Jamani wana JF, ninaomba mumsaidie huyu mama msaada wa kisheria jinsi gani apate talaka yake,
" Niliolewa ndoa ya kanisani 1999, nikazaa mtoto mwaka huo huo, tabia ya uzinzi ya mume wangu nikimfumania zaidi ya mara 3 na anakiri na kuomba msamaha, ugomvi, manyanyaso vilinifanya mwaka 2003 kurudi kanisani RC kuomba msaada. Wao walinielekeza nitafute ndugu zake wamwonye, hakusikia, hivyo 2003 nilirudi nyumbani na mtoto kuelezea tatizo. Wazazi walimwita ili aje asikie malalamiko yangu hakutaka kutokea na baada ya miezi 2 waliniambia nikachukue changu niondoke hapo, hakujali alisema niende tu hana shida na mimi. Hivyo miaka yote hii ninalea mtoto na nimekaa mwenyewe. Karibuni nimeona napoteza muda na ningependa kuolewa tena, kanisani wameniruhusu, ila nikavunje hiyo ndoa mahakamani.
Tatizo nimeanzia ustawi wa jamii wananiambia nimlete huyu mume hapo wakati mie sijui hata sasa hivi anaishi wapi, bahati nzuri karibuni nikaitwa na wenzie nikamuone amelazwa mgonjwa sana hospital, ila alipotoka tu sijui tena alipo. Sasa mie ombi langu ni nipate talaka yangu, je inawezekana niende mahakamani moja kwa moja na kudai bila hawa ustawi wanaonizungusha?
Pili kutokana na hali yake nadhani hataweza kusimama mahakamani, nami wala sintapenda kumsimamisha mgonjwa namuonea huruma je mahakama inaweza toa talaka hata kama mwingine hajulikani aliko?"
Mie sio mwanasheria msaada wenu please nimjibu nini, asante
" Niliolewa ndoa ya kanisani 1999, nikazaa mtoto mwaka huo huo, tabia ya uzinzi ya mume wangu nikimfumania zaidi ya mara 3 na anakiri na kuomba msamaha, ugomvi, manyanyaso vilinifanya mwaka 2003 kurudi kanisani RC kuomba msaada. Wao walinielekeza nitafute ndugu zake wamwonye, hakusikia, hivyo 2003 nilirudi nyumbani na mtoto kuelezea tatizo. Wazazi walimwita ili aje asikie malalamiko yangu hakutaka kutokea na baada ya miezi 2 waliniambia nikachukue changu niondoke hapo, hakujali alisema niende tu hana shida na mimi. Hivyo miaka yote hii ninalea mtoto na nimekaa mwenyewe. Karibuni nimeona napoteza muda na ningependa kuolewa tena, kanisani wameniruhusu, ila nikavunje hiyo ndoa mahakamani.
Tatizo nimeanzia ustawi wa jamii wananiambia nimlete huyu mume hapo wakati mie sijui hata sasa hivi anaishi wapi, bahati nzuri karibuni nikaitwa na wenzie nikamuone amelazwa mgonjwa sana hospital, ila alipotoka tu sijui tena alipo. Sasa mie ombi langu ni nipate talaka yangu, je inawezekana niende mahakamani moja kwa moja na kudai bila hawa ustawi wanaonizungusha?
Pili kutokana na hali yake nadhani hataweza kusimama mahakamani, nami wala sintapenda kumsimamisha mgonjwa namuonea huruma je mahakama inaweza toa talaka hata kama mwingine hajulikani aliko?"
Mie sio mwanasheria msaada wenu please nimjibu nini, asante