Mbelwa Germano
JF-Expert Member
- May 7, 2011
- 789
- 289
Imepita kama siku tatu hizi,pale ambapo nilimsikia katibu wa CCM bwana Wilson Mukama kwenye taarifa ya habari ya TBC1 saa mbili usiku akibeza viongozi wa CHADEMA wakitembelea kaburi la Baba wa Taifa. Baada ya taarifa ile nilijiuliza maswali machache kama ifuatavyo:
- Ni dhambi kwa vingozi wa CHADEMA kutembelea kaburi la baba wa Taifa?
- Je, CCM wana hati miliki ya kaburi la baba wa Taifa?
- Viongozi wa CHADEMA ni Watanzania sawa na wale wa CCM, vilevile hata ambao sio watanzania wanaweza kutembelea kaburi la Baba wa taifa,Je Mukama anataka kutufundisha nini kuhusu hili?