msaada wa maombezi

kichakorojack

Member
Sep 19, 2011
78
12
Habari za muda huu wapendwa. Naombeni msaada wenu, nimesikia kwamba kanisa la nabii florah linapatikana mbezi beach, ni sehemu gani hapo mbezi beach? Then if kuna mtu anayemjua mchungaji/mtumishi wa mungu ambaye anaona ni nabii wa kweli maana siku hizi wengine wa kweli wengine wa uongo, kuna mtu anashida sana anahitaji maombezi. Asanteni kwa msaada wenu.
 
aanze kujiombea mwenyewe huyo mtu, ndio atafute msaada kwa wengine.

Nguvu za uponyaji tumepewa equal waamini wote, ni kuamua tu kuzitumia.
 
Acheni utapeli na kutangaza biashara yenu kijanja. We sema wewe ndiyo huyo Florah mwenyewe. Kwanza unaombea umekufa au unajichulia. Mijitu mingine inatia kinyaa. Kwanini uombewe kana kwamba wewe ni kichaa au maiti. Jiombee mwenyewe acha ushirikina. Huyo Florah naye ni tapeli kama akina Rwakatare. Kama unajua wapo waongo huyo Florah wako ambaye hujui hata kanisa au duka lake la uroho mtakakitu lilipo unamwaamini vipi kama siyo ujinga na utoto wa kudhani wote ni wajinga na majuha wenzio? Kongosho mwana umesema vyema. Huyu Kichakorojack ahitaji kuombewa bali kuambiwa---- ujinga huo.
 
Mgonjwa wako inabidi hawe na Imani au asimamie Imani yako,piaunaweza kwenda sehemu yoyote watakusaidia kuna Dpc kindondoni,TAG Kinondoni,Makanisa yote TAG,EAGT,FPCT na mengineyo yote ya kipentecost, yanafanya huduma hizo.

Ubarikiwe.
 
Hahaha, Father of All, hata bible imeandika. Wataweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya. Wakati mwingine mtu wala hahitaji maombi, zaidi anahitaji counselling.
I have my reservations kuhusu nabii flora and some famous pastors though, maana focus ni juu yao na sio Bwana mtoa uzima. Maombezi hayapashwi.kuwa kama uganga wa kienyeji, kuwa asipokuwepo mwenyewe hayafanyiki.
 
Last edited by a moderator:
King'asti mwanangu umenena ambayo nilitaka kuongezea lakini nikasita. Hao wanaoitwa famous pastors ni famous money makers who can sell even indulgence as it once happened in the Roman Church. These are the John Tetzel of today who can do anything to get the monies. Huyo anayetaka kuombewa narudia anahitaji kuambiwa kuwa ni mshirikina na mjinga wa kawaida ataibiwa bure.
 
kha watu wanavyo support mambo ya ngono nao wamo katika mambo ya mombezi na damu ya mwanakondoo...kweli wasanii wapo wengi
 
Ukitokea mjini kama unaenda banana, kuna matuta kabla kidogo ya kufika kituo cha daladala cha banana, kwenye hayo matuta anagalia upande wako wa kulia opposite na gate la shule ya minazi mirefu(?) kuna kanisa la Winners Chapel International. Utapata huduma hapo. Ila jaribu kwenda siku za kazi kuanzia kama saa tatu asubuhi, maana j'pili na siku za ibada wenye kuhitaji counselling na maombi wanakuwa wengi mno na muda ni mfupi. Cheers!!!
 
Mgonjwa wako inabidi hawe na Imani au asimamie Imani yako,piaunaweza kwenda sehemu yoyote watakusaidia kuna Dpc kindondoni,TAG Kinondoni,Makanisa yote TAG,EAGT,FPCT na mengineyo yote ya kipentecost, yanafanya huduma hizo.

Ubarikiwe.

nakushukuru sana, nawe pia ubarikiwe
 
yaani wewe acha tu

ila ukikuana na mhubiri wa kweli anakuambia, kila mtu chanzo cha tatizo lake huwa analijua.

Mimi nialike tu kukusaidia kuomba, lakini ni jukumu lako kujiombea maana tumepewa nguvu sawa wote.

Alichosema ni hiki, watu wanakimbilia kuombewa wakati hata Mungu wanayemuomba hawamjui ni Mungu yupi.

Akawa anasema, Mungu wangu si lazima awe wako, japo wote tunatumia bibilia moja.

Cha kwanza, jua unamtumikia Mungu gani, ndio uombe, na uwaalike wengine waombe pamoja nawe.

Mtu anaenda kuombewa, kumbe tatizo lake liko kwenye ukoo, mchungaji atakusaidia nini??

Au mtu anaombewa maisha yaboreke, wakati ni mvivu au mfujaji wa mali?

Mtu ananeda aombewe ana mapepo wakati kutwa kucha kwa waganga? Na labda keshafunga nao agano?

Akawa anasema, mtu na ajiombee mwenyewe tu, wengine watamsaidia lakini hawawezi ondoa tatizo lake.

Hahaha, Father of All, hata bible imeandika. Wataweka mikono juu ya wagonjwa nao watapata afya. Wakati mwingine mtu wala hahitaji maombi, zaidi anahitaji counselling.
I have my reservations kuhusu nabii flora and some famous pastors though, maana focus ni juu yao na sio Bwana mtoa uzima. Maombezi hayapashwi.kuwa kama uganga wa kienyeji, kuwa asipokuwepo mwenyewe hayafanyiki.
 
Last edited by a moderator:
ushawahi kujifungia ukaombaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa kabla ya kwenda kwa muombezi?
wachungaji wenyewe wa siku hizi hawa mmmmh kuwa makini
 
Habari za muda huu wapendwa. Naombeni msaada wenu, nimesikia kwamba kanisa la nabii florah linapatikana mbezi beach, ni sehemu gani hapo mbezi beach? Then if kuna mtu anayemjua mchungaji/mtumishi wa mungu ambaye anaona ni nabii wa kweli maana siku hizi wengine wa kweli wengine wa uongo, kuna mtu anashida sana anahitaji maombezi. Asanteni kwa msaada wenu.

Are u a born again christian? tafuta kanisa uokoke then ufundishwe jinsi ya kuishi ktk imani na namna ya kushinda nguvu za giza ktk maisha yako , acha kukimbilia hao manabii wapya wa siku hizi wengine wanatumia nguvu nyingine japokuwa wanmtaja yesu be careful utavamiwa na roho nyingine.
 
Anatakiwa kabla hajaenda kuombewa awe na imani na alijue neno akilijua neno alisimamie aombe kwa bidii akikiri uponyaji na kila mara amkumbushe Mungu kwa kinywa chake kwamba anahitaji uponyaji atapona tu, akienda huko atapona kwa muda tu lakini baadae hali itamrudia maana atajisahau.
 
Habari za muda huu wapendwa. Naombeni msaada wenu, nimesikia kwamba kanisa la nabii florah linapatikana mbezi beach, ni sehemu gani hapo mbezi beach? Then if kuna mtu anayemjua mchungaji/mtumishi wa mungu ambaye anaona ni nabii wa kweli maana siku hizi wengine wa kweli wengine wa uongo, kuna mtu anashida sana anahitaji maombezi. Asanteni kwa msaada wenu.
Nisaidie nabii wa mwisho kutumwana na Mungu hapa duniani alikuwa ni Muhammad, baada ya hapo Mungu hajatuma tena nabii. kasome vitabu utajua manabii wangi
 
Back
Top Bottom