wafanyakazi wake kucheleweshewa ' Mishahara ' na najua zipo zingine nyingi tu na Kubwa ambazo zina aina hii ya tatizo. Na hakuna mahala ambapo pameandikwa kwamba Mkurugenzi wa MNF akifikisha miaka 70 basi anatakiwa ' ang'atuke ' hapo.

Mwisho kabisa tujifunze Kuwaheshimu hawa Wazee ambao Kwanza wameitumikia hii nchi kwa uwezo wao wote wa Kizalendo huku wengi wao hata ' wakihatarisha ' maisha yao kwa faida ya Tanzania lakini pia ndiyo Watu ambao walikuwa ' very loyal ' kwa Hayati Baba wa Taifa na pengine hivi sasa ilipashwa hata tuwe tunawatengenezea ' Majukwaa ' ya Kifikra ili waweze kutupa ' Madini ' yao lakini pia waweze kutupa zaidi mitizamo chanya ya Hayati Baba wa Taifa Nyerere kuliko hivi sasa tunavyoanza ' Kuwadhihaki ' kwa sababu tu ya ama Kutumika au kwa Chuki zetu.

Yangu ni hayo tu na kila la kheri nyote.

Cc: MzalendoHalisi , Companero , Mzawa Halisi , Zanaki
 
Back
Top Bottom