ARV
JF-Expert Member
- Sep 6, 2011
- 4,972
- 6,966
Ndugu yangu amepanga nyumba anakaa na familia yake,mkataba ni wa mwaka na ameshakaa miezi minne mpaka sasa.sasa mwenye nyumba juzi kabandika tangazo getini,akitangaza kusudio la kubadili matumizi ya nyumba kutoka nyumba ya makazi kuwa nyumba ya biashara, na imetakiwa kama kuna mtu ana kikwazo awasiliane na manispaa ndani ya mwezi mmoja.Je mpangaji ambaye tayari ana mkataba (umebakiza miezi 8)hapo inamhusu vipi?naombeni ushauri wandugu,je anatakiwa aende akaweke pingamizi au ubadilishaji huo wa matumizi utaanza baada ya mkataba kwisha?