Muswada wa marekebisho ya sheria ya manunuzi ya umma 2011

Siku nikiona Kikwete yuko ndani ya gari mtumba sawa niwakubalie waruhusu. Lakini hivi kapanda BMW mpya alafu sie tupande used? I seeeeeeeee????
 
sipati picha ndege ya mtumba ikitikisika angani,nafikiri itakuwa nchi ya kwanza kunnua mitumba,chini ya jk tutaona mengi
 
Ni hatari sana, tunawaomba wabunge mnao tuwakilisha wananchi wenu kweli mlikatae hili kwa nguvu zote. Kama sijakosea nia hii ya kubadili sheria ya manunuzi kwa serikali ilishika kasi wakati ambapo wadau fulani walitaka serikali inunue mitambo ya dowans kwa kigezo kuwa kuagiza mitambo mipya ya kuzalisha umeme kuna chukua muda mrefu! Hapa ndipo tunapo hitaji mawazo yenye kuvu kupinga sana hili. Nakumbuka mh Mbowe alikwisha toa kauli juu ya mpango huu wa serikali kabla haujaletwa bungeni, Mbowe alipinga vikali mpango huu wa serikali kubadili sheria ya manunuzi kwa nia ya kuruhusu mitumba kununuliwa. Nisahihishwe kama siko sawa. Mtazamo wangu ni kuwa mswada huu ni hatari kwa taifa, kwani taifa linaweza kuingia ktk manunuzi ya bidhaa/vifaa ambavyo haviwezi kutumika ktk kazi za uzalishaji kwa muda mrefu, bali kila wakati vinaweza kuitaji matengenezo na vipuri ambavyo vyaweza kosekana kwasababu teknolojia inaweza kuwa imepitwa na wakati. Taifa hili litajengwa na wananchi wote wenye moyo na uzalendo wa kweli kwa taifa.
 
Angalizo kuhusu mgongano wa kimslahi kama ulishanunua au kutumia vitu used anza kwa declaration.
Mie natumia gari la mtumba nadhani nimepoteza sifa ya kuchangia lakini vyama na wabunge pia wamebobea katika mitumba sasa kukataza serikali huku mnanunua itakuwa unafiki.
Hatuna viwanda vya mitambo na magari kung'ang'ania upya na uwezo mdogo ni kujiua na tai zenu shingoni
 
Angalizo kuhusu mgongano wa kimslahi kama ulishanunua au kutumia vitu used anza kwa declaration.
Mie natumia gari la mtumba nadhani nimepoteza sifa ya kuchangia lakini vyama na wabunge pia wamebobea katika mitumba sasa kukataza serikali huku mnanunua itakuwa unafiki.
Hatuna viwanda vya mitambo na magari kung'ang'ania upya na uwezo mdogo ni kujiua na tai zenu shingoni
Watanzania mnalo maana sasa hivi waingereza wamekaza uzi kwetu chagua moja kuwa shoga au nunua vitu chakavu ccm mnalo hapo mtanasa kotekote maana china wanatudai uingereza wanataka tuwe mashoga wao watuoe kipi bora
 
Angalizo kuhusu mgongano wa kimslahi kama ulishanunua au kutumia vitu used anza kwa declaration.
Mie natumia gari la mtumba nadhani nimepoteza sifa ya kuchangia lakini vyama na wabunge pia wamebobea katika mitumba sasa kukataza serikali huku mnanunua itakuwa unafiki.
Hatuna viwanda vya mitambo na magari kung'ang'ania upya na uwezo mdogo ni kujiua na tai zenu shingoni


Huu ujinga si wako tu, bali hata wabunge walio changia wa magamba walikuwa wanaunga mkono hoja ya mswada huu wakisema wamenunua magari ya mtumba. Sasa nikulize wewe na hao wapumbavu wengine gari ni lako au ni la watanzania wote. Viongozi wa ccm na serikali yao ni janga la kitaifa bila kuondoka hamna maendeleo nchi hii.
 
Huu ujinga si wako tu, bali hata wabunge walio changia wa magamba walikuwa wanaunga mkono hoja ya mswada huu wakisema wamenunua magari ya mtumba. Sasa nikulize wewe na hao wapumbavu wengine gari ni lako au ni la watanzania wote. Viongozi wa ccm na serikali yao ni janga la kitaifa bila kuondoka hamna maendeleo nchi hii.

Nyie watoto wa siku hizi hamtaki kabisa mawazo tofauti na yenu na ya mabwana zenu ndio maana cameroun anataka muozwe kabisa hadharani. Hatuwezi kuwa na mawazo sawa lazima tujadiliane hapa JF ndio pake.

We gari la serikali ukaite lako omba lift kama watakubeba!
 
Katika muswaada wa manunuzi ya umma serikali imependekeza kununuliwa vitu vilivyo tumika, serikali imetaja maeneo ya kununua vitu chakavu kuwa ni meli, ndege, vichwa vya treni na mabehewa yake. Cha kujiuliza katika kipindi hiki serikali inapo jipanga kufufua shirika la ndege na reli kwa nini izungumzie kununua ndege au vichwa vya treni vilivyo tumika, je sio kuwa viongozi wetu ambao wengi ni mafisadi wanatengeneza mazingira ya kuibia serikali kitapeli kwa kupitia kupitisha mswaada huu wa manunuzi?

Tukumbuke pia wakati wa kampeni rais alitoa ahadi za kununua meli sehemu mbalimbali sasa isije kuwa wajanja walio serikalini wanataka kutumia mwanya huu wakishirikiana na mafisadi wenzao wafanyabiashara kuibia serikali? Kubwa zaidi kutokana na mapendekezo ya mswada, ufisadi huu wa manunuzi utalihusisha baraza la mawaziri katika kutoa kibali cha manununuzi ya vyombo hivi vilivyo tumika. Wana jf hebu jaribuni kutoa maoni yenu katika hili.
naungana na wewe ila kitu kimoja ondoa usemi huu kusema kuibia serikali ,sema watatuibia ....watu wengi (sio wewe) huwa hawaelewi pesa inayoumika ni kodi tunazolipa direct au indirect kama kununua soda sukari chumvi majani chai nk
 
naungana na wewe ila kitu kimoja ondoa usemi huu kusema kuibia serikali ,sema watatuibia ....watu wengi (sio wewe) huwa hawaelewi pesa inayoumika ni kodi tunazolipa direct au indirect kama kununua soda sukari chumvi majani chai nk

Kwa Kweli Kama Huu Muswada Ukipita!! Hii itakuwa Ni taifa la Kwanza Duniani Kuwa na Utaratibu wa Kuokota Jalalani!! Mimi Kwa Uelewa Mdogo Huwa naJua Vitu Vingi ambavyo Vinatengenezwa Kwa Nchi za Magharibi, kama ni imara sana Huwa wanatoa Dhamana (Garantee) ya Miaka Kumi!! Kama Magari ya Scania na Benzi!! Sasa Kwa wale Tunaonunua Nje ya dhamana ndio Kama unavyoona Ajali zinavyoongezeka!! Mfano Mzuri ni kwa malori ya Mizigo, Kila uchwao ni ajali!! Yanauwa watu wasio na Hatia, Kama ukipita Mitaa ya wami kila siku ni ajali za Malori!! Ukichunguza kwa Undani ni Uchakavu wa Malori Husika!! Je Kama serekali ni Nani anataka Kutuloga!! Huu Muswada una Lengo Gani? Mimi ninavyojua kwa Mikataba ya Kimataifa katika Kukopa kama world Bank Huwa Hawapendelei sana Kununua Vitu Chakavu!! Sasa sisi Kama Watanzania tunataka kutumia hela zetu za Ndani Kununua Vitu Chakavu!! Yu Wapi Mustapha Nyang'anyi? Alitumwa Kununua Pantoni akaamua Kuchukua Chake Mapema na Kununua Pantoni Chakavu!! Je Ili weza Kufanya Kazi kwa Muda Gani? Si Kama Mwaka Mmoja Tu? Sasa Unafuu gani tulipata!! JAMANI HATA KAMA NCHI INA DHIKI ILA WABUNGE KWA UMOJA WENU TUWE WAZALENDO NA TUSEME HUU MUSWADA HAPANA!! HATA TULIO NJE TUTAWASUPPORT KWA KUSEMA ANGALAU MMEITENDEA HAKI TANZANIA!! NAWASILISHA KWA UCHUNGU!!!
 
Kufuatia sakata inayoendelea mjengoni kuanzia jana dhidi ya wabunge wa upinzani na wa chama "twawala" hoja ikiwa ni sheria ya manunuzi ya mali za umma, kwmb serikali iruhusiwe kununua vifaa used. Hapa jf naona mko kimya nini kauli zenu ktk hili? Kwenu GREAT THINKERS
 
Magamba wengi bungeni,wameambiwa wawabeze wapinzani na kutetea hoja ipite kwa ku2danganya.
 
Tumeona Muswada wa mabadiliko ya sheria ya manunuzi ya Umma ukipelekwa bungeni, tumeona na kusikia baadhi ya wabunge wakisema tuangalie, tuwape nafasi serikali, hatuna uwezo, tununue kile tunachoweza.

Wabunge wengine wakasema tuwe makini na vyombo chakavu!!

Anyway.........to cut the story short; Anayetaka sheria ya manunuzi iruhusu manunuzi ya vifaa chakavu (vyenye unafuu) ni nani? Wabunge wamesema serikali inawezakupata ndege zenye hali nzuri kabisa ''used'' au meli ''used''

Sasa hili lilikuwa ni lengo la CCM au ni baada ya Jakaya kutoa ahadi za ''ki-wendawazimu''???
Utawezaje kununua Meli tatu, kujenga viwanja cha kimataifa kule Misenyi.........kitahitaji ndege angalao moja itakayotua pale, hata kama sio ya kimataifa.....Ayway, anaweza kuyafanya haya bila kununua MELI CAHAVU NA NDEGE CHAKAVU??

Kuna dhamira ya kweli hapa??? binafsi sikubaliani na huu muswada lakini pia, nina mashaka na dhmira yake in the first place.
 
Nimekuwa nikitafakari juu ya huu muswada wa serekali wa kupendekeza utungwaji wa sheria mpya ya manunuzi ambayo itaifanyia marekebisho sheria ya manunuzi ya mwaka 2004 ili kuiwezesha serikali kununua vitu vilivyotumika (used).

Nimeona wabunge wengi wanaoiunga mkono katika huu muswada wamekuwa wakitoa mfano wa mitambo ya dowans ambayo sasa ni ya symbion! Na wengi wamejitolea mfano wao wenyewe(wabunge) kwa kununua magari used. Baadhi ya mawaziri nao wamejitosa kuutetea muswada huo, tena wengine kwa jazba na hamaki, lakini sijamsikia yeyote akisema ni nchi gani kuna sheria ya ununuzi wa vitu ''used'' kama tunayotaka kufanya hapa kwetu na manufaa yaliyopatikana kwa sheria hiyo.

Ninachojiuliza hapa ni kitu kimoja tu, kwamba serikali yetu imekuwa na kawaida ya kujitetea katika masuala ya kisera,kisheria na mikataba mbalimbali kwa msemo maarufu wa ''best practice''. Sasa najiuliza katika hii sheria ya manunuzi ya vitu ''used'' mbona serikali haisemi ni ''best practice'' ya wapi? Nawasilisha wadau.
 
Ndugu yangu we acha tu tena ukiwa kwenye field ya ugavi na ununuzi ndio utalia kabisa sababu kinachofanyika ni kuandaa shavu zaidi kwa wanasiasa na influence zao kupitia kwa "ACCOUNTING OFFICER (CEO)"
Kwamba kuwaongezea mamlaka zaidi, umezungumzia best practice tu ila hata "benchmarking" hamna hapo mkuu,
Pia kuna kitu kinaitwa GPSA, ambapo kwenye mkutano wa mwisho wa PMU Managers wa idara za umma ambao uliandaliwa na PPRA pale AICC Arusha mwaka jana walipinga uwepo wa hyo taasisi kwa uanzishwaji wake ulikuwa wa kukurupuka ambapo haikushirikisha wadau wa manunuzi.
Matokeo yake kwenye huu muswada hyo GPSA ndio inasimikwa utukufu, kitu ambacho ni kuongeza ukiritimba katika idara ya manunuzi na kuficha taalumu za wataalamu wa manispaa na halmashauri zetu.
Muswada umeandaliwa kwa matakwa binafsi na ya muda mfupi kwa wanasiasa ila haujazitangatia kwa mapana mahitaji ya "ugavi na ununuzi" kama taaluma mahsusi yenye kuokoa pesa za umma na thamani ya pesa hizo.
 
Ndugu yangu we acha tu tena ukiwa kwenye field ya ugavi na ununuzi ndio utalia kabisa sababu kinachofanyika ni kuandaa shavu zaidi kwa wanasiasa na influence zao kupitia kwa "ACCOUNTING OFFICER (CEO)"
Kwamba kuwaongezea mamlaka zaidi, umezungumzia best practice tu ila hata "benchmarking" hamna hapo mkuu,
Pia kuna kitu kinaitwa GPSA, ambapo kwenye mkutano wa mwisho wa PMU Managers wa idara za umma ambao uliandaliwa na PPRA pale AICC Arusha mwaka jana walipinga uwepo wa hyo taasisi kwa uanzishwaji wake ulikuwa wa kukurupuka ambapo haikushirikisha wadau wa manunuzi.
Matokeo yake kwenye huu muswada hyo GPSA ndio inasimikwa utukufu, kitu ambacho ni kuongeza ukiritimba katika idara ya manunuzi na kuficha taalumu za wataalamu wa manispaa na halmashauri zetu.
Muswada umeandaliwa kwa matakwa binafsi na ya muda mfupi kwa wanasiasa ila haujazitangatia kwa mapana mahitaji ya "ugavi na ununuzi" kama taaluma mahsusi yenye kuokoa pesa za umma na thamani ya pesa hizo.

Je unazungumziaje tabia za watumishi wengi katika manunuzi kutokuwa waadilifu. Tatizo ni nini? Bila 10% kazi hazifanyiki!
 
Back
Top Bottom