Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Wakizungumzia maajabu hayo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Tatwe, Kata ya Mirare ambaye jina lake hakutaka liandikwe gazetini alisema mtoto huyo alizaliwa na mama aliyejulikana kwa jina moja la Zena Juni 2, mwaka huu usiku na alijifungulia katika mji wa mzee Wabeya.
Sisi tulishangazwa kuona mtoto amezaliwa akiwa na matumbo nje akiwa hai ambapo watu wengi baada ya kupata habari hiyo tulijikusanya akiwamo mwenyekiti wa kijiji cha Tatwe na mchungaji mmoja, kilisema chanzo hicho.
Gazeti hili lilifanya juhudi kumpata mama mzazi wa mtoto huyo wa ajabu, Zena Ibrahimu [19] wa Kijiji cha Burere alikiri kujifungua mtoto huyo na kuongeza kuwa wakati akilea mimba hiyo alikuwa akihudhuria kliniki kama kawaida lakini wataalamu wa afya hawakumueleza kama angejifungua mtoto wa jinsi hiyo.
Mzazi huyo alisema kuwa, tukio hilo limehusishwa na imani za kishirikina ambazo haziamini na kudai zimekuwa zikimpa hofu.<a class="timestamp-link" href="http://kaparama.blogspot.com/2010/06/mtoto-azaliwa-utumbo-nje-mkoani-mara.html" rel="bookmark" title="permanent link"><abbr class="published" title="2010-06-30T01:15:00+04:00"></abbr> http://www.blogger.com/email-post.g?blogID=7263400288518859103&postID=3504405921470474006
:A S cry::A S cry: