Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 4,436
- 4,151
Tatizo kubwa ni unafiki wa huyu mzee sitta kila wakati atakuwa kwenye hii hali, ukiamua usafi ni kwa asilimia 100, yeye analaumu tu kila kukicha, hili hali wengine ideology zetu ni 'no one is clean in ccm' aondoke tu ccm atafute sehemu nyingine, akishindwa akae kimya!!!!! yeye hana usafi wowote ule kutaka tu publicity, aacha upropaganda wake. unalaumu weee unabaki humo humo, akili hizo!!
Sidhani kama ni unafiki tu wala sidhani kama Sitta hajui kama wapo wengi wanaojua kwamba na yeye si safi. Tatizo kubwa ni kwamba hivi sasa kuna ombwe kubwa la uongozi ndani ya chama (CCM) na serikali yake kiasi kwamba watu kama akina Sitta wanapata jeuri ya "kumwaga mboga au ugali" wanapojisikia bila wasiwasi wa kuwajibishwa. Nisahihishwe. Kinachoonekana ni kwamba uongozi wa chama umegubikwa na "shaka kubwa la ukosaji" (guilty conscious) kiasi cha kukosa ubavu wa kuwawajibisha wale wote wanaokitia kidole machoni. Ni kama vile Sitta anawaambia "mtanifanya nini?" Kazi kwenu wana-CCM! arty: