Uchaguzi 2020 Mpaka sasa Rais Magufuli ameshakiuka kwa kiwango kikubwa sana ahadi yake ya kuwepo uchaguzi wa huru na haki. Najua alichowaza mpaka akaahidi hivyo

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Zipo ishara za wazi sana kuwa Rais Magufuli anaenda kushughulikiwa vilivyo na jumuiya za kimataifa na litakalotokea mpaka watanzania wenyewe watashangaa.

Nimemsoma Dr. Christopher pahala (Huyu ni mbobezi wa mambo ya uchaguzi Afrika) anasema wazi kuwa ipo hofu Tanzania kuwa kama Zimbabwe baada ya huu uchaguzi mkuu ujao. Hili hata mimi sina shaka nalo kabisa. Tumejijengea heshima ya hovyo mbele ya mataifa wenzetu ambayo hapo kabla walituona kama mfano halisi wa ukuaji wa demokrasia.

Rais Magufuli aliahidi kuwa uchaguzi mkuu utakuwa huru na wa haki baada ya kujiaminisha kuwa wapinzani walishajifia na hakuna mtanzania atakayewaunga mkono. Alijiamini kuwa ameleta maendeleo sanaaa hivyo atakubalika kirahisi yeye pamoja na wagombea wenzake wa CCM.

Kwanza kushindwa kuujua ukweli huko ardhini ni udhaifu mkubwa sana kwa kiongozi anayejidai kujiamini. Amelazimika kuikana ahadi yake ya uchaguzi kuwa huru na wa haki. Amelazimika tena hadharani na ameenda mbali zaidi hata kuonekana kituko mbele ya jamii.

Tuseme ukweli, kama siyo uthubutu binafsi wa Tundu Lissu na Maalim Seif basi yaliyotokea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa yangekuwa yaleyale ya uchaguzi mkuu. Hawa watu wamepigana kweli kweli na nadiriki kusema kuwa wamevishinda vita.

Aidha kuna haja ya kumshukuru sana Tundu Lissu kwani kwenye huu uchaguzi "ame act" kama kiongozi mkuu wa watanzania. Amezijua shida za watanzania kwa muda mfupi kuliko Rais waliyekuwa naye kwa miaka mitano. Amefanya tuone kumbe Rais alikuwa hafanyi chochote kile kwa ustawi wa maendeleo ya watanzania. Alijielekeza kwenye mambo yake binafsi anayoyajua yeye.

RAI YANGU:
Magufuli be careful and watch iti! Hizo nguvu unazodhani unazo, huna! Na zaidi watakaoumia ni watanzania na nikueleze wazi kuwa kwa yanayoendelea huko mikoani mpaka sasa unaonekana huna ukaribu na watanzania wengi. Huo ndiyo ukweli wenyewe na ukitaka umeze au uteme ila utabaki kuwa hivyo.
 
Kuliko watanzania tufe kwa kuwekewa vikwazo Kama Zimbabwe ni Heri Yona atoswe baharini Melikenu isizame!
The conduct of the upcoming elections in Tanzania has important consequences not only for Tanzania, but for the entire East African region. Tanzania’s history of peaceful multi-party elections stretching back 25 years has made it a model on the continent.

The United States government reaffirms unequivocally that it does not support any specific candidate or party in Tanzania’s upcoming elections. The United States supports the democratic process itself. We support a genuinely free, fair, transparent, and peaceful electoral process, before, during, and after election day. This includes ensuring the safety of all contestants, respect for the rule of law, and the absolute impartiality of the authorities in charge of managing the elections.

The United States, along with other democratic nations, will be paying close attention to actions of individuals who interfere in the democratic process or instigate violence against the civilian population before, during, or after the elections. We will not hesitate to consider consequences for those found to be responsible for election-related violence or undermining the democratic process.

We welcome the calls by the leading candidates for a peaceful and transparent electoral process, and we urge them and their supporters to take measures to decrease tensions and avoid inciteful rhetoric.

By U.S. Embassy Dar es Salaam | 1 October, 2020 | Topics: Press Releases
 
Watanzania tuamke, ukitolewa wito na viongozi wetu tusimame kwa pamoja kudai haki yetu ikibidi.Go Lissu tunahitaji Taifa huru kweli kweli, sio hisani na maelekezo mfalme. Viongozi wawajengee uwezo elimu kudai haki yao endapo haki yao itaporwa ktk sanduku la kura.
 
Unamtisha wewe kama nani?

Subiri tareh 28 tuwanyoe kwa chupa
 
Fanyeni sasa

Wewe mtu mmoja unakuja kujibu comment moja badala ya nyingine, hujishtukii mzee?? Mfaidika nini wa ujinga unaondelea? Acheni kudanganywa kwamba mnaweza kujiendesha wenyewe fatlia Zimbabwe kwa umakini ndo utajua nguvu za hao mnaowaita mabeberu.
 
Back
Top Bottom