Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 734
KOCHA wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 23, Jamhuri Kiwhelu 'Julio' ameongeza wachezaji saba katika kikosi chake ili kukiongezea nguvu kwa ajili ya mchezo wao wa marudiano wa kutafuta nafasi ya kucheza mashindano ya Olimpiki dhidi ya timu ya Cameroon utakaofanyika Jumamosi hii kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mwananchi kwa niaba ya kocha huyo msemaji wa Shirikisho la soka nchini, Boniface Wambura alisema kulingana na umuhimu wa mchezo huo kocha wa timu hiyo ameongeza wachezaji saba katika kikosi hicho.
Wambura aliwataja wachezaji hao kuwa ni Mrisho Ngasa kutoka katika timu ya Azam ,Kigi Makasi wa Yanga ,David Luhende kutoka katika timu ya Kagera Sugar ,Jabiri Azizi wa Azam, Calvin Charles wa Simba Ally Lundenga wa Kagera Sugar na Juma Abdul wa mtibwa Sugar.
"Kulingana na umuhimu wa mchezo huo mwalimu ameona aongeze nguvu kwa kuwaita wachezaji hao, Kwa kuwa kigezo cha kucheza katika timu ya vijana ni umri hivyo hilo la kuwaongeza wachezaji hao siyo tatizo,"alisema Wambura.
Wakati huo huo, Shirikisho la Soka Tanzania TFF limetangaza viingilio vya mechi hiyo ambapo kiingilio cha juu kitakuwa ni shilingi 10,000 na kiingilio cha chini ni shilingi 1000.
Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema mashabiki watakaokaa kwenye viti vya kijani, bluu na rangi ya chungwa ndio watalipa shilingi 1000.
Alifafanua kuwa mashabiki watakaokaa VIP B na C kiingilio kitakuwa ni shilingi 5000 na jukwaa la VIP A lenye viti 745 kiingilio kitakuwa ni shilingi 10,000.
Alisema kuwa tiketi za mchezo huo ambao utapigwa kwenye uwanja wa taifa kuanzia saa kumi jioni zinauzwa katika vituo vya OilCom Ubungo ,Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa ,Mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora na Ohio.Aidha aliyataja maeneo mengine ambayo tiketi hizo zinauzwa kuwa ni pamoja na Big Bon Msimbazi Kariakoo na Uwanja wa Uhuru.
Alisema kuwa timu ya Kameroon imewasili juzi saa tano usiku na ndegeya Kenya Air Ways ikiwa na wachezaji 23 na imefikia katikas Hoteli ya Paradise
iliyopo Posta Jijini Dar es Salaam na itakuwa inafanya mazoezi katika uwanja wa Karume.
Akizungumza na Mwananchi kwa niaba ya kocha huyo msemaji wa Shirikisho la soka nchini, Boniface Wambura alisema kulingana na umuhimu wa mchezo huo kocha wa timu hiyo ameongeza wachezaji saba katika kikosi hicho.
Wambura aliwataja wachezaji hao kuwa ni Mrisho Ngasa kutoka katika timu ya Azam ,Kigi Makasi wa Yanga ,David Luhende kutoka katika timu ya Kagera Sugar ,Jabiri Azizi wa Azam, Calvin Charles wa Simba Ally Lundenga wa Kagera Sugar na Juma Abdul wa mtibwa Sugar.
"Kulingana na umuhimu wa mchezo huo mwalimu ameona aongeze nguvu kwa kuwaita wachezaji hao, Kwa kuwa kigezo cha kucheza katika timu ya vijana ni umri hivyo hilo la kuwaongeza wachezaji hao siyo tatizo,"alisema Wambura.
Wakati huo huo, Shirikisho la Soka Tanzania TFF limetangaza viingilio vya mechi hiyo ambapo kiingilio cha juu kitakuwa ni shilingi 10,000 na kiingilio cha chini ni shilingi 1000.
Afisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema mashabiki watakaokaa kwenye viti vya kijani, bluu na rangi ya chungwa ndio watalipa shilingi 1000.
Alifafanua kuwa mashabiki watakaokaa VIP B na C kiingilio kitakuwa ni shilingi 5000 na jukwaa la VIP A lenye viti 745 kiingilio kitakuwa ni shilingi 10,000.
Alisema kuwa tiketi za mchezo huo ambao utapigwa kwenye uwanja wa taifa kuanzia saa kumi jioni zinauzwa katika vituo vya OilCom Ubungo ,Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa ,Mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora na Ohio.Aidha aliyataja maeneo mengine ambayo tiketi hizo zinauzwa kuwa ni pamoja na Big Bon Msimbazi Kariakoo na Uwanja wa Uhuru.
Alisema kuwa timu ya Kameroon imewasili juzi saa tano usiku na ndegeya Kenya Air Ways ikiwa na wachezaji 23 na imefikia katikas Hoteli ya Paradise
iliyopo Posta Jijini Dar es Salaam na itakuwa inafanya mazoezi katika uwanja wa Karume.