Mshahara wa Nehemia Mchechu wa NHC ni USD 19,000 kwa mwezi

Status
Not open for further replies.
Dah....awa wakurugenzi ndio wanafaidi matunda ya uhuru.Sisi wavuja jasho tutaendelea tu kuisoma namba.
CCM mbele kwa mbele.
 
2kimo,

Upo vizuri sana upstairs. Safi sana kaka kwa maelezo yako hapo.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mambo mengine ukiyasikiliza utashikwa na butwaa,anacho sahau ni kwamba hilo ni shirika la UMMA sio mali au kampuni ya ukoo na mnacho kihita eti faida notwithstanding,Watanzania tunapumbazwa na uyoga wa majengo ya gharama lukuki not knowing kwamba yote hayo yamejengwa kwa mkopo kwa masharti ya kutia shaka - kuna mtu mweledi aliwahi kuonya kuhusu ukurupukaji wa uwekezaji holela lakini ni watu wachache walio muelewa.

Binafsi nachukulia miradi hii ya NHC ambayo haina breki kama ni a ticking time bomb inayo subili kulipuka as time goes by,tatizo la Watanzania tulio wengi tunaongozwa na mob saikologe wakisha msifia mtu basi hakuna mwenye ubavu wa kuhoji uwekezaji unao fanywa na shirika hili ambao mwingine umekaa ndio sivyo, tunawapa Wakuu wa mashirika a blank cheque wafanye wapendalo bila ya kuhojiwa,
hakuna cha check and balance wala nini sijui!!!

Kwa nini mtu usijiulize hivi inakuwaje Mkuu wa shirika anakuwa Judge,Jurry na excutioner all rolled in ONE


Halafu hasara itakuja kurudishwa kwetu walala hoi, hebu watuwawe na hofu ya Mungu na kuonea huruma ya wengi wanaopigika vijijini
 
Mleta hoja anapaswa kulinganisha an apple with an apple. Sio sahihi kumlinganisha mbunge na Mtendaji mkuu wa shirika anayezalisha. Benchmarking ya politicians ati ndio wawe na mishahara mikubwa is a misplaced proposal. Nchi hii hatusongi mbele kwasababu ya wana siasa.

Kiukweli, mie nilidhani huyo Mkurugenzi anapata zaidi ya shs 60m. Kama ni kweli anapata shs 36.5m tu, he is fairly cheap. Kumbuka huyo jamaa ametoka kwenye private sector, ukitaka kuvutia vichwa zaidi yake, aise hiyo pesa ni ndogo kabisa.

Wengine hatutaki kuiba, better be paid well, na ufanye mambo yako kihalali.
 
HAMY-D;
Mbona mna kawaida ya kuanza na dagaa mnaacha papa? Tueleze uhalali wa weye mbunge kupata nyongeza hiyo si kutafuta wenzio wanakula ngapi.
Kazi anayoifanya Mchechu unailinganisha na "Ndiyooo" tunayoisikia bungeni? Mbona unaogopa kuanza na yule wa TANAPA? Unaogopa kupotea au?
Usihalalishe uchafu wako kwa kuonesha wengine

wewe jamaa bongazi kweli kwa hiyo ulitaka iweje si amesema ataanza na huyu wa nhf
 
ndo tatizo la kuwa na wabunge af wanatumia fake accounts humu. mtu kuhoji milion 130 au milion36 kama mshahara ni umbea? mnadhani hii kauli mtu maskini anaweza kutamka? haiwaumI kwasababu we unaecomment inawezekana ni mbunge au ndugu yako mbunge! muwafkirie na walala hoi jamani

Mbona na wewe unatumia fake account?
 
To me kazi za mbunge sioni kama zina tija yoyote, ukiwa mbunge wa mikoa kama Dodoma, Singida, Tabora na mikoa mingi ya pwani (ukitoa Dar but including Morogoro) na ukawa unapendwa na chama chako hasa ccm, huhitaji kutumia akili yoyote kwenye kazi yako ya ubunge na still utaendelea kua mbunge; wabunge hawazalishi faida yoyote kwa taifa but wakurugenzi wa mashirika ya umma wazalisha faida (monetary) na ndio hizo pesa wanazo zalisha nyingine wanakula wabunge. Hebu niambie kwamfano nchi ikiwa na wabunge 50 tu, tutapata hasara gani? Na jiulize kwa mfano tusipokua na ceo wa shirika lolote la serikali tutapata faida au hasara? Kazi za siasa nchi hi zimepewa kipaumbele sana kuliko za kitaalamu, ningependa sasa kupitia kubana matumizi kulikofanywa na mhe Pombe kuwanufaishe madaktari, manesi, walimu, askari wote wa majeshi yote hasa magereza (kwa utafiti wangu nadhani hawa ndio wanaishi maisha magumu zaidi kuliko askari wengine) na hao ma ceo waendlee kujilipa kadiri wanavyozalisha. Kabla ya Nehemia Mchechu hajawa CEO wa NHC, shirika hilo lilikua halina vision wala mission but through him tumeona umuhimu wa shirika hilo, tumtie moyo zaidi badala ya kumkatisha tamaa. Ungenambia watu kama yule w TIC, SSRA ningekuelewa cause ukweli hayo mashirika sioni TIJA yake kwa taifa zaidi ya kuongezeana ulaji tu.

Endelea kumsifia lakini hujui kuwa shirika lina madeni makubwa sana na yeye mkataba wake utaisha na shirika ataliacha katika hali ya kukabwa na mabenki.

Sioni cha maana alichofanya Mchechu NHC zaidi ya kuliingiza shirika kwenye madeni tu. Na mbaya zaidi miradi ina returns ndogo kulinganisha na zile ambazo zilikuwa anticipated...hii ni hatari sana kwa maana madeni yatashindwa kulipwa na shirika litafilisiwa na mabenki na hilo likifanyika itakula kwetu Watanzania maana sisi ndio wenye shirika.
 
Kwani alijipangia mwenyewe au ndicho alichokubaliana nacho na waliomwajiri?

Hoja yako ni ya kijinga sana. Kwahiyo kwanini tunalalama kuhusu maslahi ya wabunge...kwani wabunge wamejipangia wenyewe!? Si ni makubaliano yao wenyewe huko Bungeni? Sasa hizi kelele huku mtaani za nini?
 
Faida anaileta personally au kama kampuni? Na ingekua kulipwa ni directly proportion watafiti wangepewa kiasi gani? Think big banaa

Ni controversial kudai CEO alipwe hela nyingi eti anadhalisha? Je watumishi wengine wasiodhalisha pesa lakini wanadhalisha Elimu, tafiti, tabibu, mawasiliano utawarate vipi mishahara yao??

Kwa ufupi hakuna mfanyakazi asiyedhalisha kinachotakiwa ni rate za mishahara ziwe proportional na kazi kuwa Dr, PhD siyo kigezo cha kulipwa mshara mkubwa
 
Hivi kazi anayofanya Rished Bade pale TRA utataka kumlipa million 3?? Kazi anayofanya Massawe pale TPA utataka kumlipa Million 3?? MD wa NSSF au PPF au TANAPA utataka kuwalipa mishahara ya hivyo?? Mkuu Msechu anafanya miradi mpaka ya mpaka 100 Billion, ukitaka kumlipa kimshahara cha million 3 si unataka kumwingiza kwenye matatizo tu?? Rished Bade anakusanya 800 Billion a month, ukitaka kumlipa Million 3 si unataka kumsababishia matatizo tu?? Hivi hawa wabunge wetu wengi wanafanya nini cha maana zaidi ya kugonga meza na kupitisha sheria zenye loopholes kibao kule bungeni??

hahahahahaha kila mtu anasimamia pesa ndefu sehemu yake kumlipa kimshahara hicho kutafuta matatizo rais anasimamia fedha za nchi nzima alipwe shilingi ngapi? Je vipi waziri, wakurungezi , wakuu wa wilaya , bure kabisa wewe.
 
Hoja yako ni ya kijinga sana. Kwahiyo kwanini tunalalama kuhusu maslahi ya wabunge...kwani wabunge wamejipangia wenyewe!? Si ni makubaliano yao wenyewe huko Bungeni? Sasa hizi kelele huku mtaani za nini?

Naweza kuwa na hoja ya kijinga. Lakini hebu tofautisha ubunge na ajira. Umetangaza kazi nq mimi nikaomba kisha tukadiskasi terms nikakwambia nataka mshahara wa 36.5m na wewe ukakubali tatizo liko wapi? Ndio maana nikauliza hilo swali langu la kijinga.
 
Sasa mnataka alipwe milioni 2?si ndio mwanzo wa kupata tamaa za kuiba?huyo kwa experience yake na kulingana na ukubwa wa ajira yake equivalent na ma CEO wenzake kwenye mashirika ya serikali hata binafsi ni sahihi kabisa
 
Tsh. 36m haizidi $17k kwa mwezi, ni mshahara wa kawaida sana kwa Mkuu wa Shirika ambaye ufanisi wake haufichiki.
Kulipa wafanyakazi vizuri ni njia mojawapo ya kuzuia tamaa za wizi, sioni tatizo na Mshahara wa Tsh. 36m.
 
Hivi kazi anayofanya Rished Bade pale TRA utataka kumlipa million 3?? Kazi anayofanya Massawe pale TPA utataka kumlipa Million 3?? MD wa NSSF au PPF au TANAPA utataka kuwalipa mishahara ya hivyo?? Mkuu Msechu anafanya miradi mpaka ya mpaka 100 Billion, ukitaka kumlipa kimshahara cha million 3 si unataka kumwingiza kwenye matatizo tu?? Rished Bade anakusanya 800 Billion a month, ukitaka kumlipa Million 3 si unataka kumsababishia matatizo tu?? Hivi hawa wabunge wetu wengi wanafanya nini cha maana zaidi ya kugonga meza na kupitisha sheria zenye loopholes kibao kule bungeni??

Wapewe mshahara wa kiasi kinachoendana na hali ya uchumi wetu pamoja na pefomance yao,

pia wapewe target wakishindwa kufikia target tunawafire, mfano TRA kukusanya bill 800 a month ni uzembe, bado performance ya taasisi nyingi IPO chini sana, sisi tuliopo kwenye private sector tunsona mapungufu mengi sana

Pomoja na hayo tuwe na sheria Kali kama za China ukilamba rushwa unakula shaba hadharani Siku ya ijumaa pale viwanja vya mnazi mmoja
 
Nadhani baada ya kuondolewa SCOPO mashirika ya umma yanajiendesha yenyewe kwa usimamizi wa bodi zao. Haya masuala ya mishahara ni makubaliano ya mwajiri na mwajiriwa.
 
Endelea kumsifia lakini hujui kuwa shirika lina madeni makubwa sana na yeye mkataba wake utaisha na shirika ataliacha katika hali ya kukabwa na mabenki.

Sioni cha maana alichofanya Mchechu NHC zaidi ya kuliingiza shirika kwenye madeni tu. Na mbaya zaidi miradi ina returns ndogo kulinganisha na zile ambazo zilikuwa anticipated...hii ni hatari sana kwa maana madeni yatashindwa kulipwa na shirika litafilisiwa na mabenki na hilo likifanyika itakula kwetu Watanzania maana sisi ndio wenye shirika.
Mkuu hupo sahihi kabisa ni watu wachache watakao kuelewa,ukiangalia vizuri na mimi nilitoa angalizo hilo mapema - chukulia mfano wa mashariti ya mikopo ya Benki na ujenzi wa Project ya pale Morocco,unajua nini kitatokea baada ya miaka kupita? Benki itanyanganya NHC jengo pamoja na aridhi!!! Kuna mikataba mengine ya ajabu kweli kweli.
 
Tsh. 36m haizidi $17k kwa mwezi, ni mshahara wa kawaida sana kwa Mkuu wa Shirika ambaye ufanisi wake haufichiki.
Kulipa wafanyakazi vizuri ni njia mojawapo ya kuzuia tamaa za wizi, sioni tatizo na Mshahara wa Tsh. 36m.

Wenzetu wakilipwa huo mshahara ni sawa kwa kuwa unajumuisha maposho (all inclusive) sana sana hapo ataongezewa Insurance tu!
Structure ya mishara ya Tanzania ni ya kiwizi wizi na Kukwepa Kodi...
Ukilipa mtu huo mshahara mwisho wa mwezi anapata tena ZIADA ya karibia millioni Kumi (10,000,000 ) au zaidi ya maposho yasiyo kuwa hata na umuhimu.
Inakuwaje mtu akae kikao cha kufuatilia kazi yake ndani ya shirika alipwe posho!!!
Waende private sector wakaone...hakuna huo Ujinga!!!!
Ndio sababu mashirika binafsi yana songa mbele, ya kwetu ya Umma yana sua sua!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom