Doyi
JF-Expert Member
- Dec 4, 2011
- 1,428
- 1,475
Leo nikiwa katika mihangaiko yangu nilienda Muhimbili kumuona ndugu yangu mmoja amelazwa pale sewahaji na nilipotoka nikaamua kutembea kuona chama langu la AZANIA SEC SCHOOL (nilimaliza hapo o level mwaka 2002 ) .kwa kweli nimeamini dunia inatutupa mkono mno mnoo.
Mazingira yamechange mno na hizo ni baadhi ya picha nilizobahatika kupiga kwa kuwa sikuwa na chaji ya kutosha katika simu nimekumbuka viiingi na mengi na nikapata furaha na huzuni kwa wakat mmoja(wana saikolojia hili wanalielewa) nimewakuta madogo wa form 5 wanajisomea wengi wakat namaliza wanasema walikuwa hawajazaliwa.
Kimsingi mambo mengi yamebadilika hasa lile boda la kwenda fire kupitia njia ya ndani ya shule ya sekondary jangwani wamelifungia siku hizi wakat sisi tulikuwa tunapita free tu kama kuna wana Azania wenzangu humu tujuane na tukumbushane vituko vya walimu kama Kwayu, Mchwa mpaka, vipanga wa enzi hizo kina Wenzi,
Pia nimewakumbuka sana marafiki zangu kama kina Onesphory, Victor Koroso, Chimpa, Mayagi, Deo, Isack, Shomary na wengine weeengi, lama kuna wadau wa Azania waliomaliza miaka kuanzia 2000- 2002 pls tushee kumbukumbu zozote za shule yetu ikibidi kufanya get together party moja tukutane hapo hata tupige stor mbili tatu na hata kuchangia chochote tutakachojaaliwa ili kusaport chama letu la Azania maana wengi limetutoa sana saaanaa.
NB: Kama wewe hukusoma Azania pia unakaribishwa kuchangia lolote hata la shulen kwako kunogesha sired hii asante wadau 🥲