Phamarcist
JF-Expert Member
- Apr 18, 2021
- 211
- 449
Habari,
Wakati nchi inapitia vuguvugu la changamoto za kimkataba kati ya serikali yetu na kampuni ya DP WORLD. Na huku spin doctors wakijaribu kututoa kwenye reli nilikua naomba kufahamishwa yafuatayo.
Kuna tofauti gani kati ya kampuni ya TICTS ( Tanzania international container terminal service) na HUTCHINSON PORT OF TANZANIA,
Kwanini nimeuliza hivi, ni hivi TICTS ndiye aliyeingia mkataba na serikali ya Tanzania mwaka 2000 juu ya uendeshaji bandari kitengo cha makasha. Lakini kipindi chote hicho TICTS akiendelea na shughuli zake kuna kampuni ilionekana ndani ya TICTS ikiitwa Hutchinson port of Tanzania.
Kama kuna mtu aliwahi kupata zabuni yeyote enzi za TICTS basi atakua shahidi juu ya hili swala kwani kuna document zilizotoka TICTS lakini zikiwa zimepitishwa na Hutchinson port.
Swali la pili, ikitokea DP WORLD wakaanza kazi rasmi je, Hutchinson port wataendelea kuwepo kama walivyokua wakifanya kwa TICTS. Kwanini nimeuliza hivi, ni kwasababu enzi za TICTS Hutchinson port alifanya kazi pia ilihali hakua na mkataba wowote na serikali.
Je, Hutchinson port watafanya hivyo pia kwa DP WORLD?
Naomba kuwasilisha,
Wakati nchi inapitia vuguvugu la changamoto za kimkataba kati ya serikali yetu na kampuni ya DP WORLD. Na huku spin doctors wakijaribu kututoa kwenye reli nilikua naomba kufahamishwa yafuatayo.
Kuna tofauti gani kati ya kampuni ya TICTS ( Tanzania international container terminal service) na HUTCHINSON PORT OF TANZANIA,
Kwanini nimeuliza hivi, ni hivi TICTS ndiye aliyeingia mkataba na serikali ya Tanzania mwaka 2000 juu ya uendeshaji bandari kitengo cha makasha. Lakini kipindi chote hicho TICTS akiendelea na shughuli zake kuna kampuni ilionekana ndani ya TICTS ikiitwa Hutchinson port of Tanzania.
Kama kuna mtu aliwahi kupata zabuni yeyote enzi za TICTS basi atakua shahidi juu ya hili swala kwani kuna document zilizotoka TICTS lakini zikiwa zimepitishwa na Hutchinson port.
Swali la pili, ikitokea DP WORLD wakaanza kazi rasmi je, Hutchinson port wataendelea kuwepo kama walivyokua wakifanya kwa TICTS. Kwanini nimeuliza hivi, ni kwasababu enzi za TICTS Hutchinson port alifanya kazi pia ilihali hakua na mkataba wowote na serikali.
Je, Hutchinson port watafanya hivyo pia kwa DP WORLD?
Naomba kuwasilisha,