Mugabe kama Kibaki?

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
UCHAGUZI Mkuu wa Zimbabwe unaelekea kwenye mkondo ule ule wa Kenya. Tume ya Uchaguzi inatoa matangazo kwa jinsi inayotia wasiwasi. Lakini dalili zinaonyesha upinzani umechukua viti vingi zaidi au umeshinda. Baadhi ya taarifa zinasema hadi sasa, upinzani umepata viti vingi zaidi (74); chama tawala ZANU-PF cha Rais Robert Mugabe kina viti 64. Mawaziri watatu wa Rais Mugabe wameangushwa. Kura za urais bado ni siri ya tume, lakini upepo unaonyesha mambo ni magumu kwa Mugabe, na tetesi ni kwamba tume inajaribu kumfanyie kile ambacho ile ya Kenya ilimfanyia Mwai Kibaki, ikamtangaza mshindi akiwa na kura chache zenye utata. Taarifa nyingine zinasema tayari Mugabe ameshajulishwa kwamba ameshindwa, na watu wake wanajadiliana namna ya kukabidhi madaraka kwa mshindi. Maana tayari upinzani umeshaanza majadiliano na majeshi ya Zimbabwe. Tusubiri!
Source: http://ngurumo.blogspot.com
 
Back
Top Bottom