Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
View attachment 45554
Ushiriki wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na Viongozi na wanachama wa chama hicho katika msiba wa marehemu Rejia Mtema umethibitisha kwamba siasa si ugomvi wala chuzi.
Nimehudhuria kuagwa kwa mara ya mwisho mwili wa marehemu Rejia Mtema katika viwanja vya Karimjee na kuwaona wana CCM na wana CDM kwa pamoja wakiomboleza kwa kupeana pole na kukumbatiana. Kwa hakika hakukuwa na kuitana MAGWANDA wala MAGAMBA.... wote walikuwa ni wamoja hata wale wa vyama vingine vikiwemo CUF, NCCR - Mageuzi, TLP, UDP na vingine.
Hata Spika wa Bunge Mama Anne Makinda alithibitisha kuwa " Kelele zinazopigwa na watu wa vyama vya siasa ni ngonjela tu, mwisho wa siku wao ni kitu kimoja kwa utanzania wao"
My take: Ushirikiano ulioonekana udumu si katika mambo ya misiba tu bali na mengineyo ya kujenga nchi likiwemo la katiba mpya tunaloliendea na mengineyo kwa ustawi wa Taifa.
Ushiriki wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na Viongozi na wanachama wa chama hicho katika msiba wa marehemu Rejia Mtema umethibitisha kwamba siasa si ugomvi wala chuzi.
Nimehudhuria kuagwa kwa mara ya mwisho mwili wa marehemu Rejia Mtema katika viwanja vya Karimjee na kuwaona wana CCM na wana CDM kwa pamoja wakiomboleza kwa kupeana pole na kukumbatiana. Kwa hakika hakukuwa na kuitana MAGWANDA wala MAGAMBA.... wote walikuwa ni wamoja hata wale wa vyama vingine vikiwemo CUF, NCCR - Mageuzi, TLP, UDP na vingine.
Hata Spika wa Bunge Mama Anne Makinda alithibitisha kuwa " Kelele zinazopigwa na watu wa vyama vya siasa ni ngonjela tu, mwisho wa siku wao ni kitu kimoja kwa utanzania wao"
My take: Ushirikiano ulioonekana udumu si katika mambo ya misiba tu bali na mengineyo ya kujenga nchi likiwemo la katiba mpya tunaloliendea na mengineyo kwa ustawi wa Taifa.