Mungu kuwapa Gold na Dimonds watanzania, zimekuwa Ungodly and demons kwao

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674
Kwa hakika tuombe Mungu Watanzania wasijue sana kuhusu madini na maliasili zao, kwa kuwa wakijua sana kuhusu hayo Madini na Migodi yao yenye Dhahabu na Alimas [MUNGU ALIZOWAPA GOLD AND DIAMONDS] ambayo VIONGOZI WAO wameigeuza imekuwa ushetani [UNGODLY AND DEMONS TO THEM]. Si vyema wakaujua ukweli manake wakiujua watakuwa wa kwanza kwa risasi za Zao ama za Watawala wao kuingia kwenye chemba za Mioyo yao.

Kutoka GOLD AND DIAMONDS mpaka UNGODLY AND DEMONS,aikuwa dhamira ya Mungu.Mungu aliwapenda awapatia MADINI na MALIASILI NYINGI SANA,kisha akawapatia MALIASILI WATU KAMA NYERERE,lakini leo uwezi amini kuwa mara baada ya muasisi huyo kufa ambae ndie alikua Mlinzi Number MOJA WA TAIFA HILI, dhidi ya maliasili na madini kila kitu kwishneyyyy kana kama kesho ndio mwisho wa Taifa la Watanzania.

Aliziitunza MALI ZIYO kwa misingi kuwa Watu wa TAIFA lake bado awajawa na maarifa ya kutosha juu ya kuzitumia maliasili hizi Mungualizowapa WAJA WAKE.Huwa nifikia hapo alafu unakutana na mpumbavu ambae aueni angekuwa mjinga anaepandikiza ujinga dhidi ya Baba wa TAIFA,uwa naoana wakatii mwingine inaweza kuwa tuna laana.

Kama yule Mzee angesema madini hayo ayachimbe enzi zake hakika TANZANIA MNAYOIONA LEO [TANZANIA YA MUUNGANO WA BARA NA VISIWANI] hakika tusingekuwa nayo na nina hakika MANYANGAU wangekuwa WAMESHAINGIZA KWENYE MATATIZO KAMA CONGO YA SASA ZAIRE YA MOBUTU. Lakini Mwalimu kwa kwa kujua hatuna maarifa alichofanya nikutujenga kwenye UMOJA NA KUSOMESHA VIJANA ILI BAADAE WAONGOZE WATOTO WAO JUU YA KUCHIMBA MALI YAO NA IWALETEE FAIDA WAO NA KIZAZI CHAO.

Naambiwa Kuna Mgodi Mama wa MIGODI YOTE TANZANIA,MGODI WA ALMASI WA MWADUI,Mwalimu aliukuta mgodi huo unamilkiwa kwa asilimia 100 na wakoloni lakini Mwalimu alipigana nao mpaka Serikali ikafikisha asilimia 50.Kulikua na Wazungu walioujenga Mgodi huo kama wako kwao Ulaya. Wazungu hao wapatao zaidi ya miatano [500] Mwalimu,alifanya maarifa yake kama kiongozi mwafrika mwenye nia watu wake wamilki mgodi aliwapandishia kodi kwenye mishahara yake,wazungu wote waliondoka.Ingawa ilikuwa siri enzi hizo wanasema Mwalimu alipandisha kodi mtu akienda kuchukua mshahara kodi hilooo!!!!!! wao wenyewe kwa hiari yao wakaondoka Mwalimu akaweka Wabongo kuendesha mgodi huo.

Mpaka Mwalimu anaondoka Madalakani Mgodi huo Serikali ilikua inamilki asilimia kubwa zaidi ya kampuni ya kigeni DE-BEERS [SOUTH AFRICA]

Mwalimu alivyowapa tu mgongo mamaaa!!!!!!!! kama walikuwa wanasubili wamsaliti hata kabla hajafa Mzee wa Watu.Mgodi wa Mwadui Hisa za Serikali zilishushwa wakapewa Wazungu ikafikia asilimia 25 ikabaki kidogo sana iwe ziro .Nafikili baadhi ya watu kwa kumuogopa Mungu wakaona Wasikufuru.

Kwa mgodi kama huo pekee ambao una historia ya aina yake,ambayo uwezi kuamini kuna ViIONGOZI WETU WA KITAIFA UKITAJIWA MAJINA YAO WENGI WAKIWA VIJANA WAMEPATA KUFANYA KAZI HUMO MIAKA YA SITINI na SABINI.Kwa hiyo kama ni swala la kujua FAIDA ya Migodi basi wanajua toka wakiwa vijana wadogo.Wengine viongozi wamesoma ndani ya shule zilizokuwa zinzmilikiwa na mgodi huo kama SHULE YA SEKONDARI YA SHINYANGA [SHY-BUSH]. Lakini naambiwa walivyougalagaza mgodi huo muhimu sana kwenye historia ya Migodi Tanzania uwezi kuamini,wameruhusu Wazungu kufanya UPROOTING kwenye Mgodi huo na sio tena uliokuwa mgodi bora kabisa dunia na katika historia ya Migodi BORA dunianio huo ulikuwa ni sehemu ya dunia ilipoonyeshwa umhimu wa Dunia kuwa na migodi bora na yenye faida kwa jamii husika.

Kwa waliopata kuishi kwenye Mgodi huo wanasema Mgodi huo ulikuwa na Mazingira na ujenzi wenye sura ya ULAYA ndani ya Tanzania. Wenyeji walikuwa wanaita CANADA NDANI YA TANZANIA] kutokana na kuwa Mwasisi wake alikuwa ni raia toka Nchi ya CANADA, DK Williamson.Ambae aliupenda mgodi wake huo,uliompa jeuri mpaka kiasi cha kumuarika Malkia wa Uingereza akiwa binti kuja kuona,alipokuja huku enzi hizo Tanganyika,ilikuwa kuwa alipotoka Tanganyika kwenda Nairobi ili aludi kwao akiwa nairobi ajaondoka akapewa taarifa ya msiba,mdio kufika kwao kuukwaa na UMALKIA.Na kituko cha DK Williamson ni kuomba kumuoa Mama huyo kwa kuwa alikuwa na UTAJIRI WA MGODI HUO.

Lakini jeuri ya Waingereza wakamwabia thubutu hata kama UNAMKWANJA MLEFU BADO HAPO NI ROYAL FAMILY hivyo huna nafasi ya kuoa hapa.Akaishia kumpa zawadi ya almas kubwa kupata kutokea katika HISTORIA YA DUNIA.

Kama ingekuwa ni Kujifunza jinsi gani tungeinvest kwenye migodi basi mgodi huo ni sehemu mama ya Viongozi wetu kuwa wamejifunza ni jinsi gani migodi yetu yapaswa kujiendesha.Tanzania ina wataalamu wazuri wa madini ambao ni lulu sana kwa wawekezaji, lakini kwa kuwa wansiasa wamenunuliwa na kutufikisha huko kwenye UNGODLY AND DEMONS wasomi hawa wamekuwa nao WATUMWA ILI WAWEZE KULISHA FAMILIA ZAO. Japo wapo wazelendo lakini wengi wao wenye ufahamu mzuri wa sekta ya Madini walipigwa chini na kamwe hawana sauti ya maamuzi,na wengine walishakufa kwa kiihoro kwa jinsi UPROOTING ILIVYOFANYIKA kwenye hifadhi ya Madini yetu.

Leo Mheshimiwa Hamis Kigwangala kajitutumua kusema mambo mengi ya Msingi sana kwenye Migodi UKWELI NCH ILIUZWA Toka Mwalimu alipongatuka.Lawama ziende kwa wanaisiasa walioigeuka jamii na kuwa WANA -SI-ASA - WATANZANIA.

Wengine ni wale wote wenye UFAHAMU wa kujifunza ama kwa kuzaliwa ambao wanajua KIPI NI CHEMA NA KIPI SI CHEMA.Dhamila zao uwa zinasemaje kuhusu UKWELI KUHUSU MATENDO YAO NA MIGODI YAO,Mnawezaje kumuangalia mtu anaeliingiza TAIFA kwenye JANGA na bado mkaona ni sawa na kuendele kusihi nae.Kwa migodi tuliyonayo daima Tanzania haikupaswa kuwa NCHI YA KUKINGA MABAKULI.TUNGEKUWA TUNACHAGUA NANI WA KUSHIRIKIANA NAE KATIKA KUUTILIZE MADINI HAYO.

SIO LAZIMA TUWAFUATE WAKOLONI ILI TUFANIKIWE,KWANINI TUSIWE NA KIBURI CHA MUASIASI WETU.HAKIKA OLE WAO WALIO UZA NCHI VIJANA WATAWAFUATA HUKO MLIKO ZIWEKA ZOTE.INGAWA WANAONA HAIWEZAKANI MUNGU ANASABABU.

HATA NAMNA WATAWALA WETU WANAVYOPLEKA MAMBO WENGI WAO WAMEINGIZWA MITEGONI NA VIBALAKA [AGENT] WA WAKOLONI [BLACK MISSION AU BLACKMAIL] KISHA WAO WANAGEUKA KUWA WATUMWA WA MATENDO YAO WAKIATHIBIWA NA MISSION WALIZOTUMBIKIZWA KISHA WENYE MISSION WANA UPROOT MALIASILI NA MADINI.NA KWA KUWA KIONGOZI YUKO NDANI YA BLACKMAIL ANABAKI KUTOA MAAMUZI AMBAYO WANANCHI WANAMSHANGAA.

TIME WILL TELL!!!!!!!!!!!!!!!SOOOOOOON AND VERY SOOOOOOOOOOOOOON!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom