Msaada: Anatumia kiwanja changu kuweza kufika kwake

Easement is a basic right in land ownership. Huna haki kisheria kumnyima njia. Fanya namba umuuzie.
 
Watu bwana. Ati weka ukuta. Hata jirani? Sasa atakuwa jirani wa JF? Zungumzeni. Mpe sehemu ya kupita, hata kama hawezi ku afford.
 
Watu bwana. Ati weka ukuta. Hata jirani? Sasa atakuwa jirani wa JF? Zungumzeni. Mpe sehemu ya kupita, hata kama hawezi ku afford.
Watu wakizibiana mwisho wa siku na yeye watamzibia. ..kukomoana
 
kuwa makini kama kiwanja kipo barabarani poa lakini kama kiko ndani tafuta jinsi ya kumaliza tatizo kwa amani, vinginevyo unaweza kumfungia mwenzio barabara na wewe wakakufungia barabara.
 
Saitot

Unaonekana huna maelewano mazuri na majirani zako..jambo dogo kama hili lakupita kwenye kiwanja linakushinda kutatua? Kwanini usikae nae mkaongea kama ndugu na majirani wenye mshikamano? Kwenye hili una haki kabisa lakini si kila jambo la kutumia nguvu za ziada! Nafikiri pia hakuna sababu ya kumzuia kupita ikiwa ujaanza kulitumia eneo! Hebu tafuta amani na majirani zako maana ukipatwa tatizo wao ndio watakusaidia...!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu weka ukuta lakini acha nafasi fulani kwa ajili ya jirani kupita. Kuna leo na kesho ie misiba ugonjwa nk.
 
Muuzie hyo njia,sio vizuri kuwa na uhasama na jirani yako.

Ushari wa ajabu sana huu! kwahiyo akishamuuzia njia hiyo hela ndo atatumia milele au? unahisi kufanya hivyo kutaleta suluhu? thamani ya ujirani itakuwepo tena?

Mkuu Saitot ulishaona wapi mtu kanunua njia ya kupita??? kiwanja chako kipo kwenye disorganized habitat, jifunze namna nzuri ya kuishi uswahilini vinginevyo hutakaa na amani!! tafuta eneo jingine uweka hiyo project yako.

Mpende jirani yako kama nafsi yako life is easy man!!!:confused: :what:
 
Last edited by a moderator:
Hayo ni mambo ya ujirani mwema mkae chini muongee kama ana tatizo na unaweza kumsaidia msaidie badala ya kumwacha anapata shida kufka kwake. Hapo anapopita kama bado eneo lako lina nafasi na yeye hana sehemu nyingine ya kumwezesha kufika kwake jaribu kuona namna utakavyomsaidia. Wote hamtazikwa hapo ya nini kujilisha upepo?

Kama ni unsurveyed area kwa maana ya kwamba eneo ambalo halijapimwa hayo ni mambo ya kawaida kutokea kwakuwa wauzaji huangalia pesa zaidi kila mtu anapokuja anauziwa ki vyake. Tafadhali usifanye kitu kitakachowajengea uhasama hasa kwakuwa hiyo hali ulisha ilea na baada ya muda ni kuwa inazoeleka na kuwa ni kawaida. Achana na wachonganishi na washauri wabaya wanaokwambia mara ujenge fensi au uchimbe mtaro. Siku utapata shida utahitaji msaasa wake utamwendeaje ili kumwomba akusaidie? Mpende jirani yako!
 
Hata ukiweka ukuta utakufa tu na kuviacha hapa duniani. Mpatie njia jirani yako kwani ndio ndugu yako
Ushauri mzuri sana huu. Wakati mwingine ukiangalia binadamu tunavyogombania ardhi na kujimilikisha utadhani tutadumu hapa duniani milele kumbe kaeneo tunakohitaji ni kadogo sana kakuchimbiwa shimo la kuzikwa. Na bahati mbaya yetu tukifa tunaondolewa pale tulipokuwa tunagombania na kupelekwa mbali kabisa wakati mwingine porini na kuzikwa huko. Biblia inasema amelaaniwa yule agombaniaye ardhi.

Kweli ni laana. Tukifa tunachimbiwa chini ya ardhi na kuzikwa huko hivyo ardhi inatumeza na kupotea kabisa juu ya uso wa dunia. Itatufaa nini kugombania ardhi ambayo kwayo tunapita tu? Nikifaika hapa huwa namkumbuka sana Nyerere alijua kuwa duniani tunapita tu. Enzi zake hakukuwa na mtu wa kumhoji hivyo angeweza hata kuambua kuchukua ardhi yote kutoka Ubungo mpaka Kiluvya na likaitwa eneo la rais.

Nani angeligusa? Lakini mzee akapiga kazi pale akarudi zake kijijini kwake ha hatimaye kuzikwa huko. Ingemfaa nini leo kama angejimilikisha ardhi kubwa kama nilivyo sema halafu kumbe hatuwezi kuishi hata miaka 100. Samba Mapangala anasema dunia tunapita, binadamu ni mchanga, ... itabaki milele ni milima... Ubarikiwe mkuu.
 
Ushari wa ajabu sana huu! kwahiyo akishamuuzia njia hiyo hela ndo atatumia milele au? unahisi kufanya hivyo kutaleta suluhu? thamani ya ujirani itakuwepo tena?

Mkuu Saitot ulishaona wapi mtu kanunua njia ya kupita??? kiwanja chako kipo kwenye disorganized habitat, jifunze namna nzuri ya kuishi uswahilini vinginevyo hutakaa na amani!! tafuta eneo jingine uweka hiyo project yako.

Mpende jirani yako kama nafsi yako life is easy man!!!:confused: :what:

Umenena vema mkuu. Mungu akubariki. Haya matatizo ni makubwa sana hasa maeneo ambayo hayajapimwa na kuna watu wengine wabishi, wakorofi na wamejaa roho mbaya ambapo wapo radhi kuona jirani zao wanateseka kwa kuwanyima kaendeo kadogo tu kakuwafanya wapumue au kupita. Inahitaji busara sana inapotokea tatizo kama hili. Lazima kujenga ujirani mwema kwa kuangalia namna ya kusaidiana.

Wengine wamejaa roho mbaya kazi kuchonganisha watu kwa kuwaambia eti achimbe mtaro au ajenge ukuta. Ajenge ukuta au achimbe mtaro siku akifa watamtoa huko juu kwa juu na kumpeleka porini kabisa au sehemu pweke kabisa kisha kuchimba shimo na kumfukia humo. Hiyo ndiyo laana ya ardhi. Tunapita na kuzunguka zunguka hapa duniani juu ya ardhi kwa muda tu halafu tunamezwa na ardhi hiyo hiyo tunayogombea.

Yaani maisha yetu hayafiki hata miaka 100 lakini makeke tunayofanya juu ya ardhi utadhani tupo hapa milele. Unaweza kukuta wahusika umri wao walioishi hawawezi kuishi tena mara mbili yake yaani miaka iliyobaki kabla hawajafutika juu ardhi haizidi hiyo waliyokwisha kuishi. Upendo tu ndio dawa ya yote hasa tunapomalizia ka muda kadogo kaliko baki kabla hatujamezwa na ardhi hiyo hiyo tunayogombea au kujidai kuweka fensi na kuchimba mitaro.
 
Ushauri mzuri sana huu. Wakati mwingine ukiangalia binadamu tunavyogombania ardhi na kujimilikisha utadhani tutadumu hapa duniani milele kumbe kaeneo tunakohitaji ni kadogo sana kakuchimbiwa shimo la kuzikwa. Na bahati mbaya yetu tukifa tunaondolewa pale tulipokuwa tunagombania na kupelekwa mbali kabisa wakati mwingine porini na kuzikwa huko. Biblia inasema amelaaniwa yule agombaniaye ardhi. Kweli ni laana. Tukifa tunachimbiwa chini ya ardhi na kuzikwa huko hivyo ardhi inatumeza na kupotea kabisa juu ya uso wa dunia. Itatufaa nini kugombania ardhi ambayo kwayo tunapita tu? Nikifaika hapa huwa namkumbuka sana Nyerere alijua kuwa duniani tunapita tu. Enzi zake hakukuwa na mtu wa kumhoji hivyo angeweza hata kuambua kuchukua ardhi yote kutoka Ubungo mpaka Kiluvya na likaitwa eneo la rais. Nani angeligusa? Lakini mzee akapiga kazi pale akarudi zake kijijini kwake ha hatimaye kuzikwa huko. Ingemfaa nini leo kama angejimilikisha ardhi kubwa kama nilivyo sema halafu kumbe hatuwezi kuishi hata miaka 100. Samba Mapangala anasema dunia tunapita, binadamu ni mchanga, ... itabaki milele ni milima... Ubarikiwe mkuu.

Mtoa mada isipo mgusa sijui. Mimi nina mfano hai tena wa tarehe 11/06/2015 mwaka huu tena juzi tu jumapili nilimuomba njia jirani yangu kwa moyo wake alisema pima kiasi unachotaka maana hata ukikataa utakufa na kuacha kila kitu huwezi amini yule jirani siku hiyohiyo aliacha wosia kuhusu ile njia kwa ndugu zake na jumatatu ya tarehe 12/06/2015 akafariki ghafla na kwenda kuzikwa Mtwara wakati yeye maisha yake yalikuwa Dar. Mkuu watu hawalioni hilo.
 
Kwa sababu umeshasema ana kiburi wala usithubutu kumuuzia njia maana anaweza hata kupageuza hapo liwe jalala au akajenga choo mshenzy ili akutibue tu si patakua kwake? Kama una uwezo mpe njia bure.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom