Msimamo wa wabunge wa Upinzani baada ya kutolewa bungeni jana

Emma.

JF-Expert Member
Jun 25, 2012
19,935
5,559
Heshima kwenu wana JF,

Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA)wakiongozana na mbunge wa ACT Zitto kabwe wameeleza kamwe hawataacha serikali iendelee kuwanyima wananchi haki ya kikatiba kwa kuwazuia kutoa na kupata habari.

Viongozi hao wa UKAWA waliwaonyooshea vidole wabunge wa CCM kwamba ni wanafiki, kwa sababu wao (wapinzani )wakijadiliana na kamati ya Uongozi wa Bunge, walikuwa wakipokea vimemo wakiomba waendelea kupambana kwa sababu hata wao hawapendi yanaendelea kufanywa.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wenzake wa UKAWA Mwenyekiti mwenza wa UKAWA, Freeman Mbowe alisema wanalaani udhalilishwaji waliofanyiwa wabunge wa upinzani bungeni, kwa kutumia askari wenye silaha mbalimbali na mbwa, kwamba ni ukiukwaji wa haki za bunge.

Amesema sababu zilitolewa serikali kuzuia TBC kurusha moja kwa moja matukio ya bungeni hazina mashiko na kwamba wamebaini mambo matano yanayoipa serikali kiwewe mpaka kufikia hatua hiyo.
Hata hivyo Mbowe amesema hawajasusia vikao vya bunge, leo wataendelea kushiriki shughuli za bunge kama kawaida lakini wakiendelea kudai haki za kikanuni na kikatiba kuzingatiwa, kwa maslahi ya watanzania wote.

Mambo matano yanayoipa serikali kiwewe ni kuhusu hali ya kisiasa Zanzibar,kasoro zilizojitokeza kwenye uchaguzi uliyomalizika 2015,maamuzi yanayochukuliwa na baadhi ya viongozi wa serikali awamu ya tano, bila kufuata kanuni mbalimbali kwa kisingizio cha kutumbua majibu. Na swala la katiba mpya.

Naye Mwenyekiti mwenza wa UKAWA James Mbatia amesema wabunge wengi kwa sasa wanafanya siasa za kizazi kipya, hawatokubali kurudishwa kwenye enzi za 'zidumu fikra za Mwenyekiti ' Mbatia amesema "Tuko tayari kuuawa sote lakini ifahamike hilo likitokea, wengine wataendelea kujitokeza kuendeleza madai mpaka haki itapopatikana "
 
Ni jambo kubwa la kusikitisha na kuuzunisha kufanyika Tanzania tena kwenye Sarikali hii ya awamu ya tano
.
Nilimwamini JPM kuwa anania ya dhati ya kuisafisha uozo wa nchi hii, pia niliamini angelitumia bunge Barbara kuwaumbua na kuwatokomeza wanyonyaji.
Bado siamini hiki kinachotokea kama kinabaraka za JPM au ni sarakasi za Nape na chama chake.
 
Ni jambo kubwa la kusikitisha na kuuzunisha kufanyika Tanzania tena kwenye Sarikali hii ya awamu ya tano
.
Nilimwamini JPM kuwa anania ya dhati ya kuisafisha uozo wa nchi hii, pia niliamini angelitumia bunge Barbara kuwaumbua na kuwatokomeza wanyonyaji.
Bado siamini hiki kinachotokea kama kinabaraka za JPM au ni sarakasi za Nape na chama chake.
Na

Kuruhusu askari wenye silaha za moto na mbwa kuingizwa ndani ya ukumbi wa bunge
Kwanisheria gani inazuia askari wenye siraha kuingia bungeni?
 
Ni jambo kubwa la kusikitisha na kuuzunisha kufanyika Tanzania tena kwenye Sarikali hii ya awamu ya tano
.
Nilimwamini JPM kuwa anania ya dhati ya kuisafisha uozo wa nchi hii, pia niliamini angelitumia bunge Barbara kuwaumbua na kuwatokomeza wanyonyaji.
Bado siamini hiki kinachotokea kama kinabaraka za JPM au ni sarakasi za Nape na chama chake.
Na

Kuruhusu askari wenye silaha za moto na mbwa kuingizwa ndani ya ukumbi wa bunge

Panapotokea dalili za wazi za uvunjifu wa amani jukumu la kulinda Raia na mali zao ni jukumu la msingi la Serikali na hakuna sheria wala kanuni ya ku over ride hii! Serikal haiwezi kusubiri kuona ngeu au damu inamwagika bungeni eti ikisubiri kutengua kanuni ili kutuliza amani bungeni. Mijadala ya Escrow na Richmond ilikuwa mikali zaid ya huo wa TBC na Live coverage uliwaona Askari ndani ya bunge? Hata nyumbani kwako mtu haruhusiwi kuingia ndani bila ya idhini yako lakini zipo exeptional za kufanya hivyo.
Kufanya vurugu bungeni kulilia kuoneshwa live ni uhayawani.
 
Mbowe anasema watapigania Kuzingatiwa Kanuni na Sheria! Ni sheria ipi au kanuni ipi inaelekeza Live Coverage ya TBC? Wajuzi wa sheria wanisaidie?
Ni nchi ya wehu tu ambao wanaweza kupuuza vyombo vya habari visiweze kuonesha kipi kinafanywa na wawakilishi wao

Wakati Japan, Korea, Indonesia, Uingereza, ukerumani na nyinginezo hutumia media ili mawaziri waweze kupata mrejesho kwa wananchi ccm inakataza?


Kama ccm inaona TBC itaingia gharama kurusha Live kwa nini ccm imewazuia wamiliki wa vyombo vingine kurusha?


Ni miaka mitatu nyuma, vyombo vya Chanel ten, ITV na Star TV walikuwa wanarusha kwa nini baada ya ccm kubanwa na ufisadi wao ikaleta hoja ya kuzuia vyombo binafsi kurusha matangazo?

Ukweli ni kuwa chama chochote kinachozuia vyombo vya habari visirushe matangazo harafu kinadai kypambana na rushwa ni ishara ya chama hicho kufilisika kifikra na kumezwa na ufisadi
 
Heshima kwenu Wana JF
Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA)wakiongozana na mbunge wa ACT Zitto kabwe wameeleza kamwe hawataacha serikali iendelee kuwanyima wananchi haki ya kikatiba kwa kuwazuia kutoa na kupata habari.
Viongozi hao wa UKAWA waliwaonyooshea vidole wabunge wa CCM kwamba ni wanafiki, kwa sababu wao (wapinzani )wakijadiliana na kamati ya Uongozi wa Bunge, walikuwa wakipokea vimemo wakiomba waendelea kupambana kwa sababu hata wao hawapendi yanaendelea kufanywa.
Akizungumza kwa niaba ya viongozi wenzake wa UKAWA Mwenyekiti mwenza wa UKAWA, Freeman Mbowe alisema wanalaani udhalilishwaji waliofanyiwa wabunge wa upinzani bungeni, kwa kutumia Askari wenye silaha mbalimbali na mbwa, kwamba ni ukiukwaji wa haki za bunge.
Amesema sababu zilitolewa serikali kuzuia TBC kurusha moja kwa moja matukio ya bungeni hazina mashiko na kwamba wamebaini mambo matano yanayoipa serikali kiwewe mpaka kufikia hatua hiyo.
Hata hivyo Mbowe amesema hawajasusia vikao vya bunge, leo wataendelea kushiriki shughuli za bunge kama kawaida lakini wakiendelea kudai haki za kikanuni na kikatiba kuzingatiwa, kwa maslahi ya watanzania wote. Mambo matano yanayoipa serikali kiwewe ni kuhusu hali ya kisiasa Zanzibar,kasoro zilizojitokeza kwenye uchaguzi uliyomalizika 2015,maamuzi yanayochukuliwa na baadhi ya viongozi wa serikali awamu ya tano, bila kufuata kanuni mbalimbali kwa kisingizio cha kutumbua majibu. Na swala la katiba mpya. Naye Mwenyekiti mwenza wa UKAWA James Mbatia amesema wabunge wengi kwa sasa wanafanya siasa za kizazi kipya, hawatokubali kurudishwa kwenye enzi za 'zidumu fikra za Mwenyekiti ' Mbatia amesema "Tuko tayari kuuawa sote lakini ifahamike hilo likitokea, wengine wataendelea kujitokeza kuendeleza madai mpaka haki itapopatikana "
Nina mashaka na Mh. Nape kama kweli alijua kile alichokiamua jana. Nadhani hata Mkulu JPM ameona Jipu jingine, ngoja tusubiri tuone.
 
Mbowe anasema watapigania Kuzingatiwa Kanuni na Sheria! Ni sheria ipi au kanuni ipi inaelekeza Live Coverage ya TBC? Wajuzi wa sheria wanisaidie?
Kama utakua na kichwa sahihi utakumbuka spika sitta aliahirisha bunge la katiba kisa tu TBC walizima matangazo akat tundu lissu anawasilisha mada kwa nini,
 
Ni nchi ya wehu tu ambao wanaweza kupuuza vyombo vya habari visiweze kuonesha kipi kinafanywa na wawakilishi wao

Wakati Japan, Korea, Indonesia, Uingereza, ukerumani na nyinginezo hutumia media ili mawaziri waweze kupata mrejesho kwa wananchi ccm inakataza?


Kama ccm inaona TBC itaingia gharama kurusha Live kwa nini ccm imewazuia wamiliki wa vyombo vingine kurusha?


Ni miaka mitatu nyuma, vyombo vya Chanel ten, ITV na Star TV walikuwa wanarusha kwa nini baada ya ccm kubanwa na ufisadi wao ikaleta hoja ya kuzuia vyombo binafsi kurusha matangazo?

Ukweli ni kuwa chama chochote kinachozuia vyombo vya habari visirushe matangazo harafu kinadai kypambana na rushwa ni ishara ya chama hicho kufilisika kifikra na kumezwa na ufisadi
Kwani wanaorusha matangazo ni TBC1 pekee? mbona sijawahi kusikia STAR BUNGE wakidai hawana fedha za kulipia urushwaji wa matangazo? Kama TBC1 hawana uwezo wa kurusha Live kwa nini serikali isiruhusu wenye uwezo wa kurusha live warushe? NAHISI HILI NALO NI JIPU. JPJM njoo huku bungeni kuna jipu jingine!
 
Ni nchi ya wehu tu ambao wanaweza kupuuza vyombo vya habari visiweze kuonesha kipi kinafanywa na wawakilishi wao

Wakati Japan, Korea, Indonesia, Uingereza, ukerumani na nyinginezo hutumia media ili mawaziri waweze kupata mrejesho kwa wananchi ccm inakataza?


Kama ccm inaona TBC itaingia gharama kurusha Live kwa nini ccm imewazuia wamiliki wa vyombo vingine kurusha?


Ni miaka mitatu nyuma, vyombo vya Chanel ten, ITV na Star TV walikuwa wanarusha kwa nini baada ya ccm kubanwa na ufisadi wao ikaleta hoja ya kuzuia vyombo binafsi kurusha matangazo?

Ukweli ni kuwa chama chochote kinachozuia vyombo vya habari visirushe matangazo harafu kinadai kypambana na rushwa ni ishara ya chama hicho kufilisika kifikra na kumezwa na ufisadi

Achana na maelezo marefu nimeuliza nitajie kifungu kipi cha sheria au kanuni kimekiukwa kama alivyosema Mh. Mbowe?
 
Magufuli ingilia kati ccm Membe na Jk term wanakupiga vita chini kwa chini .
 
Nashauri vyama vinavyounda UKAWA viichangie fedha televisheni ya Taifa - ITV kurusha live matangazo yote ya Bunge.
 
Watanzania tusione Bunge live eti gharama hapana iyo aingii akilini kabisa..labda mje na hoja nyingine kwa dunia ya sasa ilo mnarudi nyuma..enzi za stone Age..
 
Back
Top Bottom