Mume wa mtu ananipa wakati mgumu

whitehorse

JF-Expert Member
Aug 29, 2009
2,565
4,427
Niko kwenye mahusiano na mtu Kwa muda wa miaka 5 sasa. Mwanzoni aliniambia hajaoa na alikuwa anaishi hotel Kwa Sababu alihamishiwa mkoa nilipo Kikazi akitokea mikoa ya kanda ya ziwa.

Sana Sana katika mapenzi yetu niligundua Ni mtu anayejiheshimu Sana hata Kama alikuwa anapretend basi alipretend Kwa kipindi kirefu mno
Baadae alipata nyumba na tukaendelea yeye kwake na Mimi nikiwa kwangu na Mara moja moja tulilala kwake naye kulala kwangu miaka mitatu style ilikuwa hii

Nilimwambia wazi kuwa sina mpango wa kuolewa tangu nilipozalishwa mtoto na baba mtoto wangu kula kona si kutaka tena kuolewa Kwa sasa hivyo awe anajua kuwa siko katika mambo ya mipango na ndoa nayeye

Tulipendana Sana na heshima juu yetu ilishamiri. Mwaka wa nne wa mahusiano yetu alikuja kwangu siku moja akaniambia weekend twende Zanzibar me nikamwambia siwezi Kwa kuwa nitakuwa kazini akasema no no lazima niwe Nawe Zanzibar fanya uwezavyo

Ikabidi ofisini niwapelekee Report fake nikaenda Zanzibar huko jamaa yangu alionekana mkimya na mwenye mawazo Sana

Akatoa Pete mfukoni akaiweka mezani me tena macho yakanitoka Pete yandoa wala sio engagement akasema unaona hii Pete Ni yangu Mimi Ni Mume wa mtu samahani nimekaa Nawe sikuwahi kusema haya Kwa Sababu nakupenda Sana tens Sana sitaki kukukosa na sitakubali kukukosa maishani mwangu

Niliganda Kama nusu hasira zikanipanda wivu ukanikaba japo sikuwa na mpango wa kuolewa lakini Kwa jinsi trend ilivyokuwa inakwenda nilianza kufikiria tukifika miaka 7 ya mahusiano hakika atanibadili mawazo na naweza kuwa mkewe

Ndugu zangu na hata wazazi wangu wameshamuona kukitokea matukio ya mkusanyiko kwetu na upande wao pia Mara kadhaa nimeshaenda japo sio Mara nyingi ila kuna misiba na sherehe Fulani tulishiriki pamoja japo anabeba tabia zile za private life so nimemzoea hivyo hata wakati wa sherehe na misiba ya kwao hatukuwa jirani saana kiasi cha watu kuunga dots me niliona Ni kawaida yake na vile huwa simind kukabana na mtu Kama watoto wadogo mapenzini so sikuweza kugundua kuwa yeye anaprevent nini.

Turudi Zanzibar sasa pale alinibembeleza Sana kiukweli simkumsikiliza maombi yake kawa laingia kushoto lachomokea kulia
Kauli yake ilinifanya kufa ganzi Ni kuniambia mkewe anakuja kuishi nae hapa na ameona Ni vema atafute nyumba ingine Kwa Sababu pale itakuwa Ni picha tofauti Kwa majirani waliotuzoea Kama wapenzi

Nikamwambia sawa nashukuru nakutakia maisha mema he started crying na kubembelezaaa weee nikamwambia nipe muda maana akili yangu haiko sawa kabisa

Tukarudi Safari yetu kweli ilikuwa ya simanzi huku moyoni nikijiambia Mimi na yeye basi japo naumia ila Ni bora nimuache tu Kwa kweli

Nikakaa week moja huku nimeacha mawasiliano yawe upande mmoja wa yeye kunitafuta Mimi. Akaja kwangu one evening ameshakonda na kupungua ya kutosha kabisa akaniambia week ijayo mkewe anakuja nikamwanbia sawa akawa Kama anaishiwa maneno maana me jibu langu lilibaki sawa . Hata Mimi nilikonda pia Kwa Sababu jambo hili lilikuwa sio je je pesi kabisa.

Akaendelea kuja kwangu Sana hata baada ya mkewe kufika na tuakenda hivyo hivyo Hadi ukiingia mwaka huu wa tano . Ila Ni mapenzi tofauti na mwanzo . Akaanza kujitahidi kugharamia assets akaninunulia viwanja viwili na gari yangu akaniambia niuze niagize ingine aka ongeza pesa juu nikaagiza akaenda kulipa ada ya mtoto wangu shuleni Kwa miaka mitatu mbele vitu ambayo hajawahi kufanya kabisa tena Kwa majina yangu hizo asset amezinunua na kunikabadhi nyaraka zote na nilikuwa nazifuatilia mwenyewe . Ni hivi juzi tu nimetoka kuchukua nyaraka ya kiwanja kimoja wapo

Last week alikuja kwangu jioni Mimi nilichelewa kutoka kazini basi nikamkuta kakaa na mwanangu anamsaidia kumalizia home works baadae akapokea simu akaongea kilugha kisha akamaliza akaweka simu pembeni tukaendelea na mazungumzo yetu Mimi na yeye akaaga na kuondoka alisema mke hajisikii vema hivyo amemwambia ende hospital atamkuta huko ikawa bye

Kesho yake asubuhi akapiga simu saa 11 asubuhi akasema kuna tatizo Kumbe Jana alipo malizia kuongea na simu hakuikata so mke wake amefaidi mazungumzo yetu tano yake Kwa hiyo bomu baya limelipuka on my side nikaona haya mambo Ndio siyataki kabisa hii Ni Sababu muafaka ya Mimi kuachana nae for good

Mwanaume akasema usiwa na wasiwasi I'll handle situation me nikabaki na hasira moyoni mwangu cause I need a free man sio Mume wa mtu kila napofikiria kuachana limoyo langu linanisaliti . Nikaacha kupokea simu zake na nikablock namba yake kabisa Kwa kuanzia tu

Akaja akabembeleeza Sana akalia akasema yale yale Maneno ya Zanzibar kuwa hakubali kunikosa. Nikamwambia anipe nafasi na muda wa miezi miwili hivi ili nifikirie akasema miezi miwili mingi nikamwambia msimamo wangu Ni huo akaondoka zake Kwa makubaliano ya mawasiliano ya Mara moja moja Kwa simu ila asije kwangu wala sitaki kukutana nae popote . Nilichofanya nika unblock namba yake ili aweze kupiga na kutuma text

Wana JF Leo nimeamka asubuhi Ni siku 7 tu tangu tukwaruzane na kupeana time and space nakutana na message

"Hello baby , nimemwambia wife everything about us Kwa Sababu sitaki kukukosa please baby don't panic"

Jamani wanaJF hii message yaleo asubuhi imegeuza ulimwengu totally completely nifanyejeee
 
Mume wa mtu sumu. Itaenda weee at the end ukweli utabaki pale pale kuwa he is nit yours at all. So kama umeshaamua hivyo kaa mbali nae, utaumia sana ila mwisho wa siku utazoea kama mjane azikavyo mume. Kama angekuwa anamaanisha hayo yote kwanza angebreakup na wife ukaamini kuwa yu akupenda kweli. Huyo kakuzoea sio anakupenda. Pole lakini
 
Duh! First try and figure out lengo lake la kumwambia mkewe. Is it because he plans to officially leave her for you or was it in hopes that you and the missus can come to terms with the situation and live in harmony moving forward? If it's the former, and you do love or still want to be with him then I'll say go for it! Though at this point for me ingekua shida kumuamini. 4+ years of keeping such a crazy secret...........It seems like he wants to have his cake and eat it too.
 
Sijawahi kuona watu wanao pendana kama ninyi.
Ama kwa hakika mshikilie huyo jamaa, na usiogope wala usiwaze kuhusu mkewe, saaaana jihesabu kama mkewe wa pili na jitahidi uzoee hivyo.
Nikiunganisha maelezo yako yooote naona kabisa jamaa anakupenda kwa dhati, sema inawezekana alijikuta ameoa mke ambae badae aligundua hampendi na pengine ipo shida kwenye ndoa yake, na kwakua umesema kwamba ni mtu wa kupenda maisha ya usiri basi inawezekana aliamua tu kuishi na mkewe na asiyaseme matatizo yao nje kwa kupenda kutunza usiri.
Kimtazamo jamaa anakupenda kuliko anavyo mpenda mkewe.
Nawewe nikiyasona maandishi yako, naona yamejawa narangi ya mihemko ya wivu na donge la jakamoyo....
Ebu tulizana mama ufanye maisha aiseee.....
Kwanza bora hata huyo mume wa mtu anae kupenda kwa dhati kuliko single kaka atakae kupanga kama gari bovu.
Ebu ngoja niishie hapa aiseee..
 
Gari, nyumba, viwanja na kulipa ada ya mtoto hapo hakuna namna.....kubali tu kuwa second wife endelea kutumia fursa..... All the best
 
Fanya maamuzi ya busara maana yaelekea huyo jamaa mapenzi yamemchanganya sana hadi hawezi kufanya maamuzi sahihi...Umeshagundua ni mme wa mtu na anafamilia yake usikubali wewe uje kuwa sababu ya familia yake kuteseka..Na kama ni malipo ya uhusiano wenu nadhani kiwanja sijui na gari si vinatosha..Mpe fact kuwa wewe na yeye basi no matter what...Naamini baada ya huyo mwanamke wake kupewa habari zako hakufurahia na atakuwa busy sana kutaka kukujua live na unadhani nini kitakachofuata kwako?
 
"Hello baby , nimemwambia wife everything about us Kwa Sababu sitaki kukukosa please baby don't panic"

Jamani wanaJF hii message yaleo asubuhi imegeuza ulimwengu totally completely nifanyejeee

Dunia imegeuka in favour of the man. Moyo wako siku mingi ulishatamani kuolewa naye. Usikilize moyo wako na kutenda sawasawa na mapenzi yake. Tayari wewe ni mke mdogo unataka hutaki hivyo we endelea.

Tuliopitia JKT tunajua ktk kulenga shabaha kuna msemo "UKIIONA TARGET ENDELEA". Umeshaiona target unataka ushauri upi tena? Endelea tu
 
Hongera kwa kuopoa mwanaume Bushoke anayelialia kama kama yule waziri mkuu mstaafu. Kwetu ukililia mwanamke ukoo unakutenga usiniambie ni msukuma na kama ni msukuma basi kakulia Dar kwa wanaume wanaokula chips
 
Upo kwenye point of no return, endelea nae hapo mlipofikia wote mwapendana, all in all unataka nini zaidi kwenye mapenzi, mkamatie huyo huyo, ukimwacha utakuja tena humu kulialia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom